HISTORIA (WASIFU WA) YA MAREHEMU DKT. WILLIAM AUGUSTAO MGIMWA

Similar documents
HOTUBA YA WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS IKULU NA UTAWALA BORA MHESHIMIWA DKT. MWINYIHAJI MAKAME

KWA VILE ni kanuni ya Kanisa Anglikana ulimwenguni ambalo ni sehemu ya Kanisa Katholiko kwamba Dayosisi kadhaa ziungane pamoja na kuunda Jimbo;

Taarifa ya Utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM (Oktoba, 2010 hadi Septemba, 2012) kuhusu Zanzibar SERIKALI YA MAPINDUZI YA ZANZIBAR

UCHAMBUZI MUUNGANO WA TANZANIA YA MWAKA 1977

PROPOSED STANDARD COUNCIL LEVEL HOSPITALS. Schedule of Material, Labour & Drawings for Septic and Soak way pit PROJECT AREA TANZANIA MAINLAND

Learning by Ear Unce upon a time... in Africa Episode 3: TRADE IN AFRICA. Author: Marta Barroso Editors: Maja Braun, Jan-Philipp Scholz CHARACTERS:

DEFERRED LIST ON 23/10/2018

Learning by Ear Once upon a time... in Africa Episode 8: COLONIALIZATION. Author: Marta Barroso Editors: Maja Braun, Jan-Philipp Scholz CHARACTERS:

JAMUHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA RAIS TAMISEMI

Learning by Ear Once upon a time... in Africa Episode One: CRADLE OF MANKIND. Author: Marta Barroso Editors: Maja Braun, Jan-Philipp Scholz

KUFANIKISHA MAGEUZI YA SHERIA ZA KUMILIKI ARDHI NCHINI KENYA TOLEO MAARUFU LA MSWADA WA KUMILIKI ARDHI YA JAMII

Cambridge International Examinations Cambridge Ordinary Level

SIMON & SCHUSTER S PIMSLEUR SWAHILI 1 READING BOOKLET

Remarks You Must Read & Know Before Buying Guingamp vs RC Strasbourg Tickets: Event date and time are subject to change - these changes are not

TOKA SABATO KWENDA JUMAPILI CARLYLE B. HAYNES

UCHANGANUZI WA MAKOSA YA KISARUFI KATIKA INSHA ZA WANAFUNZI WA SHULE ZA MSINGI NA YANAVYOCHANGIA MATOKEO MABAYA YA MITIHANI, KATA YA GANZE, KAUNTI

CROP PROTECTION PROGRAMME. Identifying the factors causing outbreaks of armyworm as part of improved monitoring and forecasting systems

unajua ulichofanya; umevumilia Vema ninataka umwambia Shetani katika jina la Yesu anapokufanyia jambo baya, Toka! Toka!

2017 Student Program Curriculum

THE SPINE CLINIC. Spine Care. Huduma Ya Uti Wa Mgongo Kanuni Za Kutunza Shingo Na Mgongo. principles of neck and back care IOM SYSTEM ENDOSCOPE

Ikimbieni Zinaa. Ellis P. Forsman. Ikimbieni Zinaa (Flee Fornication) 1

NOVENA YA ROHO MTAKATIFU

Pasaka Na Meza Ya Bwana Sehemu Ya 2

Ni Nani Aliye Upande Wa Bwana?

Lesson 60: Quantifiers OTE and O OTE

Hennepin County Kiongozi cha jinsi ya kuondoa taka

Mbeya City FC x Mtibwa Sugar Online stream tv today WATCH HERE LINK

U.S. Overview. Gathering Steam? Tuesday, October 1, 2013

EXL6 Swahili PhraseBook Davis

Postgraduate Taught Tuition Fees for 2013 entry

The history of Zaire as told and painted by Tshibumba Kanda Matulu in conversation with Johannes Fabian

Graduate Student Enrollment

Mayor and Councillors COUNCIL 28 JUNE 2012

Bellville GC Membership Fees 2018

Bellville GC Membership Fees 2019

As long as anyone can remember, we have tilled the fields in our

More of the Same; Or now for Something Completely Different?

Fee Table:1 - Ph.D. Programmes (Full Time and Part-Time Internal)

The Mystery of Growing Foreign Exchange Reserve

Kilometer Time Trial Session #1 - Friday - July 20, Redmond, WA kph

Japan Salary Benchmark 2018

The Cantonal Government

27 February 28 February 2012 or 12 March - 13 March 2012 ICC Headquarters 38, Cours Albert 1er, Paris - France

ABA Commercial Real Estate Lending Committee

Debenture Servicing Audit

Government of India Ministry of Youth Affairs & Sports Department of Sports

Trends in SE DHIA Dairy Industry, and SE DHIA Awards

HEALTH AND COMMUNITY DESIGN IN BEACON HILL, SEATTLE, WA

President and Chief Executive Officer Federal Reserve Bank of New York Washington and Lee University H. Parker Willis Lecture in Political Economics

KENYA INSTITUTE OF CURRICULUM DEVELOPMENT EDU CHANNEL TV BROADCAST LINE UP AUGUST DEC 2017 WEEKLY TV PROGRAMMES

Cadaretta Wine & Golf Camp Information Sheet, Itinerary, & Bios

Muhlenkamp & Company. Webinar December 1, Ron Muhlenkamp, Portfolio Manager Jeff Muhlenkamp, Portfolio Manager Tony Muhlenkamp, President

Tamilnad Mercantile Bank Ltd., Head Office, Thoothukudi Applicable ROI Minimum and Maximum for Investment Grade Loans Non-Agri Schemes.

No. 2-3/2013-SP-IV Government of India Ministry of Youth Affairs & Sports Department of Sports

EXPERT GLOBAL TRUSTED

Volleyball Coaching Manual READ ONLINE

STRATEGIC REVIEW OF ATHLETICS TERMS OF REFERENCE

The outlook: what we know, the known unknowns and the unknown unknowns

MRCPI General Medicine Calendar

Postgraduate Programmes Registration and Welcome Presentation Schedule 2018

WORLD. Geographic Trend Report for GMAT Examinees

6 th April, 2018 Current Affairs Questions for Bank (IBPS Clerk, IBPS PO, RBI Grade-B, SBI Clerk & SBI PO) and Railways Exams

streetfootballworld Festival 2015

Economic Outlook: fear over fundamentals

Virginia International University

Comparison of fees at Strathclyde and other universities. Postgraduate taught fees for 2017 and 2018 entry

MRCPI General Medicine Calendar

Safety & Efficacy of TAE for LGIB

TANZANIA BUREAU OF STANDARDS

KARATE TSHWANE ELITE AND DEVELOPMENT CHAMPIONSHIPS

Household Wealth: Panel Study of Income Dynamics (Thousands of 1999 dollars)

Principal Operations in Japan

Pearson Edexcel Price List January 2018 Bangladesh

SPORTS AUTHORITY OF INDIA NETAJI SUBHAS NATIONAL INSTITUTE OF SPORTS PATIALA SYLLABUS FOR DIPLOMA IN COACHING

Other Transporation Accommodation Meals Subtotal Other Expenses Total

Hanshi Sadashige Kato. International Japan Karate-do Association & IJKA Bulgaria

Heidrun Kröger, SIL Southern Africa for Bantu 6 in Helsinki,

December 13, Governor Deval Patrick Massachusetts State House Office of the Governor, Room 280 Boston, MA Dear Governor Patrick:

Educating the next generation of Leaders in Sport Management. Postgraduate Diploma in Football Business JOHAN CRUYFF INSTITUTE. Barcelona,

SA economic review Kevin Lings. August 2018

SADTA in conjunction with and recognised by IDTA Proudly Presents SOUTH AFRICAN FREESTYLE. C hampionships

This table has been produced by. The State & Regional Fiscal Studies Unit, University of Missouri-Columbia

Facilities Master Plan 2013 Update CWU / City / County / Community Planning Forum Mary Grupe Conference Center By Campus Development Committee March

Chief Operating Officer Approved by. Responsible Officer. Vice-Chancellor Approved and commenced 25 September, 2017 Review by September, 2020

Selected Interest & Exchange Rates

Fish or Cut Bait! The Case for Individual Transferable Quotas in the Salmon Fishery of British Columbia. edited by Laura Jones and Michael Walker

Renewable Power & Smart Grid Community Partnership

PROPOSED HIGH STREET TRAFFIC CALMING PLAN

2016 Kids Marathon Training Packet

Position Description

Israel Innovation Authority

TRIATHLON WA 2018 BOARD NOMINEE PROFILES

What can National Membership do for You?

Food and Drug Administration Center for Devices an d * 1Ya I a Radiological Health WARNING LETTE R

United States Lifesaving Association

Jim Richardson hired as HEDC CEO. Inside This Issue: PwC completes report on business transitions

Debenture Servicing Audit Follow Up June 28, 2007

BULLETIN POLISH OPEN WKF X INTERNATIONAL KARATE GRAND PRIX BIELSKO-BIAŁA

Puget Sound Regional Forecast Chris Mefford Community Attributes

REPORT ON CONSULTATION MEETINGS HELD WITH THE PEMBA CHANNEL CONSERVATION AREA DISTRICT COMMITTEES ON ESTABLISHING NO-TAKE FISH BREEDING GROUNDS

Transcription:

HISTORIA (WASIFU WA) YA MAREHEMU DKT. WILLIAM AUGUSTAO MGIMWA (MB) ALIYEKUWA WAZIRI WA FEDHA KATIKA SERIKALI YA AWAMU YA NNE YA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA 1. KUZALIWA Marehemu Dkt. William Augustao Mgimwa alizaliwa tarehe 20 Januari, 1950 katika kijiji cha Magunga, mkoa wa Iringa. 2. ELIMU Marehemu Dkt. William Mgimwa alianza elimu ya msingi katika shule ya Msingi WASA mwaka 1961 hadi 1965. Alijiunga na shule ya kati (Middle School) ya Tosa kuanzia mwaka 1965 hadi mwaka 1967. Kwa upande wa elimu ya sekondari, marehemu Dkt. Mgimwa alisoma katika shule ya Seminari ya Tosamaganga mwaka 1968 mpaka 1969 na shule ya Seminari ya Mafinga mwaka 1970 hadi 1971. Mwaka 1975 hadi mwaka 1978, marehemu Dkt. Mgimwa alisomea na kupata stashahada (Advanced Diploma) ya masuala ya kibenki katika Chuo cha Usimamizi wa Fedha -IFM. Mwaka 1983 hadi 1984 alipata Postgraduate Diploma, ya masuala ya fedha katika Chuo cha Usimamizi wa Fedha. Mwaka 1989 hadi 1991, marehemu Dkt. Mgimwa alisoma na kupata Shahada ya Uzamili (MBA-Finance) ya masuala ya fedha katika Chuo cha Uongozi Mzumbe, wakati huo kikiitwa Institute of Development Management(IDM). 1

Mwaka 2003, marehemu Dkt. Mgimwa alitunukiwa Shahada ya juu ya Uzamivu ya Masuala ya Fedha yaani Doctor of Philosophy (Ph.D) in Finance Aidha, marehemu Dkt. Mgimwa amehudhuria mafunzo mbalimbali ya masuala ya fedha ndani na nje ya nchi pamoja na kupelekwa Attachment kumjengea uwezo katika Taasisi mbalimbali zikiwemo; Bank of England mwaka 2001, Chuo cha Benki ya ABSA, Afrika Kusini, 2000, Chuo cha Benki Kuu ya India,2003 IMF, Washington, 2001 Bank for International Settlement, Switzerland Kwa watumishi wengi nchini na hasa wale wa mabenki na vyombo mbalimbali vya fedha watamkumbuka marehemu Dkt. Mgimwa kama Mwalimu na Mlezi. Mbali na kufundisha, marehemu Dkt. Mgimwa ameandika na kuhariri vitabu kadhaa vikiwemo Advanced Credit Operations 2006/7 na Advanced Treasury Management 2008/9. Aidha, Marehemu Dkt. Mgimwa amechapisha makala kadhaa yanayohusu sekta ya uchumi na fedha katika majarida mbalimbali ndani na nje ya nchi. 3. AJIRA Kuanzia mwaka 1980 hadi 1981, marehemu aliajiriwa na kufanya kazi katika Benki ya Taifa ya Biashara (National Bank of Commerce-NBC) kama Mhasibu (Bank Accountant). Mwaka 1981 alihamishiwa Tawi la NBC Mtwara akiwa Meneja wa Tawi (Branch Manager) 2

Mwaka 1982 hadi 1989, alifanya kazi kama Mhadhiri (Instructor/Trainer) katika Chuo cha Benki ya Taifa ya Biashara (NBC) Iringa. Mwaka 1996 hadi 1997 alikuwa Meneja Mkuu (Chief Manager) wa Benki ya Taifa ya Biashara(NBC), akishughulikia Mafunzo na Bajeti. Mwaka 1997 hadi 2000, alipanda cheo na kuwa Mkurugenzi (Director of Corporate Services) katika benki hiyo hiyo ya NBC, akishughulikia masuala ya Usimamizi wa mikopo na operesheni za Kimataifa. Mwaka 2000 hadi 2010, aliajiriwa Benki Kuu ya Tanzania akiwa Mkurugenzi na Mkuu wa Chuo cha Benki Kuu ya Tanzania (BoT) kilichopo jijini Mwanza. Kuanzia Mei, 2012 alikuwa Waziri wa Fedha hadi mauti yalipomkuta. 4. MAISHA YA SIASA Kati ya mwaka 1991 hadi 1994, marehemu Dkt. W. Mgimwa alikuwa Diwani wa Kata ya Gangilonga, mkoani Iringa kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi. Mwaka 1994 hadi 1995 alikuwa Kamanda Msaidizi wa Umoja wa Vijana wa CCM (UVCCM) Iringa. Kuanzia mwaka 2008 hadi 2010 alikuwa Mlezi wa Kata ya Wasa mkoani Iringa. Mwaka 2010 hadi 2014 mauti yalipomkuta, marehemu alikuwa Mbunge wa jimbo la Kalenga mkoani Iringa. Aidha, baada ya kuchaguliwa kuwa mbunge, Marehemu Dkt. Mgimwa amekuwa Mjumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge iliyokuwa ya Fedha na Uchumi. Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania alimteua Dkt. William A. Mgimwa kuwa Waziri wa Fedha kuanzia mwezi Mei 2012. 3

Kwa wadhifa wake aliokuwa nao ulimfanya pia awe;pamoja na nyadhifa nyingine: Mjumbe wa Baraza la Kisekta la Mawaziri wa Fedha wa Jumuiya ya Afrika Mashariki kuhusu Masuala ya Fedha na Uchumi, Gavana katika Benki ya Dunia, Gavana wa Shirika la Fedha la Kimataifa IMF, Gavana wa Benki ya Maendeleo ya Afrika, ADB, Mjumbe wa Baraza la Uongozi (Governing Council) la Benki ya Maendeleo ya Afrika Mashariki (EADB), na Mjumbe wa Bodi ya Uongozi ya PTA Bank. Kutokana na ujuzi na uzoefu wake, marehemu Dkt. Mgimwa amekuwa akitoa mchango mkubwa na kupewa nafasi za kuwa mwenyekiti na mzungumzaji mkuu kwenye mikutano ya kimataifa. 5. KUUGUA Marehemu Dkt. William Mgimwa alienda nchini Afrika ya Kusini kuanzia tarehe 3 Novemba, 2013 kwa ajili ya uchunguzi wa kawaida wa afya yake katika Hospitali ya Kloof Medi Clinic iliyoko Pretoria. Baada ya Uchunguzi Madaktari walishauri alazwe kwa uangalizi zaidi na matibabu. Akiwa amelazwa Hospitalini, aliendelea na matibabu hadi mauti ilipomfika kutokana na tatizo la figo. 6. KUFARIKI Marehemu Dkt. W. Ngimwa alifariki Mwaka Mpya, Jumatano tarehe 1 Januari 2014 saa 6.25 mchana saa za Afrika Mashariki katika Hospitali hiyo ya Kloof Medi- Clinic. 4

7. HITIMISHO Marehemu Dkt. William Mgimwa ameacha Mjane Bi. JANE KAKINGU na watoto saba (7) ambao ni MARIO, FLORA, GODFREY, FELIX, SCOLA, JAMES na DENNIS. BWANA AMETOA NA BWANA AMETWAA, JINA LA BWANA LIHIMIDIWE +++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++ 5