UCHANGANUZI WA MAKOSA YA KISARUFI KATIKA INSHA ZA WANAFUNZI WA SHULE ZA MSINGI NA YANAVYOCHANGIA MATOKEO MABAYA YA MITIHANI, KATA YA GANZE, KAUNTI

Size: px
Start display at page:

Download "UCHANGANUZI WA MAKOSA YA KISARUFI KATIKA INSHA ZA WANAFUNZI WA SHULE ZA MSINGI NA YANAVYOCHANGIA MATOKEO MABAYA YA MITIHANI, KATA YA GANZE, KAUNTI"

Transcription

1 UCHANGANUZI WA MAKOSA YA KISARUFI KATIKA INSHA ZA WANAFUNZI WA SHULE ZA MSINGI NA YANAVYOCHANGIA MATOKEO MABAYA YA MITIHANI, KATA YA GANZE, KAUNTI YA KILIFI, KENYA. ROSE SULUBU KITSAO Tasnifu imewasilishwa katika Kitivo cha Sanaa na Sayansi Jamii ili kutosheleza baadhi ya mahitaji ya Shahada ya Uzamili (Kiswahili) ya Chuo Kikuu Cha Pwani, Kenya. AGOSTI, 2015.

2 i UNGAMO NA IDHINI. Ungamo. Kazi hii ya utafiti ni yangu mwenyewe na haijawahi kutolewa katika chuo chochote kwa mahitaji ya Shahada yoyote ya Uzamili. Sahihi: Tarehe: Rose Sulubu Kitsao Mtahiniwa Idhini. Kazi hii imetolewa kwa idhini yetu, tukiwa wasimamizi walioteuliwa rasmi na Chuo Kikuu cha Pwani, Kenya. 1. Prof. R.M Chimerah Sahihi: Tarehe: 2. Prof. S. K. Beja Sahihi: Tarehe:

3 ii TABARUKU Kwa mume, watoto, ndugu na marafiki zangu.

4 iii SHUKRANI Ninamshukuru Mwenyezi Mungu kwa kunipa uhai na kunilinda katika hali zote zilizonikumba katika safari yangu ya kupata Shahada ya Uzamili.Wasimamizi wangu wakiwa Prof.R.M Chimerah na Prof. S.K. Beja nawapa mkono wa shukrani kwa kunielekeza vyema katika kazi yangu ya utafiti,mungu awabariki na awainue siku baada ya nyingine. Miongoni mwa walimu walionipa elimu ya Shahada ya Uzamili na mawaidha mbalimbali ni Bi. Nancy Ngowa, Bw. Nicholus Malau, Bw.Ndiso, Bw. Tunje, na Bw. Marifa, Mungu awabariki vilivyo. Zaidi namshukuru mume wangu Bw. Festus Mbaru, watoto wangu, Gladys, Queenter, Faith na Emmanuel kwa maombi na uvumilivu wa upweke wakati nilipokuwa Chuoni na nyanjani kung ang ania Shahada.Wengine walioniombea ni mama yangu mpendwa, Tabitha Kadzo, dada na kaka zangu, Mungu awabariki. Wale wote walionyosha mkono na kunisaidia kifedha na kimawazo, Mungu awajalizie marudufu. Nawashukuru ndugu zangu wa Baraka Bureau katika kata ya Kaloleni, ndugu William Salania na Brian Kazi kwa msaada walionipa wa uchapishaji wa utafiti na utoaji wa nakala. Mola azidi kukuza talanta yao. Mwisho kabisa, shukrani zangu ni kwa wote waliojihusisha kwa hali moja au nyingine ili kufanikisha kazi hii, Mungu awazidishie wote.

5 iv IKISIRI. Utafiti huu umeshughulikia uchanganuzi wa makosa ya kisarufi katika insha za Kiswahili za wanafunzi wa darasa la nane na jinsi yanavyochangia matokeo mabaya ya mitihani katika kata ya Ganze, kaunti ya Kilifi, nchni Kenya. Mtafiti alipata ari ya kufanya utafiti huu wakati alipofahamu ya kwamba kuna malalamishi kutoka kwa washikadau wa elimu kuwa matokeo mabaya ya mtihani wa Kiswahili yamekuwa yakidhihirika kwa muda mrefu, wakidai kuwa makosa ya kisarufi ni mojawapo ya sababu za matokeo mabaya. Madhumuni ya utafiti huu yalikuwa ni kutambulisha makosa ya kisarufi, kuainisha makosa haya kisha kubaini kiini cha makosa haya,hatimaye, kupendekeza njia za kurekebisha makosa haya na kuboresha uandikaji wa insha. Nadharia tete za utafiti ni kuwa, makosa ya kisarufi ni mengi na mambo yanayosababisha makosa haya pia ni mengi.nadharia zilizoongoza utafiti ni Nadharia ya Uchanganuzi Makosa (N.U.M.) ikiwa nadharia kuu na Nadharia ya Uchanganuzi Linganuzi (N.U.L) ikiwa nadharia saidizi.katika Nadharia ya Uchanganuzi Makosa, Corder (mwasisi), anasema,kufanya kosa ni njia mojayapo ya kujifundisha lugha ya pili.kwa hivyo,mwanafunzi afanyapo kosa,asiadhibiwe bali kiini cha kosa kibainishwe,kisha kosa lirekebishwe.nadharia ya Uchanganuzi Linganuzi ilitumika kwa kutambua vyanzo vilivyosababishwa na athari za lugha ya kwanza. Kwani Lado (mwasisi) anasema,athari za lugha ya kwanza husababisha makosa ya kisarufi katika ujifundishaji wa lugha ya pili,endapo L1 na L2 zinatofautiana kimuundo.kwa hivyo mwalimu wa lugha anahitajika kufunza tofauti kati ya LI na L2 bali sio kufanana.

6 v Mtafiti alitumia utaratibu wa nyanjani katika ukusanyaji wa data. Data iliyokusanywa ni makosa ya kisarufi katika kipengele cha mofosintaksia na semantiki. Data ilikusanywa kutoka shule za msingi za kata ya Ganze. Mbinu iliyotumika katika kukusanya data ni utaratibu wa nyanjani ambapo wanafunzi wa darasa la nane waliandika mjarabu wa insha. Mtafiti alikusanya insha,akazipitia ili kutambua makosa ya kisarufi yaliyofanywa na wanafunzi kama data ya utafiti. Data ilichanganuliwa kwa kutumia uchanganuzi wa kithamano (maelezo) na uchanganuzi wa kiwingi idadi. Vifaa vilivyotumiwa ni hojaji kwa walimu na mjarabu wa uandikaji wa insha kwa wanafunzi. Matokeo ya utafiti ni kuweko kwa makosa ya udondoshaji, uchopekaji, hijai na mpangilio wa vipashio katika sentensi. Vyanzo vya makosa vilivyobainishwa katika utafiti ni pamoja na ujumuishaji, athari za L1, kutozingatia sheria za lugha lenga, na wanafunzi kutokuwa makini wakati wa kufanya mijarabu ya insha, Miongoni mwa njia za kurekebisha makosa haya ni wanafunzi kupewa mazoezi mengi ya uandikaji wa insha na kusoma vitabu vya hadithi za Kiswahili. Watakao nufaika na utafiti huu ni wanafunzi katika kuboresha uandishi wao wa inshaambao utaboresha matokeo ya mitihani.waandishi wa vitabu vya Sarufi ya watafaidika kwani wataweza kuingiza yote yanayohitajika katika ujifunzaji wa sarufi ya Kiswahili. Hatimaye, Kiswahili kama lugha ya taifa itakuwa ya kiwango cha juu.

7 vi YALIYOMO Ungamo na idhini...i Tabaruku.ii Shukrani...iii Ikisiri... iv Yaliyomo... vi Viambatanishi.. ix Orodha ya Majedwali....x Vifupisho vya Maneno....xii SURA YA KWANZA. 1 UTANGULIZI Usuli wa Mada Swala la Utafiti Madhumuni ya Utafiti Nadharia Tete Upeo na mipaka ya Utafiti Natija ya Utafiti Maelezo ya Istilahi....6

8 vii SURA YA PILI.. 8 MAPITIO YA MAANDIKO Utangulizi Msingi wa Nadharia Nadharia ya Uchanganuzi Makosa (N.U.M) Nadharia ya Uchanganuzi Linganuzi(N.U.L) Msingi wa Kidhana Muhtasari. 22 SURA YA TATU..23 MBINU ZA UTAFITI Ukusanyaji Data Data iliyokusanywa Eneo la Utafiti Jumuia na Uteuzi wa Sampuli Mbinu za kukusanya Data Vifaa vya kukusanyia Data Uchanganuzi wa Data SURA YA NNE. 30 UCHANGANUZI NA UFASIRI WA DATA Utangulizi Uchanganuzi na Ufasiri wa Data Kutambulisha Makosa ya Kisarufi katika Insha za Wanafunzi Kuainisha Makosa ya Kisarufi katika Insha za Wanafunzi

9 viii Makosa ya Udondoshaji Udondoshaji wa Viambishi Makosa ya Udondoshaji wa Neno au Maneno katika Sentensi Makosa ya Uchopekaji Makosa ya Uchopekaji wa Viambishi katika Sentensi Makosa ya Uchopekaji wa Neno au Maneno katika Sentensi Makosa ya Hijai/Tahajia Makosa ya Mfuatano wa Vipashio katika Sentensi Kutafuta Vyanzo vya Makosa ya Kisarufi yaliyotambulishwa Kutathmini Kiwango cha Makosa yaliyotambulishwa katika Data ya Utafiti Kurekebisha makosa ya kisarufi yaliyotambulishwa katika utafiti Matokeo ya Mahojiano kwa Walimu SURA YA TANO 109 Hitimisho na Mapendekezo Utangulizi Hitimisho Mapendekezo MAREJELEO

10 ix VIAMBATANISHO Kiambatanisho 1 Certificate of Ethical Approval 119 Kiambatanisho Kiambatanisho Kiambatanisho Kiambatahisho 5: INSHA Kiambatanisho 6: INSHA Kiambatanisho 7: INSHA Kiambatanisho 8: INSHA Kiambatanisho 9:INSHA 5 127

11 x ORODHA YA MAJEDWALI Jedwali 1. Ripoti kutoka KNEC ya mwaka Jedwali 2: Umoja na Wingi wa Nomino za Lugha za Kibantu Jedwali 3: Umoja na Wingi wa Nomino za Lugha ya Kigeni Jedwali 4: Ngeli za Awali.(K.I.E ) Jedwali 5.Mabadiliko ya Ngeli Jedwali 6: Maneno yaliyofanana yenye Maana tofauti katika L1 na L Jendwali 7: Kielezi cha Kanda, Idadi ya Shule za msingi na idadi ya Wanafunzi wa Darasa la Nane Wilayani Ganze..24 Jedwali 8: Takwimu kutoka Ofisi ya Elimu ya Kata ya Ganze Jedwali 9 : Kielelezo cha Viambishi awali katika Unominishaji Jedwali 10:.Kielelezo cha Viambishi awali katika Umoja na Wingi...34 Jedwali.11: Kielelezo cha Nafsi na Viwakilishi vyake Jedwali 12:Kielelezo cha Viambishi Nafsi kuchukua Nafasi ya Pili Kabla ya Mzizi katika Vitenzi..36 Jedwali 13: Kielelezo cha Nyakati na Viambishi Viwakilishi husika..37 Jedwali 14:Kielelezo cha Aina za Virejeshi Jedwali 15: Kielelezo cha Viambishi Ngeli katika Sentensi Jedwali16:Kielelezo cha Nomino za Ngeli za Kiambishi Ngeli Kimoja katika Umoja nawingi Jedwali 17 :Kielelezo cha Unominishaji kutumia Vambishi vya Wingi Jedwali 18: Kielelezo cha Nyakati katika Usemi Halisi na Usemi wa Taarifa Jedwali 19:Kielelezo cha Nomino za Kigeni zisizohitaji Viambishi vya Wingi..96

12 xi Jedwali 20:Kielelezo cha Nomino za Kibantu na Nomino za Kigeni katika hali ya Umoja na Wingi katika Sentensi 100 Jedwali21:Kielelezo cha Uambishaji wa Nomino za L1 na L2 katika hali ya Umoja na Wingi..101 Jedwali 22: Kielelezo cha Uambishaji wa Nomino za Kigeni katika L1 (Kigiriama) katika hali ya Wingi. 101 Jedwali 23: Kielelezo cha Aina za Makosa ya Kisarufi na Viwango vyake katika kila Kanda, Kata ya Ganze Jedwali 24: Kielelezo cha Viwango vya Aina za Makosa ya Kisarufi. 103 Jedwali 25: Kielelezo cha Viwango vya Aina za Makosa ya Kisarufi katika Grafu 104

13 xii Maelezo ya vifupisho vya maneno. L 1 Lugha ya kwanza L 2 Lugha ya pili N.U.M Nadharia ya Uchanganuzi Makosa (Error Analysis Theory) N.U.L Nadharia ya Uchanganuzi Linganuzi (Constrastive Analysis Theory)) KNEC Kenya National Examination Council (Baraza la Mtihani la Kitaifa la Kenya) KCPE Kenya Certificate of Primary Education (Cheti cha Elimu ya Msingi ya Kenya) RISSEA Research Institute of Swahili Studies in East Africa. UCH _ Uchopekaji UD _ Udondoshaji K _ Kauli Mf _ Mfuatano

14 xiii V _ Kivumishi N _ Nomino U _ Kiunganishi Kt _ Kitenzi Nj _ Njeo Kiony _ Kionyeshi Ng _ Ngeli T _ Tenganisha Cha _ Changanya Dak. _ Dakika

15 SURA YA KWANZA UTANGULIZI 1.1 Usuli wa mada Kiswahili ni mojawapo ya lugha za mawasiliano nchini Kenya, ikiwa lugha rasmi ya kitaifa. Kuna malalamishi kuwa chimbuko la lugha ya Kiswahili ni upwa wa Afrika Mashariki (Massamba 2001), likiwemo eneo la Mkoa wa Pwani, nchini Kenya.Tume ya Elimu ya Gachathi 1976, ilipendekeza kuwa Kiswahili liwe somo la lazima kisha litahiniwe katika shule za msingi na za upili. Nayo Tume ya Elimu ya Mackay 1981, ikatekeleza pendekezo la Tume ya Elimu ya Gachathi 1976 katika mfumo wa elimu wa Kufikia sasa, ni zaidi ya miongo miwili tangu Kiswahili kilipoanza kutahiniwa katika kiwango cha kitaifa, kukiwa bado kuna madai kwamba matokeo ya mitihani ya Kiswahili ya K.C.P.E na K.C.S.E yamekuwa mabaya na yanaendelea kuwa mabaya. Matokeo ya wanafunzi katika Kiswahili hayaridhishi. Kazi ya wanafunzi hasa katika insha za Kiswahili ilionyesha tofauti ndogo sana kutoka kwa ile ya mwaka wa *Ripoti ya KNEC ya mwaka wa Wanafunzi wachache walipata alama thelathini na zaidi, wanafunzi wengi bado wanaendelea kufanya vibaya katika Kiswahili hasa katika uandikaji wa insha *Ripoti ya KNEC ya mwaka wa 1998.

16 Aidha, KNEC ilitoa uchanganuzi wa matokeo ya insha za Kiswahili katika baadhi ya mitihani ya K.C.P.E. Matokeo ya Kiswahili ya insha (K.C.P.E) kutoka Mwaka Jumla ya alama Alama ya wastani Alama ziliyotuzwa watahiniwa wengi Jedwali 1. Ripoti kutoka KNEC ya mwaka Licha ya chimbuko la lugha ya Kiswahili kuwa Mkoa wa Pwani, matokeo ya K.C.P.E na K.C.S.E yanaendelea kuwa mabaya. Suala la Mkoa wa Pwani kuwa chimbuko la lugha ya Kiswahili limesababisha Wapwani kufikiria kwamba wanafunzi wana ustadi wa lugha ya Kiswahili.Kwa hivyo hakuna haja ya kufanya mazoezi ya lugha ya Kiswahili wakiwa shuleni ama hata nyumbani. Matokeo ya wazo hili yakiwa matokeo mabaya ya mitihani ya Kiswahili. Ripoti ya Rissea ya kongamano iliyokuwa 19/05/2011

17 Kulingana na ripoti ya KNEC ( ) na Rissea (2011), ni wazi kwamba matokeo ya wanafunzi katika mtihani wa Kiswahili hasa katika insha za Kiswahili yameendelea kuwa mabaya na yanachangia kuanguka kwa wanafunzi katika mitihani ya Kiswahili Ripoti ya RISSEA (2011), ilidhihirisha kutambuliwa kwa tatizo hili la wanafunzi kuanguka mtihani wa Kiswahili na kukaitishwa kongamano ya Kiswahili mnamo tarehe , lakini wataalamu wa lugha ya Kiswahili hawakushughulikia sehemu maalum ambazo zingetoa thibitisho la matokeo mabaya ya mitihani ya Kiswahili, badala yake walishughulikia kiini cha matokeo mabaya kwa jumla. 1.2 Swala la utafiti. Kuna sababu nyingi zinazochangia kuanguka kwa wanafunzi katika mitihani ya Kiswahili, kata ya Ganze. Mojawapo ya sababu zinazochangia ni makosa ya kisarufi. Kulingana na udurusu wa awali wa mtafiti, hakuna utafiti uliofanywa katika kata ya Ganze ulioweka wazi mchango wa makosa ya kisarufi katika matokeo ya Kiswahili hususan katika insha wanazoandika wanafunzi. Hali hii inadhihirisha kuwepo kwa mwanya wa kielimu juu ya mchango wa makosa ya kisarufi katika kuanguka kwa wanafunzi katika mitihani ya Kiswahili. Utafiti huu umeziba mwanya huu. 1.3 Madhumuni ya utafiti. Katika utafiti huu, mtafiti alikuwa na madhumuni yafuatayo:- i) Kutambulisha makosa ya kisarufi katika mitihani ya insha ya wanafunzi wa shule za msingi, katika kata ya Ganze.

18 ii) Kuainisha makosa ya kisarufi katika mitihani ya insha ya wanafunzi wa shule za msingi, katika kata ya Ganze. iii) Kubainisha kiini cha makosa ya kisarufi katika mituhani ya insha ya wanafunzi wa shule za msingi, katikakata ya Ganze. 1.4 Nadharia Tete i) Kuna makosa mengi ya kisarufi katika mitihani ya insha za Kiswahili ya wanafunzi wa shule za msingi katika kata ya Ganze. ii) Kuna aina nyingi za makosa ya kisarufi katika mitihani ya insha ya wanafunzi wa shule za msingi katika kata ya Ganze. iii) Kuna vyanzo vingi vinavyosababisha kuweko kwa makosa ya kisarufi katika mitihani ya insha ya wanafunzi wa shule za msingi katika kata ya Ganze. 1.5 Upeo na mipaka ya utafiti. Mtafiti alichunguza makosa ya kisarufi katika insha za wanafunzi wa shule za msingi katika kata ya Ganze. Kuna vipengele tofautitofauti vya lugha ambavyo ni fonolojia, mofolojia, semantiki, sintaksia, leksia na hata pragmatiki. Vipengele vilivyoshughulikiwa katika utafiti ni mofolojia na sintaksia ambavyo muungano wake ni makosa ya kimofosintaksia. Hivyo mtafiti hakujihusisha na makosa ya kifonolojia (matamshi) na kisemantiki (maana). Katika karatasi ya mtihani wa Kiswahili, kuna sehemu mbili ambazo sarufi hutahiniwa. Katika karatasi ya kwanza, swali la kwanza (1) hadi la thelathini (30) ni maswali ya sarufi, ambayo hubeba asilimia thelathini na sita (36%).Swali la thelathini na moja hadi hamsini

19 (31-50) ni maswali ya ufahamu ambayo huchukua alama asilimia hamsini na mbili (52%). Karatasi ya pili ni ya uandikaji wa insha ambayo sehemu ya sarufi huwa na alama kumi na mbili (12%). Sarufi yote ni asilimia arubaini na nane (48%) ambayo ni kubwa. Ili mwanafunzi aweze kupata hizi asilimia hamsini na mbili (52%), ni lazima awe ni mzuri katika sarufi ya lugha ya Kiswahili. Nayo sarufi ya lugha hudhihirika katika uandikaji wa insha. Aidha, karatasi ya kwanza inazo alama nyingi za sarufi, naye mtafiti hakushughulika na sehemu hii kwa sababu maswali yake ni ya uchaguzi wa majibu, hivyo basi haina uthibitisho wa sarufi ya lugha ya Kiswahili wa mwanafunzi. Zaidi, msingi wa lugha ni sarufi. Kwa hivyo, mtafiti alishughulikia sehemu ya insha peke yake ili kuthibitisha tajriba na umilisi wa lugha ya Kiswahili ya wanafunzi. 1.6 Natija ya utafiti. Utafiti huu ni wa manufaa kwa wanafunzi kwani unatambulisha makosa ya kisarufi ambayo wanafunzi hufanya katika uandishi wa insha. Kwa hivyo wanafunzi watanufaika kupitia kwa walimu wao ambao kulingana na ushauri wao na mapendekezo ya mtafiti, watatambua kanuni za lugha ya Kiswahili kuhusu aina na vyanzo vya makosa ya kisarufi. Mapendekezo ya mtafiti yatawawezesha walimu wa lugha ya Kiswahili kuimarisha mbinu za ufundishaji kisha wataweza kusaidia wanafunzi kupita mitihani ya lugha ya Kiswahili. Hatimaye, walimu wataweza kutambua njia za kupunguza na kukabiliana na aina mbalimbali za makosa ya kisarufi. Waandishi wa vitabu vya sarufi vya shule za msingi watanufaika kwa kuandika vitabu vya sarufi wakijua vyanzo vya makosa ya wanafunzi ili

20 watoe mafunzo na mazoezi yanayokabiliana na aina za makosa yaliyodhihirishwa katika utafiti huu. 1.7 Maelezo ya Istilahi. Hijai Utaratibu maalum unaokubalika katika kuendeleza maneno ya lugha fulani. Natija Manufaa au umuhimu wa jambo, tukio au kitu fulani. Ruwaza Mpangilio maalum wa maneno katika kuunda sentensi sanifu. Uakifishaji Matumizi sahihi ya alama za uandishi mbalimbali katika uandikaji wa makala Vipashio Vipande vya tungo vyenye maana, vinavyojenga sentensi. Udurusu Kupitia maandishi ya wengine kwa madhumuni ya kusahihisha, kuboresha au kutoa chapisho zengine. Mahafali Sherehe ya kufuzu katika shahada ya uzamili Athari za lugha Ujuzi wa lugha moja ambao ni tofauti na ujuzi wa lugha nyingine, ambao huathiri sheria na kanuni za lugha nyingine. Mikakati Mipango maalum inayoandaliwa kwa ustadi ili itumike kama njia ya kufikia lengo la ujifunzaji wa L 2 (Kiswahili)

21 Mchakato Mfululizo wa shughuli unaosababisha kitu fulani kufanyika au lengo fulani kufikiwa. Kigezo Sifa inayokubalika kama msingi wa kupimia au kutolea uamuzi wa jambo

22 SURA YA PILI MAPITIO YA MAANDIKO. 2.1 Utangulizi. Baraza la Mtihani wa Kitaifa la Kenya (KNEC, 1998), lilitoa sababu za wanafunzi kuanguka mitihani ya Kiswahili katika karatasi ya insha. Mojawapo ya sababu ikiwa ni matumizi ya lugha isiyokuwa sanifu. Kuna wataalamu wengi wa lugha ambao wamefanya tafiti za lugha ya Kiswahili. Baadhi ya wataalam walioshughulikia swala la lugha ni pamoja na Mangwa (2005), Kevogo (2007), Mulei (2006), Lado (1957), KNEC (1998), Halliday (1964) Corder (1978), alifanya utafiti wa lugha akagundua kwamba watu wanapojifunza lugha ya pili (L 2 ) huwa wanayo lugha ya kwanza (L 1 ), nao hutumia kanuni wanazozielewa katika L1 katika upataji au ujifunzaji wa L2, kisha huhamisha muundo wa L 1 kwa L2. Kwa hivyo, mazoea ya wanafunzi kutumia kanuni za L 1 katika L 2 hutawaliwa na kaida za L 1. Kazi ya Corder ni tofauti na ya mtafiti huyu kwa kuwa Corder (1978) alishughulikia lugha yoyote ya kwanza na ya pili, ilhali L1 katika utafiti huu ni Kigiriama na L2 ni Kiswahili. Mtafiti alifaidika na kazi ya Corder (1978) katika kuainisha makosa ya kimofosintaksia na kutambua kiini cha makosa hayo kutokana na insha za wanafunzi. Kevogo (2007), alishughulikia makosa ya kisarufi na jinsi yanavyoathiri ujifunzaji wa lugha ya Kiswahili. Alichunguza makosa ya kisarufi katika insha za wanafunzi wa darasa la nane miongoni mwa jamii ya Wajaluo. Katika utafiti wake, aligundua kwamba lugha ya kwanza ya wanafunzi iliathiri ujifunzaji wa lugha ya Kiswahili. Tofauti ya utafiti wa

23 Kevogo (2007) na utafiti huu ni lugha ya kwanza ya wanafunzi kwani Kevogo alijishughulisha na lugha ya Kijaluo wilayani Bondo ilhali mtafiti alijishughulisha na lugha ya Kigiriama(L1) na maeneo ya utafiti yakiwa mkoa wa pwani, kata ya Ganze. Utafiti wa Kevogo (2007) ulimsaidia mtafiti katika kuthibiti welewa na athari ya L1 katika ujifunzaji wa L2. He Dan (2010), alifanya utafiti juu ya uchanganuzi wa makosa yanayofanywa na wanafunzi wa Kichina katika chuo kikuu cha Huizho, wakiwa lugha yao ya kwanza ni Kichina na L2 ni Kiingereza. Alitumia Nadharia ya Mwingiliano Lugha ambapo alizingatia makosa yanayotokana na uhamishaji wa Kichina kwa Kiingereza. Data aliyokusanya ilitokana na insha za wanafunzi. Aidha, alichunguza makosa ya kisintaksia. Utafiti wa He Dan (2010), unalingana na utafiti wa mtafiti katika ukusanyaji wa data na baadhi ya makosa yaliyozingatiwa yakiwa ni pamoja na ya kisintaksia na kisemantiki. Kazi ya He Dan (2010) inatofautiana na kazi ya mtafiti kwani He Dan (2010) alifanya utafiti wake China katika chuo kikuu, L 1 ikiwa Kichina, makosa yaliyoshughulikiwa yalikuwa pamoja na ya kisemantiki, nayo nadharia iliyotumiwa ni Nadharia ya Mwingiliano Lugha, ilhali mtafiti alifanya utafiti nchini Kenya katika shule za msingi. Lugha ya kwanza ya wanafunzi ikiwa Kigiriama na L2, Kiswahili. Makosa yaliyochunguzwa ni ya kimofosintaksia nayo nadharia iliyotumiwa ni Nadharia ya Uchanganuzi Makosa(N.U.M) ikisaidiwa na Nadharia ya Uchanganuzi Linganuzi (N.U.L). Utafiti wa He Dan (2010) ulimnufaisha mtafiti katika ukusanyaji na uchunganuzi wa data. Mangwa (2005), alishughulikia athari za Ekegusii katika lugha ya Kiswahili na jinsi athari hizo zinavyochangia matokeo mabaya katika mtihani wa kitaifa wilayani Kisii Kusini katika kiwango cha sekondari. Katika kazi yake, alifanya uchunguzi katika kipengele cha

24 kifonetiki, kifonolojia na sarufi. Alitumia Nadharia ya Uchanaganuzi Makosa (N.U.M) na Nadharia ya Uchanganuzi Linganuzi (N.U.L). Utafiti wa Mangwa (2005) unatofautiana na utafiti huu katika kiwango na vipengele alivyoshughulikia. Utafiti wa mtaalam huyu unalingana na wa mtafiti katika nadharia zilizotumiwa kwani ndizo zilizotumiwa katika utafiti huu. Kazi ya Mangwa (2005) ailimnufaisha mtafiti kudhibitizaidi suala la athari za L2 katika ujifunzaji wa L2. Seliger na Shohamy (1989), na Larse Freeman na Long (1994), walifanya utafiti wa makosa wanayofanya wanafunzi katika tungo mbalimbali. Katika utafiti wao, walipendekeza mbinu za kukusanyia data ya makosa katika tungo za wanafunzi. Mojawapo ikiwa ni uandikaji wa insha. Katika utafiti wao, Seliger na Shohamy (1989), walitumia Nadharia ya Uchanganuzi Makosa(N.U.M). Utafiti wa wataalamu hawa unafanana na utafiti huu katika mbinu ya ukusanyaji wa data na nadharia iliyotumiwa. Kazi ya wataalam hawa ni tofauti na kazi ya mtafiti kwa kuwa walishughulikia makosa katika vipengele vyote vya lugha ilhali mtafiti alishughulikia makosa ya kimofosintaksia pekee. Mtafiti alinufaika na utafiti wa wataalam hawa katika kuthibiti data ya utafiti. Ellis na Rathbone (1987) walichunguza athari za kuhudhuria mafunzo darasani katika kujifunza Kijerumani kama L2. Katika utafiti wao, walitoa maagizo ya mafundisho kirasmi na mazoezi ya sarufi yakafanywa kwa usimamizi. Waligundua kwamba wanafunzi waliohudhuria mafunzo haya walifanya vizuri katika sarufi. Utafiti wa wataalam hawa ni tofati na utafiti wa mtafiti kwani walishughulikia Kijerumani kama L2 na athari za kuhudhuria mafunzo darasani, naye mtafiti alichunguza makosa ya kimofosintaksia katika lugha ya Kiswahili ikiwa lugha ya pili. Utafiti wa Ellis na Rathbone

25 (1987) unafanana na utafiti wa mtafiti katika vifaa vya kukusanyia data ambazo ni insha za wanafunzi aidha katika usimamizi wa mtafiti. Mtafiti alinufaika katika hali ya kupata data ambayo ilitokana na wanafunzi waliokuwa darasani. Halliday (1964) alifanya utafiti juu ya ujifunzaji wa lugha ya pili yoyote. Katika utafiti wake, aligundua kwamba mwanafunzi wa L2 huwa ana umilisi wa L1. Kwa hivyo, huhamisha muundo wa L1 kwa L2, hatimaye L2 huathiriwa. Baadaye, lugha atakayozungumza mwanafunzi, hudhibitisha athari za L1. Utafiti wa Halliday (1964) ulishughulikia L1 na L2 kwa jumla naye mtafiti alichunguza lugha ya Kiswahili kama L2. Utafiti wa Halliday (1964) ulimnufaisha mtafiti katika kudhibiti welewa wa athari za L1 na L2. Lado (1957) alichunguza L1 na L2 ikiwa L1 ni lugha asili ya mwanafunzi na L2 ni lugha ngeni ya mwanafunzi husika. Kupitia uchunguzi wake, aligundua kwamba, mwanafunzi wa lugha ngeni hupambana na vipashio vigumu ambavyo havimo katika lugha yake asilia. Aidha, hupata vipashio vingine vikiwa rahisi maana viko sawa na vile vya lugha yake ya kwanza. Mwanafunzi huyu, hujaribu kuongeza mofimu fulani kutoka lugha yake katika L2 kwa kutumia mfumo wa lugha yake ya kwanza. Hii ni kwa sababu baadhi ya mofimu za lugha tofauti hukaribiana kimuundo. Kazi ya Lado (1957) ni tofauti na kazi ya mtafiti kwa kuwa Lado alishughulikia L1 na L2 katika lugha yoyote ile, bali mtafiti alishughulikia lugha maalum ikiwa L1 ni Kigiriama na L2 ni Kiswahili. Mtafiti alifaidika na utafiti wa Lado katika kudhibitisha athari za L1 katika ujifunzaji wa L2. Stockwell, Bowen na Martin (1965) walifanya uchunguzi wa kutambua ruwaza za lugha ambazo zilisababisha ugumu katika kulinganisha L1 na L2. Waliweza kuutazama ugumu

26 wa ruwaza za lugha kwa kina na wakagundua kwamba, kila lugha ina ruwaza zake kulingana na sheria za lugha hiyo. Utafiti wa wataalam hawa ni tofauti na utafiti huu kwa kuwa walishughulikia ruwaza za lugha mbalimbali ilhali mtafiti alishughulikia makosa katika kazi za wanafunzi (insha). Mtafiti alinufaika na utafiti wa wataalam hawa katika kudhibiti athari za L1 katika L2. Campbell na Qorro (1997), walishughulikia matokeo ya mtihani katika shule za upili nchini Tanzania. Utafiti wao ulichunguza lugha ya Kiingereza. Wataalamu hawa waligundua kwamba, matokeo yalikuwa mabaya, mojawapo ya visababishi ikiwa athari za L1. Lugha za kwanza za wanafunzi walioshirikishwa katika utafiti huu zilikuwa tofautitofauti, japo baadhi yao walikuwa lugha yao ya kwanza ni Kiswahili. Hii ina maana kuwa, L1 yoyote inaweza kuathiri L2. Utafiti huu ni tofauti na utafiti wa mtafiti kwa kuwa ulishughulikia lugha ya Kiingereza ikiwa mtafiti alishughulikia lugha ya Kiswahili ikiwa L2. Kazi ya wataalamu hawa zitamfaidi mtafiti kudhibiti zaidi elimu ya ujifunzaji wa L2. Dulay na Burt (1972) walifanya utafiti wa kulinganisha L1 na L2, nao wakasema kwamba L1 ni sawasawa na L2. Utafiti wa watafiti hawa unatofautiana na utafiti huu kwa kuwa walishughulikia L1 na L2 katika hali ya kuzilinganisha. Kazi ya Dulay na Burt (1972) inalingana na kazi ya mtafiti katika nadharia iliyotumiwa ambayo ni Nadharia ya Uchanganuzi Linganuzi (N.U.L). Mtafiti alinufaika na utafiti wa wataalam hawa kwa kuwa alitumia hatua za Nadharia ya Uchanganuzi Linganuzi katika kubaini tofauti za L1 (Kigiriama) ya wanafunzi na lugha lengwa (Kiswahili).

27 Ng ang a (2002), alifanya utafiti juu ya makosa ya kisarufi katika insha za wanafunzi wa darasa la saba na jinsi yanavyoshughulikiwa na walimu katika tarafa ya Ndaragwa. Alichunguza makosa ya kisintaksia, kisemantiki, kimofolojia na makosa ya hijai. L1 ya wanafunzi ilikuwa Kikikuyu na L2 iliyoshughulikiwa ni Kiingereza.Hivyo ni kumaanisha,wanafunzi walikuwa Wakikuyu na walikuwa wakijifunza Kiingereza. Data ilikusanywa kutokana na insha za lugha ya Kiingereza kutoka kwa wanafunzi wa darasa la saba. Katika utafiti wake, Ng ang a aligundua kwamba, lugha ya Kiingereza (L2), iliathiriwa na lugha ya Kikikuyu (L1) kwani makosa mengi yaliyobainika yalisababishwa na athari za L1. Utafiti wa Ng ang a (2002), unatofautiana na wa mtafiti kwani Ng ang a alishughulikia Kikikuyu (LI) na Kiingereza (L2) ilhali mtafiti alishughulikia Kigiriama (L1) na Kiswahili (L2). Ng ang a alichunguza makosa ya kisarufi na jinsi yanavyoshughulikiwa na walimu ilhali mtafiti alichunguza makosa ya kisarufi na jinsi yanavyochangia matokeo mabaya ya mitihani ya Kiswahili. Zaidi, sampuli ya utafiti wa Ng ang a ilitokana na wanafunzi wa darasa la saba katika tarafa ya Ndaragwa, nayo sampuli ya utafiti wa mtafiti ilitokana na wanafunzi wa darasa la nane katika kata ya Ganze, kaunti ya Kilifi. Nayo misingi ya nadharia iliyotumika ikiwa ndiyo mfanano wa utafiti wa Ng ang a (2002) na wa mtafiti, kwani wote walitumia Nadharia ya Uchanganuzi Makosa isipokuwa mtafiti alisaidiwa na Nadharia ya Uchanganuzi Linganuzi (N.U.L).Utafiti wa Ng ang a ulimfaidisha mtafiti katika kuthibiti na kuelewa athari za L1 katika L2. Mudhune (1994), alichunguza matatizo ya kimofosintaksia yaliyowakumba wanafunzi wa jamii ya Wajaluo katika kujifunza lugha ya Kiswahili (L2). Matatizo yalibainishwa kutokana na insha za lugha ya Kiswahili zilizoandikwa na wanafunzi wa darasa la nane.

28 Mudhune alichanganua data kwa kutumia Nadharia ya Uchanganuzi Linganuzi. Katika utafiti wake, Mudhune aligundua ya kwamba,lugha ya Kiswahili katika insha za wanafunzi iliathiriwa sana na lugha ya kwanza ya wanafunzi (Kijaluo). Utafiti wa Mudhune (1994), unafanana na utafiti wa mtafiti katika sampuli ya wanafunzi ikiwa darasa la nane. Licha ya kufanana, utafiti wa Mudhune(1994), unatofautiana na utafiti wa mtafiti katika L1, kwani Mudhune alishughulikia Kijaluo(L1) naye mtafiti akashughulikia Kigiriama (L1). Katika misingi ya kinadharia, Mudhune alitumia Nadharia ya Uchanganuzi Linganuzi ilhali mtafiti alitumia Nadharia ya Uchanganuzi Makosa (N.U.M) ikisaidiwa na Nadharia ya Uchanganuzi Linganuzi (N.U.L). Aidha, Mudhune alichunguza matatizo ya kimofosintaksia na jinsi yanavyowakumba wanafunzi katika jamii ya Wajaluo katika kujifunza lugha ya Kiswahili ilhali mtafiti alichunguza makosa ya kimofosintaksia katika insha na yanavyochangia matokeo mabaya ya mitihani ya Kiswahili.Utafiti wa Mudhune (1994), ulimnufaisha mtafiti katika uelewa wa athari za L1 katika ujifunzaji wa L2. Musa (2008), alichunguza athari za lugha ya Kigweno (L1) katika ujifunzaji wa lugha ya Kiswahili (L2) na jinsi zinavyoathiri matokeo mabaya ya mtihani wa kitaifa wa kidato cha nne. Katika kuchanganua data, Musa alitumia Nadharia ya Uchanganuzi Linganuzi ikisaidiwa na Nadharia ya Uchanganuzi Makosa. Musa alishughulikia vipengele vya kisemanti, kimofolojia na kisintaksia. Data iliyokusanywa ilitokana na mazungumzo ya wanafunzi katika mijadala. Katika utafiti wake, Musa aligundua kwamba, athari za lugha ya kwanza katika ujifunzaji wa lugha ya pili, huathiri matokeo ya mtihani kwa kiwango kikubwa. Utafiti wa Musa unatofautiana na wa mtafiti katika L1 kwani Musa alishughulikia Kigweno (L1) ilhali mtafiti alishughulikia Kigiriama (L1).

29 Aidha, Musa (2008) alichunguza athari za L1 katika ujifunzaji wa L2 na jinsi zinavyoathiri matokeo mabaya ya mtihani wa Kiswahili katika kidato cha nne ilhali mtafiti alichanganua makosa ya kisarufi katika insha na jinsi yanavyochangia matokeo mabaya ya mitihani ya Kiswahili ya darasa la nane. Vilevile, Musa alitumia misingi ya kinadharia ya Nadharia ya Uchanganuzi Linganuzi kama nadharia kuu, ikisaidiwa na Nadharia ya Uchanganuzi Makosa,naye mtafiti alitumia nadharia zizi hizi lakini kinyume cha matumizi ya Musa. Yaani, mtafiti alitumia Nadharia ya Uchanganuzi Makosa ikiwa nadharia kuu na Nadharia ya Uchanganuzi Linganuzi ikiwa nadharia saidizi. Vipengele vya lugha vilivyoshughulikiwa na Musa ni semantiki, mofolojia na sintaksia ilhali mtafiti alishughulikia kipengele cha mofolojia na sintaksia pekee. Musa alikusanya data kwa kutumia mijadala kama kifaa ilhali mtafiti alitumia insha za lugha ya Kiswahili kama vifaa vya kukusanyia data ya utafiti. Utafiti wa Musa (2008) ulikuwa wa msaada kwa mtafiti kwani ulimpa muongozo katika kutambua na kuthibiti athari za L1 katika ujifunzaji wa L2 miongoni mwa wanafunzi wa jamii ya Wagiriama. 2.2 Msingi wa Nadharia. Mtafiti alitumia Nadharia ya Uchanganuzi Makosa (N.U.M) ikiwa nadharia kuu na Nadharia ya Uchanganuzi Linganuzi (N.U.L) ikiwa nadharia saidizi.

30 2.2.1 Nadharia ya Uchanganuzi Makosa (N.U.M) Nadharia ya Uchanganuzi Makosa (N.U.M) ni nadharia inayochunguza makosa yanayofanywa na wanaojifunza lugha ya pili (Gas na Selinker 2008). Nadharia hii (N.U.M), iliasisiwa na Corder (1967). Corder (1967), alizungumza umuhimu wa makosa ya wanafunzi katika matumizi ya lugha. Kulingana na Corder (1967), misingi ya N.U.M ni kama ifuatayo: i) Katika ujifunzaji wa L2, mwanafunzi lazima afanye makosa. ii) Kufanya makosa ni kawaida kwa hivyo mwanafunzi anapofanya makosa asiadhibiwe bali makosa hayo yachukuliwe kama kigezo cha kuthibitisha kuwa mwanafunzi bado hajajifundisha lugha. Kwa hivyo,hatua zifuatazo zitekelezwe:- - Makosa yaweze kutambuliwa. - Makosa hayo yaainishwe. - Njia mwafaka za kurekebisha makosa hayo ziweze kupendekezwa. Corder 1974 alitoa hatua tano muhimu za kutumiwa na watafiti katika kutafuta na kuchanganua data. Hatua hizo ni: i) Ukusanyaji wa maandishi yote ya waandishi (wanafunzi wa darasa la nane) kutokana na mada moja ambayo ni, Siku ambayo sitaisahau. ii) Utambuaji wa makosa yenyewe kwa mfano: a) Ukosefu wa uwiano wa kisarufi katika matumizi ya njeo.

31 b) Udondoshaji wa viambishi katika maneno ya lugha iii) Uainishaji wa makosa katika makundi maalum. Kwa mfano, udondoshaji wa viambishi ngeli. iv) Makosa yaelezwe kulingana na kiini cha makosa hayo. Kwa mfano, athari za lugha ya kwanza katika lugha ya pili, na kuendeleza maneno ya lugha vibaya. v) Kuonyesha kiwango cha athari inayosababishwa na tokeo la kosa hilo Nadharia ya Uchanganuzi Linganuzi(N.U.L) Ni nadharia inayoshughulikia uchanganuzi wa kiisimu unaouhusu ulinganishi wa lugha mbili (James, 1980). Nadharia ya Uchanganuzi Linganuzi (N.U.L) iliasisiwa na Lado (1957), naye alidai kwamba kuna vipengele vinavyofanana katika lugha ya kwanza na lugha ya pili (L 2 ). Vipengele hivi huwa rahisi kwa mzungumzaji ilhali vile ambavyo vinatofautiana katika L 1 na L 2 huwa vigumu kwa mwanafunzi yeyote wa lugha ya pili. Kwa mfano; LUGHA YA KWANZA (KIGIRIAMA) LUGHA YA PILI (KISWAHILI) UMOJA WINGI UMOJA WINGI Muhi mubomu Mihi mibomu Mti mkubwa Miti mikubwa Kihi kiki ni changu Vihi zhangu Kiti changu Viti vyangu Kinu kidzo Vinu vidzo Kinu kizuri Vinu vizuri Gari rehu Magari yehu Gari letu Magari yetu Jedwali 2: Umoja na wingi wa nomino za lugha za kibantu

32 Katika mifano hii, viambishi vya wingi vinavyotumika katika L 1 ndivyo vinavyotumika kama viambishi vya wingi katika L 2. Kwa hivyo, wanafunzi huchukua kipengele hiki kuwa rahisi, vilevile, hupata ugumu kwa sababu sheria hii haitumiki katika nomino zote. Kwa mfano: L 1 (Kigiriama) L 2 (Kiswahili) Umoja Wingi Umoja Wingi Karathasi rangu Makarathasi gangu Karatasi yangu Karatasi zangu Sahani ridzo Masahani madzo Sahani zuri Sahani nzuri Jedwali 3: Umoja na wingi wa nomino za lugha ya kigeni Lado (1957) aliweka wazi kuwa, mwalimu anayeweza kutofautisha L1 na L2 ya mwanafunzi hujua wazi sehemu ambazo zina matatizo.mwalimu huweza kutoa mafunzo mwafaka katika kutatua matatizo hayo. Nadharia ya Uchanganuzi Linganuzi pia huchangia jinsi lugha inavyobadilika kutoka kipindi fulani maalum hadi chengine. Kwa mfano, awali, upatanisho wa kisarufi wa ngeli ulitokana na viambishi vya umoja na wingi wa nomino.

33 Kwa mfano: SENTENSI UMOJA WINGI NGELI ZA AWALI Mtu ameingia ndani. Watu wameingia ndani. M-WA Jina lake limefutwa Majina yake yamefutwa. JI-MA Mti umeanguka. Miti imeanguka. M-MI Uso umepujuka. Nyuso zimepujuka. U-N Jedwali 4: Ngeli za awali.(k.i.e ) Baadaye, utaratibu wa ngeli ulibadilika kutoka viambishi vya umoja na wingi wa nomino na kuwa viambishi awali vinavyoambatanishwa na vitenzi vikirejelea nomino husika katika sentensi husika.kwa mfano: Umoja Wingi Ngeli Mti umenguka Miti imeanguka U-I Mtu analima Watu wanalima A-WA Jani limekauka Majani yamekauka LI-YA Jedwali 5.Mabadiliko ya ngeli Zaidi, baadhi ya ngeli zilizotumika awali hazitumiki kamwe. Kwa mfano, ngeli ya U-N, JI- MA na ngeli ya M-MI. Lado (1957), anasema kwamba N.U.L huchukulia kuwa wazungumzaji wa lugha hujaribu kuhamisha maana kutoka L 1 hadi L 2.

34 Kwa mfano; L1 (Kigiriama) L2 (Kiswahili) maana Zama Kuinama Zama Kuingia ndani ya maji Kujificha Kutoweka Jedwali 6: Maneno yaliyofanana yenye maana tofauti katika L1 na L2. Kipindi (wakati) Kwa hivyo, nadharia hii hushughulikia jinsi L1 inavyomwathiri mwanafunzi wa L2. Katika karatasi hii L1 ni kigiriama na L2 ni lugha ya Kiswahili.Mtafiti alitumia nadharia hii kuthibiti athari za lugha ya kwanza katika lugha ya pili. Vilevile, kubaini njia za kurekebisha makosa ya kisarufi yanayofanywa na wanafunzi Nguzo za Nadharia ya Uchanganuzi Linganuzi ni: i) Makosa katika kujifunza lugha ya pili husababishwa na athari za lugha ya kwanza endapo lugha ya kwanza na ya pili zinatofautiana kimuundo, kwa hivyo wanafunzi hutatizika katika kujifunza L2 kwani tayari huwa wanaumilisi wa L1. ii) Matokeo ya kulinganisha lugha ya kwanza na ya pili hubashiri matatizo ya makosa yatakayotokea katika kujifunza lugha ya pili. iii) Mwalimu wa lugha anahitajika kufunza tofauti kati ya L1 na L2 bali sio kufanana. James (1980), anasema kwamba wanafunzi wanastahili kufunzwa kufanana kwa L1 na L2 ili waweze kujigundulia sehemu ambazo uhamishaji unakubalika na wapi haukubaliki.

35 2.3. Msingi wa Kidhana. Insha Makosa ya kisarufi Makosa ya kimofolojia Makosa ya kisintaksia Makosa ya Kimofosintaksia Uwiano wa viambishi k.m. ngeli, njeo, vikanusho, virejeshi n.k Mifuatano ya vipashio k.m. nomino, vitenzi, vielezi n.k. Kiini cha makosa Njia za kurekebisha makosa Lugha sahihi

36 2.4 Muhtasari. Mtafiti alinufaika na tafiti za wataalam alizonukuu katika utafiti wake, katika kuthibitisha wazi nadharia tete alizoibuka nazo katika utafiti huu. Nadharia ya Uchanganuzi wa Makosa na Nadharia ya Uchanganuzi Linganuzi zilimnufaisha mtafiti kwa kuchanganua data aliyokusanya. Nao msingi wa kidhana, ulimuongoza mtafiti katika hatua za kuendeleza utafiti wake kwa mpangilio maalum.

37 SURA YA TATU. MBINU ZA UTAFITI. 3.1 Ukusanyaji data. Mtafiti alikusanya data kutumia utaratibu wa nyanjani. Utaratibu wa nyanjani ulikuwa mwafaka kwa sababu mtafitialihitaji wanafunzi shuleni waandike insha kupitia mjarabu aliyowapa.wanafunzi walifanya mjarabu chini ya usimamizi wa mtafiti, ndani ya muda wa dakika arubaini (dak.40). Baada ya mjarabu, mtafiti alikusanya insha hizo na kwa wakati wake, alizipitia na kuzisahihisha ili aweze kutambua makosa. Data iliyokusanywa ni makosa ya kimofosintaksia yaliyotokana na lugha ya wanafunzi waliyotumia katika uandikaji wa insha Data iliyokusanywa. Mada mojailitolewa kama mjarabu wa insha katika kila shule iliyoteuliwa. Mada ya mjarabu wa insha ulikuwa: Sikuambayo sitaisahau. Mtafiti alitoa mada hii kwa sababu inampa mwanafunzi uhuru wa kujieleza ambapo atakuwa na mawazo mapana yatakayomfanya kuwa na hoja nyingi za kufafanua kwa lugha ya Kiswahili Eneo la Utafiti. Utafiti ulifanywa katika shule ishirini na nne(24) za msingi katika kata ya Ganze ambako wakaazi wengi ni Wagiriama.Shule hizi ni Malomani, Mwaeba, Petanguo, Mayowe, Mwapula, Vitsapuni, Migumomiri, Mwangea, Mihuhuni, Rare, Dunguni, Dungicha, Danicha, Bogamachuko, Dzikunze, Dida, Mitsemerini, Kidemu, Mwakwala, Nzovuni, Mnago wa Dola, Midoina, Jila,na Ndigiria. Lugha inayotumika sana katika maeneo haya

38 kama lugha ya kwanza ni Kigiriama ilhali lugha yao ya pili itakayoshughulikiwa katika utafiti huu ni Kiswahili Jumuia na uteuzi wa sampuli. Jumuia ya utafiti ilikuwa shule za msingi, walimu na wanafunzi wa darasa la nane katika kata ya Ganze. Kielimu, kata ya Ganze ina kanda (zoni) tatu (3) ambazo ni Ganze, Bamba na Vitengeni. Kanda ya Ganze ina shule za msingi ishirini na nne (24), kanda ya Bamba ina shule za msingi ishirini na tano (25) na kanda ya Vitengeni ina shule za msingi thelathini (30). Shule hizi zikiwa ni zile zilizofika kiwango cha darasa la nane.katika kila kanda, mtafiti aliteua shule nane (8). KANDA IDADI YA SHULE ZA MSINGI IDADI YA WANAFUNZI WA DARASA LA NANE. Ganze Bamba Vitengeni Jumla Jendwali 7: Kielezi cha kanda, idadi ya shule za msingi na idadi ya wanafunzi wa darasa la nane wilayani Ganze. Kila kanda,ina shada nne za kielimu. Inaaminika kwamba, takriban wanafunzi wote wa shule ambazo zimo katika shada moja huwa na tabia na sifa zinazokaribiana. Kwa sababu hii, mtafiti alitumia uteuzi wa kishada kwa kuteua sampuli ya shule. Mtafiti, aliorodhesha shule zote katika kila shada, kisha kwa kutumia mbinu yakinasibu, aliteua shule mbili za

39 msingi kama kiwakilishi cha shule zote za msingi katika shada husika. Hivyo, sampuli ya walimu ilikuwa na walimu ishirini na wane (24).

40 Kanda Shada Shule zilizoteuliwa Idadi ya Wanafunzi wa darasa la nane wa 2014 Jumla Sampuli (1/3) ya Jumuia Ganze Ganze Malomani Mwaeba Dungicha Petanguo Dungicha Jaribuni Mayowe Mwapula Palakumi Vitsapuni Migumomiri Vitengeni Vitengeni Mwangea Mihuhuni Sokoke Rare Dunguni Dulukiza Danicha Bogamachuko Dzikunze Dzikunze Dida Bamba Bamba Mitsemerini Kidemu Nzovuni Mwakwala Nzovuni Midoina Midoina Mnago wa Dola Karimani Jila Ndigiria Jumla Jedwali 8: Takwimu kutoka Ofisi ya Elimu ya kata ya Ganze.

41 Mtafiti aliteua wanafunzi kutumia mbinu ya kinasibu. Kulingana na idadi ya wanafunzi katika kila darasa la nane lililoteuliwa, mtafiti alichukua thuluthi ya jumla ya idadi ya wanafunzi katika kila darasa kwa kutumia mbinu ya kinasibu. Ili kupata idadi ya sampuli ya wanafunzi, mtafiti aliandika neno NDIYO katika vijikaratasi kulingana na thuluthi ya idadi ya darasa. Kisha akaandika neno LA katika vijikaratasi kulingana na idadi iliyosalia.mtafiti alichanganya vijikaratasi vyote na akaviweka katika kisanduku,kisha akaomba kila mwanafunzi wa darasa husika aokote kijikaratasi kimoja.baadaye,mtafiti aliorodhesha wale wote ambao walipata vijikaratasi vilivyokuwa na neno NDIYO kama sampuli ya wanafunzi. Hatimaye,mtafiti alikuwa na wanafunzi 359 walioshiriki katika utafiti. Uteuzi wa walimu ulifanywa kutumia mbinu ya kimakusudi. Mbinu hii ilikuwa mwafaka kwa sababu ilimuwezesha mtafiti kuteua walimu waliokuwa wahusika katika ufundishaji na uandikaji wa insha katika lugha ya Kiswahili katika darasa la nane katika kata ya Ganze. Zaidi, walimu hawa ndio waliotoa ujumbe uliohitajika na mtafiti. Ujumbe wenyewe ulihusu wanafunzi wa darasa la nane na utendaji wao katika somo la Kiswahili insha. Iwapo shule ilikuwa na darasa la nane zaidi ya moja na somo la Kiswahili insha linafundishwa na walimu tofautitofauti, mtafiti aliteua mwalimu aliyekuwa katika jopo la somo la Kiswahili. Hatimaye,sampuli ya walimu ilikuwa walimu ishirini na wanne (24) Mbinu za kukusanya data. Seliger na Shahamy (1986), walitoa mapendekezo juu ya mbinu za kukusanya data inayohusu makosa wanayofanya wanafunzi wanapojifunza lugha ya pili.mapendekezo haya yalikuwa;

42 1. Wanafunzi wajibu maswali ya tafsiri kwenye hojaji. 2. Wanafunzi wapewe mjarabu wa insha. 3. Kuuliza wanafunzi wapewe vipindi vya kutamba hadithi. Kati ya mapendekezo haya, mtafiti alizingatia pendekezo la pili, (kutoa mjarabu wa insha) ambapo mada ilikuwa moja kwa kila shule teuliwa. Mbinu hii ilifuatilizwa kulingana na hatua za ukusanyaji wa data, zilizotolewa na Corder (1967). Data iliyokusanywa ni makosa ya kimofosintaksia katika insha za wanafunzi. Mbinu ya mjarabu ilikuwa faafu katika utafiti huu kwa sababu ndiyo iliyotoa data ya utafiti iliyohitajika Vifaa vya kukusanyia data. Mtafiti alitumia mjarabu wa insha katika kukusanya data ya utafiti. Mjarabu ulikuwa mwafaka katika utafiti huu kwa sababu, baada ya uandikaji wa insha, mtafiti aliweza kukusanya insha za wanafunzi na kuondoka nazo kwa usahihishaji.hali hii ilimfanya mtafiti kupata wakati mzuri wa kuzipitia insha za wanafunzi kwa makini ili kupata data iliyohitajika. Aidha, mtafiti alitumia maswali ya mahojiano kwa walimu, ambayo yalimuwezesha kuthibiti mapendekezo ya utafiti wake Uchanganuzi wa data. Baada ya kukusanya data, mtafiti aliichanganua kwa kutumia mchakato wa Corder (1967) katika Nadharia ya Uchanganuzi Makosa. Mchakato huu ulitumiwa kama mfumo wa uchanganuzi wa data. Hatua zilizofuatwa katika mfumo wa Corder (1967) ni:-

43 i) Kutambua makosa katika data iliyokusanywa. ii) Kutoa maelezo ya makosa kulingana na aina ya makosa yaliyoshughulikiwa katika utafiti. Mfano wa makosa ya kimofosintaksia yaliyochanganuliwa ni kama vile, ukosefu wa uwiano wa viambishi ngeli na viambishi njeo. iii) Kutafuta kiini cha makosa kwa kutumia uchanganuzi wa kithamano na wingidadi ambapo mbinu ya msambao wa umaratokezi na kipimo cha ulemeakati cha wastani wa kihesabu zilitumika. Uchanganuzi wa kithamano ambao ni wa kimaelezo ulitumika zaidi.

44 SURA YA NNE UCHANGANUZI NA UFASIRI WA DATA 4.1 Utangulizi Sura hii inahusu uchanganuzi na ufasiri wa data kwa lengo la kutambulisha makosa ya kisarufi katika insha za wanafunzi, kuainisha makosa hayo, kubainisha vyanzo vya makosa hayo, kutathmini makosa hayo, hatimaye, kupendekeza njia za kurekebisha makosa hayo. 4.2 Uchanganuzi na ufasiri wa data. Katika kuchanganua data, mtafiti alitumia Nadharia ya Uchanganuzi Makosa (N.U.M) iliyoasisiwa na Corder (1967), ikisaidiwa na Nadharia ya Uchanganuzi Linganuzi (N.U.L) ililyoasisiwa na Lado (1957). Hatua zilizofuatwa na mtafiti katika kuchanganua data ni za nadharia ya Corder (1967) ambazo ni : i. Kutambulisha makosa ya kisarufi katika data iliyokusanywa. ii. iii. iv. Kuainisha makosa ya kisarufi yaliyotambuliwa katika data ya utafiti. Kutafuta kiini cha makosa hayo. Kutathmini kiwango cha makosa hayo. v. Kurekebisha makosa ya kisarufi yaliyotambuliwa katika data ya utafiti. Mifano yote katika sura hii ilinukuliwa katika insha za wanafunzi wa darasa la nane(2014).

45 4.2.1 Kutambulisha makosa ya kisarufi katika insha za wanafunzi. Kulingana na hatua ya kwanza ya Corder (1967) ya kuchanganua data, mtafitianahitajikakutambulisha makosa katika maandishi ya wanafunzi. Ili kuendeleza hatua hii, mtafiti alipitia insha za wanafunzi na akapiga mstari chini ya sehemu zilizodhihirika kuwa na makosa ya kimofosintaksia.mtafiti alitambua makosa ya kisarufi katika insha za wanafunzi kutumia ujuzi wake wa sarufi ya lugha ya Kiswahili. Mfano wa sehemu ya insha iliyopitiwa na mtafiti.

46 4.2.2 Kuainisha makosa ya kisarufi katika insha za wanafunzi. Kulingana na Corder (1967), hatua ya pili ya uchanganuzi wa data ni kuainisha makosaya kisarufi yaliyotambulishwa katika kazi za wanafunzi. Katika kuendeleza hatua hii,mtafiti aliorodhesha makosa yote ya kisarufi aliyoyatambulisha katika kazi za wanafunzi.baadaye,mtafiti aliweka makosa haya katika makundi bainifu. Hatimaye, makosa ya kisarufi yaliyobainishwa yaliainishwa katika makundi yafuatayo; a) Makosa ya udondoshaji. b) Makosa ya uchopekaji. c) Makosa ya hijai / tahajia. d) Makosa ya mfuatano wa vipashio Makosa ya udondoshaji Kulingana na utafiti huu, udondoshaji ni kuacha mofimu, neno au maneno katika uundaji wa sentensi za lugha lengwa. Kuna aina mbalimbali za udondoshaji, lakini aina za udondoshaji zilizotambulishwa katika utafiti huu ni:- 1. Udondoshaji wa viambishi 2. Udondoshaji wa neno au maneno katika sentensi Udondoshaji wa viambishi Viambishi ni vipashio vyenye maana na hutokezea kabla au baada ya mzizi wa kitenzi au nomino ili kuleta maana iliyodhamiriwa.

47 Viambishi vinapotokezea kabla ya mzizi wa kitenzi au nomino hurejelewa kama viambishi awali na vinapotokezea baada ya mzizi wa nomino au kitenzi hurejelewa kama viambishi tamati X Mzizi wa Kitenzi Viambishi awali Viambishi tamati Viambishi vinapotumiwa kwa ufasaha huleta upatanisho wa kisarufi katika sentensi na vinapotumiwa kimakosa husababisha ukosefu wa upatanisho wa kisarufi katika sentensi. Mfano: Watoto amelala. Kiambishi awali a katika neno amelala, hakilingani na kiambishi cha wingi wa, kwa hivyo kiambishi a kilitumika kimakosa kwani, hakileti upatanisho wa kisarufi katika sentensi hii. Ili kuleta upatanisho wa kisarufi katika sentensi hii kiambishi a katika kitenzi lala kinastahili kuwa wa.

48 Katika nomino,viambishi awali hutumika katika unominishaji au wingi wa nomino. UNOMINISHAJI Kitenzi Una waza nini? Ukitaka kufaulu omba sana Alitembea polepole kama kobe. Nomino Kuwaza kwako ni bure Kuomba sana sio kujibiwa Kutembea polepole hakuchokeshi Jedwali 9 : Kielelezo cha viambishi awali katika unominishaji. UMOJA Mti huu ni mrefu. Kiti chake ni kipya. Wazo lako ni zuri. WINGI Miti hii ni mirefu. Viti vyake ni vipya. Mawazo yako ni mazuri. Jedwali 10:.Kielelezo cha viambishi awali katika umoja na wingi. Makosa ya udondoshaji wa viambishi yaliainishwa katika makundi yafuatayo; a) Makosa ya udondoshaji wa viambishi nafsi. b) Makosa ya udondoshaji wa viambishi njeo c) Makosa ya udondoshaji wa viambishi virejeshi d) Makosa ya udondoshaji wa viambishi shamirisho e) Makosa ya udondoshaji wa viambishi nomino katika sentensi.

49 a) Makosa ya udondoshaji wa viambishi nafsi. Kuna nafsi tatu, kila nafsi huwakilishwa na viambishi maalum. Viambishi vinavyowakilisha nafsi ni: Nafsi Kiwakilishi Viambishi umoja Viambishi wingi Kwanza Mimi ni tu Pili Wewe u m Tatu Yeye a wa Jedwali.11: Kielelezo cha nafsi na viwakilishi vyake. Viambishi nafsi huchukua nafasi ya mwisho kutoka mzizi wa kitenzi kuelekea kushoto. Mifano yote iliyotolewa kwa uchanganuzi, ilinukuliwa na mtafiti kutokana na insha za wanafunzi. Uchanganuzi wa kila sentensiiliyotolewa mfano, utafanywa kulingana na aina ya kosa linaloshughulikiwa katika sehemu husika. Iwapo sentensi ina makosa mengi, uchanganuzi utazingatia kosa linaloshughulikiwa katika sehemu hiyo na hayo mengine yatawachwa jinsi yalivyo. Mfano wa sentensi iliyodondoshwa viambishi nafsi katika kazi za wanafunzi ni: Tulipanda gari hilo tulikwenda hadi kwenye hoteli tukala, kunywa na hata kupumzika. Katika sentensi hii, mwanafunzi alidondosha kiambishi tu cha nafsi ya kwanza wingi katika vitenzi kunywa na kupumzika, kisha akachopeka kiambishi ku cha unominishaji.

50 Kulingana na maendelezo ya sentensi hii, vitenzi tukala, kunywa na kupumzika ni vitenzi sambamba kwani vimetokezea kwa mfululizo. Kwa hivyo,ili kuthibitisha hali hii, inastahili kiambishi ku kidondoshwe, badala yake kiambishi ka kichopekwe,kwani ka huwakilisha hali ya kutendeka na humaanisha kitendo kilitendeka na kufuatwa na ekingine. Baada ya kuchopeka kiambishi ka, vitenzi hivi ni lazima vianze na kiambishi tu cha nafsi ya kwanza ili kuleta upatanisho wa kisarufi. Kwa hivyo katika mazingira ya sentensi iliyotolewa mfano hapo juu, kisarufi, kitenzi kunywa kinapaswa kuwa tukanywa ilhali kupumzika kiwe tukapumzika Pia kiambishi nafsi huchukua nafasi ya pili kutoka kushoto kabla ya mzizi iwapo kitenzi kiko katika ukanusho wa hali ya wingi. Kwa mfano: Umoja wingi Nafsi ya kwanza Niliandika barua Hatukuandika barua Nafsi ya pili Nilirauka shambani Hamkurauka shambani Nafsi ya tatu Alisoma vizuri Hawakusoma vizuri Jedwali 12:Kielelezo cha viambishi nafsi kuchukua nafasi ya pili kabla ya mzizi katika vitenzi. Mtafiti alibaini sentensi zilizodondoshwa viambishi nafsi katika ukanusho wa hali ya wingi.

51 Miongoni mwa sentensi hizi ni: i) Wahenga ha*kuenda sege mnege walipolonga kuwa siku njema huonekana asubuhi. Katika sentensi hii, kiambishi wa cha nafsi ya tatu wingi kilidondoshwa katika nafasi iliyowekwa alama ya nyota. Kwa hivyo, kitenzi ha*kuenda kinapaswa kuwa hawakuenda. ii) Mwalimu alisema, mkiadhibiwa ha*tachelewa tena. Katika mfano (ii) kitenzi ha*tachelewa kilidondoshwa kiambishi m cha nafsi ya pili wingi.. Kwa hivyo, ili kufanya sentensi hii kuwa sahihi, kiambishi m kinastahili kuchopekwa katika nafasi ya pili ya kitenzi ha*tachelewa hatimaye, kitakuwa hamtachelewa. (b)makosa ya udondoshaji wa viambishi njeo. Viambishi njeo hurejelea wakati wa kitendo kutendeka. Kuna viambishi maalum katika kila wakati. Viambishi hivi ni kama vifuatavyo; Wakati Uliopo Uliopita Ujao Timilifu Mazoea Kiambishi kiwakilishi. -na- -li- -ta- -mehu- Jedwali 13: Kielelezo cha nyakati na viambishi viwakilishi husika.

52 Mtafiti alitambua makosa ya udondoshaji wa viambishi njeo katika tungo za wanafunzi. Miongoni mwa sentensi zilizodondoshwa viambishi njeo ni: Mfano 1. Ni*panda kwenye matatu mhadi pale alipokuwa anaishi. Katika mazingira ya sentensi hii, kitenzi ni*panda kilidondoshwa kiambishi li cha wakati uliopita. Udondoshaji huu umepoteza upatanisho wa kisarufi katika sentensi hii, kwa hivyo kiambishi li cha wakati uliopita kinapaswa kuchopekwa katika nafasi iliyowekwa alama (*).Vilevile, kuna viambishi ambavyo huwakilisha hali. Viambishi hivi huwa havionyeshi wakati maalum wa kutendeka kwa kitendo bali huonyesha hali. Kati ya hali hizi ni hali ya mfululizo, yaani kitenzi kimoja kutendeka baada ya kingine. Miongoni mwa viambishi vinavyotumika kuwakilisha hali hii ni ka na ki.viambishi hivi hutumika ili kuwakilisha nyakati mbalimbali kulingana na maendelezo ya senteni husika. Kwa mfano; Tulienda tukiimba mpaka tukaingia mjini. Katika sherehe hiyo, tulikula, tukanywa,tukacheza,kisha tukalala. Katika data ya utafiti, mtafiti alibaini makosa ya udondoshaji wa viambishi ka na ki vya wakati katika baadhi ya sentensi zilizotungwa na wanafunzi. Kwa mfano: 1. Tuling oa nanga tu*elekea kwa majirani ili tu*jue ni nini kimetokea.

53 Vitenzi tu*elekea na tu*jue vilidondoshwa kiambishi ka cha wakati. Katika mazingira ya sentensi hii, kiambishi ka kinastahili kuonyesha kuwa kuna kitendo fulani kilichotendeka ndipo kitendo kingine kikafuata (hali yake). Kwa hivyo, katika sentensi iliyotolewa hapo juu, kitenzi cha kwanza ni tuling oa ambacho kiko katika wakati uliopita. Kitenzi hiki kinastahili kufuatwa na kitenzi kilichoambishwa na kiambishi ka cha wakati. Kitenzi tuelekee kinapaswa kuwa tukaelekea ilhali tujue kiwe tukajue.hatimaye sentensi ingekuwa; Tuling oa nanga tukaelekea kwa majirani ili tukajue ni nini kimetokea, badala ya Tuling oananga tuelekea kwa majirani ili tujue ni nini kimetokea. Mfano (ii) Tulikuwa tusubiri gari wakati shangazi akiwasili. Kitenzi cha kwanza ni tulikuwa ambacho kiko katika wakati uliopita. Kitenzi cha pili ni tusubiri ambacho hakina kiambishi chochote kinachowakilisha njeo. Kwa hivyo, kiambishi ambacho kinastahili kuchopekwa katika kitenzi tusubiri. Kiambishi ki kinapaswa kuchukua nafasi baada tu ya kiambishi tu cha nafsi. Hatimaye, sentensi itakuwa; Tulikuwa tukisubiri gari wakati shangazi akiwasili. (c Makosa ya udondoshaji wa viambishi virejeshi Virejeshi ni viambishi vinavyorejesha nomino kwa kitendo, kwani hurejelea nomino ambazo habari zake zinatolewa. Kuna virejeshi mbali mbali katika lugha ya Kiswahili.

54 Miongoni mwa virejeshi hivi ni kirejeshi o na kirejeshi amba. Mifano ya virejeshi katika sentensi ni kama ifutavyo: VIREJESHI Kirejeshi o kati Kirejeshi o tamati Virejeshi amba 1 Dada anayelima ni mzuri Dada alimaye ni mzuri Dada ambaye analima ni mzuri. 2 Kiatu kitakachokatika ni changu Kiatu kikatikacho ni changu Kiatu ambacho kinakatika ni changu 3 Gari linaloegeshwa ni bovu Gari liegeshwalo ni bovu Gari ambalo linaegeshwa ni bovu. Jedwali 14:Kielelezo cha aina za virejeshi Kulingana na mifano ya sentensi iliyotolewa hapo juu ni wazi kwamba, nafasi ya virejeshi o- kati ni baada tu ya kiambishi cha wakati katika vitenzi ikiwa nafasi ya virejeshi otamati ni mwisho wa kitenzi kuelekea kulia baada ya mzizi na viambishi vingine. Nayo nafasi ya kirejeshi amba ni baada ya kitenzi kisaidizi amba. Kuna sentensi zilizobainika kuwa na udondoshaji wa virejeshi katika insha za wanafunzi. Miongoni mwa sentensi hizi ni: 1. a) Maswali mengi yalinijia kichani name nikakumbuka jinsi nili*muacha abu yangu. b)maswali mengi yalinijia kichwani name nikakumbuka jinsi nilivyomuacha abu yangu. 2. a)alikuwa na raha kama mama ajifungua* pacha.

55 b )Alikuwa na raha kama mama ajifunguaye pacha. 3. a)nilianza kuparaga muembe amba* ulikuwa umejaa maembe. b)nilianza kuparaga muembe ambao ulikuwa umejaa maembe. Kulingana na mifano iliyotolewa hapo juu, sentensi l (a), 2(a) na 3(a) zilidondoshwa virejeshi. Sentensi hizi zina ukosefu wa uwiano wa kisarufi. Na baada ya marekebisho kufanywa katika sentensi 1(b), 2(b), na 3(b) uwiano wa kisarufi umejitokeza. Kwa hivyo, udondoshaji wa viambishi virejeshi husababisha ukosefu wa uwiano wa kisarufi. Vilevile, kiambishi ji hutumika kama kirejeshi. Kiambishi ji hurejelea nomino inayojitenda kitendo. Makosa ya udondoshaji wa kiambishi ji ulidhihirika katika baadhi ya sentensi zilizotungwa na wanafunzi katika uandikaji wa insha. Kwa mfano: 1. a) Jamii ilikuwa maskini hohehahe haikuwa na hali yoyote ya ku*saidia katika maisha yake. b) Jamii ilikuwa maskini hohehahe haikuwa na hali yoyote ya kujisaidia katika maisha yake. 2. a) Tuli*panga wawili wawili ili kutumia chakula tulichokuwa tumepikiwa. b) Tulijipanga wawili wawili ili kutumia chakula tulichokuwa tumepikiwa. Aidha, sentensi l (a) na 2(a) zilizotolewa hapo juu, zilizodondoshwa kiambishi ji cha kirejeshi. Sentensi hizi pia zimekosa upatanisho wa kisarufi. Baada ya marekebisho sentensi 1(b) na 2(b) zimejitokeza zikiwa na uwiano wa kisarufi.

56 b) Makosa ya udondoshaji wa viambishi shamimirisho. Viambishi shamirisho hurejelea kiumbe au kitu kinachoathiriwa na kitenzi katika usemi. Viambishi virejeshi pia hurejelewa kama mtendwa au mtendewa. Viambishi shamirisho huchukua nafasi ya kwanza baada ya mzizi kuelekea kushoto. Kati ya sentensi zilizobainika kudondoshwa viambishi shamirisho ni: 1(a)Masahibu wangu wali*pokea kwa furaha (b)masahibu wangu walinipokea kwa furaha 2 (a)modi alipata mpira na aka*piga safari b)modi alipata mpira na akampigia safari. Katika sentensi 1(a) na 2(a), nafasi zilizowekwa alama (*) zimedondoshwa viambishi shamirisho. Sentensi 1(a) imedondoshwa kiambishi ni ilhali sentensi 2(a) imedondoshwa kiambishi m. Kisarufi, sentensi 1(a) inastahili kusoma kama 1(b) ilhali 2(a) inanstahili kusoma kama 2(b). Hitimisho la makosa ya udondoshaji wa viambishi katika vitenzi. Viambishi vya nafsi,njeo virejeshi na viambishi shamirisho ni viambishi katika vitenzi.hivyo basi,kulingana na matokeo ya utafiti, makosa ya udondoshaji wa viambishi katika vitenzi husababisha ukosefu wa upatanisho wa kisarufi katika sentensi za lugha ya Kiswahili. Kila lugha ina sheria zake na ili kuweza kuwa na umilisi wa lugha fulani,inapasa mwanafunzi awe na ufasaha wa sheria za lugha lengwa na aweze kuzitumia kwa usahihi.

57 Wanafunzi walioshiriki katika utafiti, walikosa ufahamu wa sheria za mpangilio wa viambishi katika vitenzi, ndipo makosa haya yakatokezea. Mpangilio wa viambishi katika vitenzi huwa na mfuatano huu; Viambishi awali Mzizi wa Kitenzi Viambishi tamati X Nafsi Njeo Kirejeshi Shamirisho Kauli Kiishio (Mtendwa) (K) (ksh) (Mtendi) (Sh) Nafsi Njeo kirejeshi (Nfs) (nj) (krj) Sheria Nafsi + Njeo + kirejeshi +Shamirisho + X + Kauli + kiishio Sheria Nfs + Nj + krj + sh + X + K + ksh. Si lazima viambishi vyote vijitokeze katika vitenzi katika sentensi. Jambo la kuzingatia ni,ukaribu wa kiambishi na mzizi wa kitenzi.

58 (e) Makosa ya udondoshaji wa viambishi vya mahali. Nomino inaweza kuambishwa ili kuonyesha mahali maalum. Kiambishi kinachotumika katika hali hii ni kiambishi ni cha mahali kikiwa kiambishi tamati. Kwa mfano: i) Mbuzi ameingia shambani ii) Babu yuko garini akielekea Mombasa. Mtafiti alitambua kuweko kwa makosa ya udondoshaji wa kiambishi ni cha mahali katika data ya utafiti.baadhi ya makosa haya ni; 1. a)nikaanza kujiandaa nielekee ilikanisa* b)nikaanza kujiandaa ili nielekee kanisani 2. a)hakuwa na la kusea imla kuenda nyumba* b)hakuwana lakus akuenda nyumbani 3. a)tulipomaliza tulifunga kuni zetu tukaziwekakivuli*. b)tulipomaliza tulifunga kuni zetu tukaziweka kivulini. 4. a)nilichukua mkoba wangu wa vitanu na kuelekeashule* b)nilichukua mkoba wangu wa vitabu na kuelekea shuleni. Sentensi 1(a), 2(a), 3(a), na 4(a), zimedondoshwa kiambishi ni cha mahali. Sentensi hizi zimekosa upatanisho wa kisarufi. Na baada ya kiambishi ni cha mahali kuwekwa katika nomino husika katika sentensi 1(b), 2(b) 3(b), na 4(b), sentensi hizi zinaupatanisho wa kisarufi kwa hivyo, kisarufi sentensi hizi sahihi.

59 Makosa ya udondoshaji wa neno au maneno katika sentensi. Lugha ya Kiswahili ina aina mbalimbali za maneno. Maneno haya yakiwa ni nomino, vitenzi,vielezi, vivumishi, viunganishi,viwakilishi,vihusishi na vihisishi. Maneno haya hutumika katika uundaji wa tungo za lugha ya Kiswahili.Uundaji wa tungo hizi huzingatia uhusiano wa neno kwa neno. Kulingana na data iliyokusanywa, makosa ya udondoshaji wa neno au maneno yaliainishwa kulingana na aina za maneno yaliyodondoshwa. Hatimaye, makundi yafuatayo yalibainishwa. a) Makosa ya udondoshaji wa vivumishi katika sentensi b) Makosa ya udondoshaji wa vitenzi katika sentensi. c) Makosa ya udondoshaji wa vielezi katika sentensi. d) Makosa ya udondoshaji wa vihusishi katika sentensi e) Makosa ya udondoshaji wa nomino katika sentensi f) Makosa ya udondoshaji wa nomino pamoja na vihusishi katika sentensi g) Makosa ya udondoshaji wa viwakilishi katika sentensi. (a) Makosa ya udondoshaji wa vivumishi katika sentensi. Vivumishi ni maneno yanayotoa maelezo zaidi juu ya nomino. Kuna aina mbalimbali za vivumishi katika lugha ya Kiswahili. Makosa ya udondoshaji wa vivumishi yaliainishwa kulingana na aina ya vivumishi vilivyodondoshwa.makundi mawili makuu yaliweza kubainishwa. (i) Makosa ya udondoshaji wa vivumishi virejeshi (ii) Makosa ya udondoshaji wa vivumishi vimilikishi.

60 (i) Makosa ya udondoshaji wa vivumishi virejeshi katika sentensi. Vivumishi virejeshi ni maneno yanayorejelea nomino inayozungumziwa katika sentensi. Nafasi yake katika sentensi ikiwa ni baada tu ya nomino husika. Kwa mfano: (a)mtu huyo aliingia garini bila shati (b)harusi hiyo ilifana sana Miongoni mwa sentensi zilizodondoshwa vivumishi virejeshi ni: 1. a) Naye asiyekuwa na mwana siku * alieleka jiwe. b) Naye asiyekuwa na mwana siku hiyoalieleka jiwe. 2. a)baada ya nusu saa kupita, kasisi wa kanisa * alisimama kidete kisha akasalimia umati b) Baada ya nusu saa kupita, kasisi wa kanisa hiyo alisimama kidete kisha akasalimia umati. (ii) Makosa ya udondoshaji wa vivumishi vimilikishi. Vivumishi vimilikishi ni maneno yanayoonyesha kuwa kitu fulani kimemilikiwa na mtu au kitu fulani, kwa mfano: a) Nguo yangu ni nzuri b) Mchumba wangu ameng oa mtunguja. 1. a)nami nilimfuata unyounyo kama mtu na kivulivuli * b) Nami nilimfuata unyounyo kama mtu na kivulivuli chake.

61 2. a) Alipoangalia ndani alimkuta mume * na akaanza kumuuliza maswali. b) Alipoingia ndani alimkuta mume wake na akaanza kumuuliza maswali. Katika sentensi 1(a) na 2(a) hapo juu, vivumishi vimilikishi chakena wake vimedondoshwa. Katika sentensi 1(a) nomino mtu imehusishwa na kuvulivuli. Katika mazingira ya sentensi hizi, nomino hizi zinamiliki vitu maalum. Ikiwa nomino mtu 1(a) inamiliki kivulivulina anayezungumziwa katika sentensi 2(a) ni bibi ambaye anamilikimume. Kwa hivyo, ambazo zingetumiwa na wanafunzi wahusika ni 1(b) na 2(b) badala ya 1(a) na 2(a). (b) Makosa ya udondoshaji wa vitenzi katika sentensi. Vitenzi ni maneno yanayoelezea jambo linalofanywa. Kuna aina mbalimbali za vitenzi. Miongoni mwa aina za vitenzi ni vitenzi vikuu na vitenzi visaidizi. Sentensi za lugha ya Kiswahili lazima ziwe na vitenzi. Sentensi inaweza kuwa na kitenzi kimoja au zaidi. Katika hali hii, wanafunzi hutumia vitenzi katika sentensi na bila kujua wakaacha vitenzi vingine katika sentensi hiyo hiyo. Hali hii husababisha kuathirika kwa sentensi. Kwa mfano: 1. a)mwalimu wa Kiswahili aliingia darasani na kuanza * somo la Kiswahili. b)mwalimu wa Kiswahili aliingia darasani na kuanzakutufundishasomo la Kiswahili. 2. a)muda si muda tulifika shuleni salama salmini * na furaha na buraha. b)muda si muda tulifika shuleni salama salmini tukiwana furaha na buraha.

62 ( c ) Makosa ya udondoshaji wa vielezi katika sentensi. Vielezi ni maneno yanayofafanua vitenzi, vivumishi na vielezi vyengine katika sentensi. Kwa mfano. Dada aliandika vizuri sana. N T E E Katika sentensi iliyotolewa hapo juu, neno vizuri ni kielezi kinachofafanua jinsi kitenzi andika kilivyofanyika ilhali kielezi sana kinafafanua kielezi. Data ya utafiti ilidhihirisha wazi kwamba wanafunzi wachache walidondosha baadhi ya vielezi katika sentensi chache walizotumia katika uandikaji wa insha. Sentensi zifuatazo zilinukuliwa kutokana na insha za wanafunzi zikiwa na udondoshaji wa vielezi. Mfano; (i) Yule mwalimu aliniuliza * nini sikubeba kifaa chochote. Katika nafasi iliyoashiriwa na alama ya nyota, kuna kielezi kilichodondoshwa ambacho kinastahili kueleza au kufafanua kitenzi aliniuliza. Kwa hivyo, kielezi mwafaka kinachopaswa kuchopekwa katika nafasi hii ni kwa. Kielezi kwa ndicho ambacho kingeeleza kitenzi aliniuliza. Baada ya kielezi kwa kuchopekwa katika nafasi iliyoko na alama (*) sentensi hii (Mf. i) inastahili kuwa; Yule mwalimu aliniulizakwanini sikubeba kifaa chochote.

63 Mfano; (ii) Hakuna adinasi aliyejibu hata* Sentensi hii haina kielezi cha kubaini kiwango cha majibu kinachoelezewa na kielezi hata. Hii inamaana ya kwamba, hata ni kielezi ambacho kinastahili kufafanuliwa zaidi. Kielezi kinachofaa kutumika ni kidogo katika nafasi ya mwisho wa sentensi. Hatimaye, sentesi inastahili kuwa; Hakuna adinasi aliyejibu hata kidogo. (d) Makosa ya udondoshaji wa vihusishi katika sentensi. Vihusishi ni maneno yanayoonyesha uhusiano baina ya vitu viwili katika sentensi. Vitu hivi huwa ni maneno, ambayo ni nomino katika sentensi. Mtafiti alitambulisha makosa ya udondoshaji wa vihusishi katika baadhi ya sentensi katika data ya utafiti. Pamoja na sentensi hizi ni; Mfano (i) Baada ya muda * nipe nikupe matwana hiyo ilibingirika bingiribingiri Katikati ya nomino muda na nipe panastahili kuwa na kihusishi ili kuonyesha uhusiano baina ya nomino hizi mbili. Kihusishi mwafaka katika sentensi hii ni wa. Hivyo, sentensi hii inapaswa kuwa; Baada ya muda wa nipe nikupe matwana hiyo ilibingirika bingiribingiri.

64 Mfano(ii) Basi tajiri huyu alipitia katikati * mji ule pale palikuwa watu wale ambao walikuwa hawana kazi wala basi. Mwanafunzi mhusika wa sentensi hii, aliacha kihusishi ya ambacho kingeonyesha uhusiano baina ya sehemu aliyopitia tajiri (katikati) na mji. Baada ya uchopekaji wa kihusishi ya katika nafasi yake, sentensi hii itakuwa; Basi tajiri huyu alipitia katikati ya mji ule pale palikuwa watu wale ambao walikuwa hawana kazi wala basi. Mfano (iii) Wakati huo ulikuwa * likizo ya mwezi wa Disemba Kulingana na maendelezo ya sentensi hii, nomino wakati inastahili kuhusiana na nomino likizo. Uhusiano huu unatoa nafasi ya matumizi ya kihusishi hususan kihusishi wa ambacho kiliwachwa na mwanafunzi mhusika. Hatimaye sentensi itasoma 'Wakati huo ulikuwawa likizo ya Disemba. (e) Makosa ya udondoshaji wa nomino katika sentensi. Nomino ni jina la kiumbe, kitu au mahali. Sentensi za lugha ya Kiswahili zinaweza kuwa na nomino moja au zaidi.data ya utafiti ilidhihirisha kuwa wanafunzi walifanya makosa ya kudondosha nomino katika baadhi ya sentensi walizotumia katika uandikaji wa insha.

65 Ifuatayo ni mifano ya sentensi zilizodondoshwa nomino na zilitokana na insha za wanafunzi. Mfano; (i) Wenyewe tukapanda mtini tukacheza vya kutishiana Katika sentensi hii vya ni kihusishi japokuwa kilitumiwa kimakosa kisarufi, kihusishi hutangulia nomino, lakini sentensi iliyotolewa hapo juu, mwanafunzi mhusika alitanguliza kihusishi baada ya kitenzi (tukacheza). Hili ni thibitisho kuwa kuna nomino iliyodondoshwa. Nomino yenyewe ikiwa ni mchezo ambayo kihusishi chake ni wa. Kwa hivyo katika mazingira ya sentensi (Mf :i) hapo juu, kihusishi vya ni lazima kibadilishwe ili sentensi iweze kuwa na upatanisho wa kisarufi. Hatimaye sentensi hii inapaswa kusoma, Wenyewe tukapanda mtini tukacheza mchezo wa kutishiana. (f) Makosa ya udondoshaji wa nomino pamoja na vihusishi katika sentensi. Katika maendelezo ya sentensi ambayo ina kihusishi, nomino huchukua nafasi kabla ya kihusishi.kulingana na kanuni hii, ni rahisi mwanafunzi kuacha nomino na kihusishi chake katika uundaji wa sentensi. Sentensi zifuatazo zinatoa thibitisho la hali hii. Alama mbili za nyota (**) zilizotumiwa katika mifano ya sentensi, alama ya kwanza inaashirianafasi ya nomino na ya pili inaashiria nafasi ya kihusishi.

66 Mfano; (i) Baada ya * * sekunde kuvunja ugo na kuwa dakika, tulisikia mlio wa gari ya maanzili. Katika mazingira ya sentensi hii, sekunde kuvunja ungo kuna maanisha muda wa dakika kutimia baada ya sekunde sitini. Aidha sekunde pekee haiwezi kuunda dakika. Kwa hivyo katika alama (*) ya kwanza panastahili kuwa na nomino muda kisha ifuatilizwe na kihusishi chake cha upatanisho wa kisarufi ambacho ni wa katika alama (*) ya pili. Hivyo basi, sentensi inapaswa kuwa; Baada ya muda wa sekunde kuvunja ungo na kuwa dakika, tulisikia mlio wa gari ya maanzili. Mfano (ii) Shangazi alimtuma mtoto wake dukani akanunue vitu vya * * mchana. Mwanafunzi alitumia vitu vya nomino na kihusishi katika sentensi. Maneno haya hayatoi maelezo kamili ya ujumbe ambao mwanafunzi alikusudia kutoa. Vitu ikiwa nomino ya kawaida, haijaeleza kama vitu vya mchana vilikuwa vitu gani kwani mchana una vitu tofautitofauti ambavyo hununuliwa. Kwa hivyo, mwanafunzi angetumia ufafanuzi zaidi wa vitu hivi kwa kuongezea nomino chakula na kihusishi cha. Hatimaye, katika nafasi zinazoashiria udondoshaji katika sentensi hii zingekuwa na chakula cha. Nayo sentensi ingesomwa, Shangazi alimtuma mtoto wake dukani akanunue vitu vya chakula cha mchana.

67 (g) Makosa ya udondoshaji wa nomino na kitenzi katika sentensi. Mtafiti alibaini sentensi ambazo wanafunzi walidondosha nomino na kitenzi katika nafasi mbalimbali katika sentensi moja. Kwa mfano; Yote hayo yalimalizika * ambapo jua * likicheza donedone katikati ya miti na kuiaga miti na kupisha mwezi. Katika nafasi ya kwanza, nomino wakati ilidondoshwa ilhali katika nafasi ya pili mwanafunzi alidondosha kitenzi lilikuwa. Maneno haya yanapowekwa katika nafasi zao na sentensi kuandikwa upya, sentensi hii itakuwa; Yote hayo yalimalizika wakati ambapo jua lilikuwa likicheza donedone katikati ya miti na kuiaga miti na kupisha mwezi Makosa ya uchopekaji Kulingana na kipengele cha mofosintaksia, makosa ya uchopekaji ni kuweka mofimu, neno au maneno mahali yasipotakikana katika sentensi. Katika data ya utafiti, makosa ya uchopekaji yaliainishwa katika makundi makuu mawili. (i) (ii) akosa ya uchmakosa ya uchopekaji wa viambishi (mofimu) Mopekaji wa neno au maneno katika sentensi Makosa ya uchopekaji wa viambishi katika sentensi Makosa ya uchopekaji wa viambishi yaliainishwa katika makundi yafuatayo:

68 a) Makosa ya uchopekaji wa viambishi virejeshi. b) Makosa ya uchopekaji wa viambishi njeo. c) Makosa ya uchopekaji wa viambishi ngeli. d) Makosa ya uchopekaji wa viambishi vya umoja na wingi. e) Makosa ya uchopekaji wa viambishi vya mnyambuliko wa vitenzi (Kauli). f) Makosa ya uchopekaji wa viambishi vya ukanusho. g) Makosa ya uchopekaji wa viambishi vya mahali. (a) Makosa ya uchopekaji wa viambishi virejeshi katika sentensi. Kutokana na data ya utafiti, ilibainika wazi kwamba wanafunzi hufanya makosa ya kutumia viambishi virejeshi visivyokuwa sahihi katika sentensi husika. Kwa mfano: 1. a)nilitimua mbio hata sikutaka kumwambia saibu yangu kuwa mwenye shamba ndio huyo. b)nilitimua mbio hata sikutaka kumwambia saibu yangu kuwa mwenye shamba ndiye huyo. 2. a)yalionifanya kuwa na raha ni kuwa nilikuwa ninaasi ukapera na kidosho mrembo kama tausi. b)yaliyonifanya kuwa na raha ni kuwa nilikuwa ninaasi ukapera na kidosho mrembo kama tausi. Sentensi 1(a) na 2(a) zimechopekwa kiambishi cha o rejeshi ambacho si sahihi. Badala yake, sentensi 1a ilikuwa inastahili kutumia kirejeshi ye kikimrejelea mwenye shamba,

69 ilhali sentensi 2(a) ilikuwa inastahili kuwekwa kiambishi kirejeshi yo ili kurejelea mambo hayo. Hivyo 1(b) na 2(b) ndizo sentensi sahihi. (b) Makosa ya uchopekaji wa viambishi njeo katika sentensi. Viambishi njeo ni mofimu zinazofahamisha wakati kitendo kilifanyika, kinafanyika au kitafanyika. Mofimu za njeo huwakilisha nyakati tofautitofauti. (taz.jedwali 12) Kwa mfano: (i) Nilienda dukani kununua unga. (iii) Dada anafua nguo. Wanafunzi hufanya makosa ya kutumia viambishi vya njeo visivyokuwa sahihi katika sentensi husika. Miongoni mwa sentensi zilizokuwa na makosa haya kutokana na data ya utafiti ni: Kwa mfano, Alikabwa mikono yake kwa pingu huku machozi yamemtoka. Sentesi hii ina vitenzi viwili. Kimoja kilifanyika kikiwa chengine kinaendelea. Katika hali hii, kitenzi cha kwanza katika sentensi huwa na kiambishi li kuonyesha wakati kamili wa kutendeka kitendo kisha kitenzi cha pili huwa na kiambishi bayana cha wakati kadiri ya hali. Kiambishi hiki huwa hakionyeshi wakati kamili wa kutendeka kwa kitendo bali huonyesha hali fulani. Kitenzi cha kwanza alikabwa kina mofimu li ya wakati uliopita ilhali kitenzi cha pili yamemtoka kina mofimu me ya wakati timilifu.

70 Kulingana na kanuni za matumizi ya viambishi njeo na mazingira ya sentensi me haistahili kuwa katika kitenzi ya hali ingetumika, hususani mofimu ki,. Hatimaye, sentensi inastahili kuwa. Alikabwa mikono yake kwa pingu huku machozi yakimtoka badala ya, Alikabwa mikono yake kwa pingu huku machozi yamemtoka. Aidha,kuna sheria za matumizi ya mofimu za njeo katika uandikaji wa tungo za lugha ya Kiswahili zikiwa katika usemi wa taarifa au usemi halisi.miongoni mwa sheria hizi ni; Iwapo sentensi iko katika wakati uliopita na katika usemi halisi, mofimu ta hutumika. Sentensi hiyo hiyo hubadilishwa katika usemi wa taarifa kwa kutumia mofimu nge ya wakati badala ya mofimu ta Kwa mfano: Mwalimu alisema, Nitafika shule kuchelewa, (usemi halisi). Mwalimu alisema ya kwambaangefika shule kuchelewa (usemi wa taarifa) Kulingana na data ya utafiti, ilithibitika wazi kwamba baadhi ya wanafunzi wana utofahamu wa sheria hii. Hivyo wanafunzi hufanya makosa ya matumizi ya mofimu hizi. Kwa mfano: 1(.a) Nilimuuliza maswali lakini aliendelea kuniambia kwamba nitakwambia tukifika. (b) Nilimuuliza maswali lakini aliendelea kuniambia kwamba angenijibu tukifika. 2(a) Alisema baba atakuja karibuni. (b) Alisema baba angekuja karibuni.

71 Kulingana na mifano iliyotolewa hapo juu, ni wazi kwamba, makosa ya uchopekaji wa viambishi njeo husababisha ukosefu wa upatanisho wa kisarufi katika sentensi. (c) Makosa ya uchopekaji wa viambishi ngeli katika sentensi Ngeli ni makundi ya nomino yenye sifa zinazofanana kisarufi katika lugha ya Kiswahili. Makundi haya hubainishwa na viambishi vya umoja na wingi vinavyochopekwa kama viambishi awali katika vitenzi katika sentensi za lugha ya Kiswahili. Kwa mfano: Umoja Wingi Ngeli Mtoto analia Watoto wanalia A-WA Mti umeanguka Miti imeanguka U-I Nguo yangu imechafuka Nguo zangu zimechafuka I-ZI Jedwali 15: Kielelezo cha Viambishi ngeli katika sentensi. Kulingana na data ya utafiti, mtafiti aliainisha makosa haya katika makundi mbalimbali. Makundi yaliainishwa kulingana na aina ya ngeli ambayo ingekuwa sahihi katika sentensi husika. Hatimaye, makundi yafuatayo yalibainishwa wazi; (i) Makosa ya uchopekaji wa ngeli nyingine badala ya ngeli ya A WA. (ii) (iii) (iv) (v) Makosa ya uchopekaji wa ngeli nyingine badala ya ngeli ya U ZI. Makosa ya uchopekaji wa ngeli nyingine badala ya ngeli ya LI YA. Makosa ya uchopekaji wa ngeli nyingine badala ya ngeli ya I ZI. Makosa ya uchopekaji wa ngeli nyingine badala ya ngeli ya KI VI. (vi) Makosa ya uchopekaji wa ngeli nyingine badala ya ngeli ya U I.

72 (vii) Makosa ya uchopekaji wa ngeli nyingine badala ya ngeli ya YA YA. (i) Makosa ya uchopekaji wa viambishi vyingine badala ya ngeli ya A WA. Ngeli hii hutumika katika upatanisho wa kisarufi wa nomino za viumbe katika sentensi za lugha ya Kiswahili. Kwa mfano: Mbuzi ameingia shambani. Mbuzi wameingia shambani. Nomino mbuzi iko katika ngeli ya A WA. Data ya utafiti ilikuwa na sentensi ambazo zilihusishwa na viambishi ngeli visivyokuwa vya nomino husika. Kwa mfano; (i )Tulipofika hapo mahuluki wa aila hiyo inalia sana. Katika kitenzi inalia, mofimu i ni kiambishi ngeli ambacho kinarejelea nomino mahuluki katika sentensi hii. Ikiwa mahuluki ni nomino inayoregelea kiumbe au binadamu, mofimu i haistahili kutumiwa. Mofimu ambayo ni sahihi ni mofimu wa kama kiambishi ngeli kwani nomino mahuluki iko katika ngeli ya A WA. Katika mazingira ya sentensi, mofimu wa ni mofimu ya wingi kwa hivyo, sentensi hii inastahili kuwa; Tulipofika hapo mahuluki wa aila hiyo wanalia sana.

73 Mfano (ii) ; Ilikuwa siku ya likizo ambapo jamaa zangu alikuwa furaha tele. Nomino jamaa inamilikiwa na kivumishi zangu kumaanisha kuwa iko katika hali ya wingi. Kitenzi kinachoambatana na nomino jamaa ni alikuwa. Kitenzi alikuwa kinaeleza kuhusu jamaa katika umoja kwa sababu ya kiambishi ngeli a kilichotumiwa. Mwanafunzi mhusika wa sentensi hii alitakikana kutumia kiambishi ngeli cha wingi ambacho ni wa kwani jamaa ni nomino ya viumbe na iko katika ngeli ya A WA. Hatimaye, sentensi inapasa kusoma. Ilikuwa siku ya likizo ambapo jamaa zangu walikuwa furaha tele. (ii)makosa ya uchopekaji wa ngeli nyingine badala ya ngeli ya U ZI Ngeli ya U ZI inahusu nomino ambazo upatanisho wake wa kisarufi huwa kiambishi awali u katika umoja wa zi katika hali ya wingi. Sentensi zilizojitokeza katika data ya utafiti zikiwa na makosa haya ni pamoja na; Mfano (i) Tuliabiri gari hilo huku nyuso zetu zikiwa vimejaa joho la tabasamu. Katika kitenzi vimejaa, mofimu vi inaregelea nomino nyuso. Matumizi ya mofimu vi katika sentensi hii, yamesababisha ukosefu wa upatanisho wa kisarufi sababu ikiwa, mofimu vi haiambatani na nomino nyuso, kwani nyuso ni nomino katika ngeli ya U ZI. Kwa hivyo, mofimu vi ikiwa mofimu ya hali ya wingi, inastahili kudondoshwa badala yake mofimu zi ichopekwe. Mwishoni, sentensi inastahili kuwa;

74 Tuliabiri gari hilo huku nyuso zetu zikiwa zimejaa joho la tabasamu. Mfano (ii); Ilikuwa ni wakati wa macheo tuliporejea manzilini kutoka shuleni. Kulingana na maendeleo ya sentensi iliyotolewa mfano hapo juu, kiambishi awali i katika kitenzi kisaidizi ilikuwa, kimerejelea nomino wakati. Nomino wakati ikiwa katika ngeli ya U ZI, kiambishi i kilitumika kimakosa. Wakati ikiwa ni nomino ya umoja, kiambishi ngeli sahihi ambacho kilistahili kutumiwa ni kiambishi u. Nayo sentensi ingesoma; Ulikuwa wakati wa macheo tuliporegea manzilini kutoka shuleni. (iv) Makosa ya uchopekaji wa ngeli nyingine badala ya ngeli ya LI YA Nomino za ngeli ya LI YA huchukuwa kiambishi awali li katika umoja na ya katika hali ya wingi katika upatanisho wa kisarufi. Data ya utafiti ilibainisha kuwa wanafunzi huchopeka viambishi makosa katika vitenzi badala ya viambishi ngeli vya ngeli ya LI YA. Makosa haya yalidhibitishwa katika baadhi ya sentensi zilizotumiwa na wanafunzi. Kwa mfano; Ghafla bin vu gari moja ikaja kasi sana na ikanigonga na ikaniumiza mkono wangu. Katika sentensi iliyotolewa mfano hapo juu, mwanafunzi alitumia mofimu i ya upatanisho wa kisarufi katika vitenzi ikaja,ikanigonga na ikaniumiza. Mofimu i ilitumika kimakosa kwa sababu, nomino inayoregelewa na mofimu hii ni gari. Ili kuleta upatanisho

75 wa kisarufi,nomino gari huchukua kiambishi ngeli li katika umoja na ya katika hali ya wingi. Kwa hivyo, badala ya kiambishi ngeli i katika vitenzi ikaja, ikanigonga na ikaniumiza katika sentensi iliyotolewa hapo juu, mwanafunzi alitakikana kutumia kiambishi ngeli li. Hivyo, sentensi ingesoma; Ghafla bin vu gari moja likaja kasi sana na likanigonga na likaniumiza mkono wangu. (iv). Makosa ya uchopekaji wa viambishi ngeli vingine badala ya viambishi ngeli vya ngeli ya I ZI. Katika upatanisho wa kisarufi, nomino za ngeli ya I ZI huchukua kiambishi awali i katika hali ya umoja na kiambishi ngeli zi katika hali ya wingi. Mtafiti alibaini kwamba wanafunzi hufanya makosa ya kutumia viambishi ngeli vya nomino nyingine katika upatanisho wa kisarufi wa nomino za ngeli ya I ZI. Baadhi ya sentensi zilizotambulishwa zikiwa na makosa haya ni Mfano: Polisi walikuwa na kazi ngumu ya kuzima moto huo.wakabidi kuwaita zimamoto. Ujumbe anaotoa mwanafunzi unahusu hali ya kazi. Hivyo, nomino inayohusika zaidi katika sentensi hii ni hali japo nomino yenyewe haikuandikwa. Katika kitenzi wakabidi, mwanafunzi alitumia kiambishi ngeli wa kilitumiwa kimakosa kwani nomino hali huchukua kiambishi ngeli i cha umoja na zi katika wingi. Kwa hivyo, mwanafunzi angeandika; Polisi walikuwa na kazi ngumu ya kuzima moto huo. Ikabidi kuwaita zimamoto.

76 Mifano mingine; 1(a) Basi siku hiyo alikuwa ni siku ya kwanza kuenda matembe. (b). Basi siku hiyo ilikuwa ni siku ya kwanza kuenda matembezi. 2.(a). Roho ilinipapa kana kwamba ulitaka kufunguliwa utoroke. (b). Roho ilinipapa kana kwamba ilitaka kufunguliwa itoroke. Katika sentensi 1 (a). Mwanafunzi alitumia kiambishi ngeli a cha umoja kuregelea nomino siku. Ikiwa nomino siku iko katika ngeli ya I ZI, mwanafunzi alipaswa kutumia kiambishi ngeli i kama ilivyoonyeshwa katika 1(b). Vivyo hivyo, katika sentensi 2 (a) Kiambishi ngeli u cha umoja kilitumika katika vitenzi ulitaka na utoroke. Kiambishi hiki (u) kiliregelea nomino roho. Kulingana na matumizi ya lugha sanifu, nomino roho huchukua kiambishi ngeli i cha umoja na kiambishi ngeli zi cha wingi. Kwa hivyo, 2(a) kisarufi iko makosa. Inastahili kusoma kama 2(b) hapo juu. (v) Makosa ya uchopekaji wa vaimbishi ngeli vingine badala ya viambishi ngeli vya ngeli ya KI-VI katika sentensi. Ngeli ya KI-VI ni ngeli inayohusu vitu mbalimbali visivyo na uhai. Kwa mfano; 1 (a) Kiti kimevunjika darani. (b) Viti vimevunjika darani. 2 (a) Kidole kimefura sana.

77 (b) Vidole vimefura sana. Katika data ya utafiti, ilibainika wazi kwamba kazi za wanafunzi huwa na makosa ya matumizi ya viambishi ngeli hususan katika ngeli ya KI-VI. Mtafiti alinukuu sentensi ifuatayo. Vilio vya huzuni zilihinikiza hewani. Katika sentensi hii, mofimu zi katika kitenzi zilihinikiza ilichopekwa kama kiwakilishi ngeli c ha nomino vilio. Vilio ni nomino ya ngeli ya KI-VI, ambayo kiwakilishi ngeli cha umoja ni ki ilhali cha wingi ni vi. Kwa hivyo, sentensi iliyopo juu inastahili kuwa; Vilio vya huzuni vilihinikiza hewani. Katika hali hii, upatanisho wa kisarufi umejitokeza waziwazi. (vi)makosa ya uchopekaji wa viambishi ngeli vingine badala ya viambishi ngeli vya ngeli ya U-I Nomino zinazopatikana katika ngeli hii ni nomino za vitu mbalimbali visivyokuwa na uhai. Mofimu ambazo hutumika katika upatanisho wa kisarufi katika ngeli ya U I ni mofimu u ya umoja na mofimu i ya wingi. Data ya utafiti ilibainisha kuwa na sentensi zilizokuwa na makosa ya kuchopekwa viambishi vya ngeli nyingine badala ya viambishi vya ngeli ya U I katika sentensi. Sentensi zilizobainishwa katika data ya utafiti zikiwa na makosa ya aina hii ni pamoja na ;

78 Mtihani ilikuwa rahisi. Nomino mtihani inaashiria hali ya umoja. Kitenzi ilikuwa kina mofimu i, inayoregelea nomino mtihani. Mofimu i inastahili kutumiwa kama kiwakilishi ngeli katika hali ya wingi lakini mwanafunzi mhusika alikitumia mofimu hii kuregelea nomino ya umoja. Hii ni wazi kuwa mofimu i katika kitenzi kisaidizi ilikuwa ilitumiwa kimakosa. Kisarufi, kiambishi ngeli sahihi katika kitenzi hiki kulingana na mazingira ya sentensi hi, kinasthili kuwa u Hatimaye, sentensi ingelisoma; Mtihani ulikuwa rahisi. (vii) Makosa ya uchopekaji wa viambishi ngeli vingine badala ya viambishi ngeli vya ngeli ya YA YA. Ngeli ya YA YA hutumika katika upatanisho wa kisarufi wa nomino za wingi ambazo huchukua kiambishi awali ya katika umoja wa wingi. Hii ni kumaanisha, nomino za ngeli ya YA YA hazina viambishi vya umoja wala wingi. Aidha, vitu asilia vinavyowakilishwa na nomino hizi huwa haviwezi kugawanyika katika hali ya umoja wala wingi.

79 Kwa mfano; UMOJA Maziwa yameharibika. Mate yake yamekauka. Marashi aliyokuwa akitumia yameisha. WINGI Maziwa yameharibika. Mate yake yamekauka. Marashi aliyokuwa akitumia yameisha. Jedwali la 16:Kielelezo cha nomino za ngeli za kiambishi ngeli kimoja katika Umoja na Wingi. Katika kazi za wanafunzi, mtafiti alibaini makosa ya uchopekaji wa viambishi ngeli katika sentensi zilizokuwa na nomino za wingi, Viambishi hivyo viliregelea nomino za wingi kimakosa. Pamoja na sentensi zilizobainishwa zikiwa na makosa haya ni:- Baba yangu alifurahi sana maana maisha yake itabadilika. Nomino maisha ni moja wapo ya nomino za wingi. Aidha, ni mofimu huru kwani haihitaji kuambishwa katika hali yoyote. Kulingana na maendelezo ya sentensi hii, kitenzi kinachohusu nomino maisha ni itabadilika. Uambishaji awali wa kitenzi hiki ulifanywa kimakosa, kwani kiambishi cha upatanisho wa kisarufi kilichotumiwa ni i. Kulingana na nomino inayoregelewa na kiambishi hiki, kiambishi sahihi kinastahili kuwa cha ngeli ya YA YA. Hivyo basi, sentensi inapaswa kusoma. Baba yangu alifurahi sana maana maisha yake yatabadilika. c) Makosa ya uchopekaji wa viambishi vya umoja na wingi katika sentensi. Viambishi vya umoja na wingi hupachikwa mwanzoni mwa nomino. Kuna nomino ambazo huhitaji viambishi vya wingi na nyingine hazihitaji kuambishwa kwa viambishi vya wingi

80 kwani huwa ni nomino zenye umbo moja la umoja na wingi. Aidha nomino zisizohitaji viambishi vya wingi takriban asilimia tisini na tisa (99%) huwa ni nomino za lugha za kigeni. Kwa mfano; Nomino zinazohitaji kuambishwa Mtoto wangu amepotea Watoto wangu wamepotea Mtiumeangukia nyumani ya babu Nomino zisizohitaji kuambishwa Sahani yangu imepotea Sahani zangu zimepotea Karatasiimepasuka Karatasi zimepasuka Mitiimeangukia nyumba za babu Jedwali 17 :Kielelezo cha Unominishaji kutumia viambishi vya wingi. Katika data ya utafiti, mtafiti alibaini sentensi zilizokuwa na makosa ya uchopekaji wa viambishi vya umoja na wingi. Baadhi ya sentensi hizi ni; Mfano (i) Kila mtu alienda nyumbani akiwa na raha kama mama aliyejaliwa kujifungua mapacha: Katika mfano (ii), nomino mapacha ina mofumu ma ya wingi iliyochopekwa kimakosa. Nomino pacha ikiwa nomino ya umbo moja la umoja na wingi, aidha nomino ya lugha ya kigeni, haihitaji kuambishwa ili iwe katika hali ya wingi. Kwa hivyo, mofimu ma katika nomino pacha inastahili kudondoshwa, kisha mwishoni, sentensi itakuwa sanifu kwani itasoma. Kila mtu alienda nyumbani akiwa na raha kama mama aliyejaliwa kujifungua pacha.

81 Mfano (ii) Si pete za dhahabu si vidani si mishanga na kadhalika. Nomino mishanga katika sentensi hii ilichopekwa mofimu mi ya wingi ndiposa ikaandikwa mishanga. Katika upatanisho wa kisarufi, nomino shanga iko katika ngeli ya U-ZI. Kwa sababu hii, katika hali ya umoja inastahili kuwa ushanga ilihali katika hali ya wingi hutokezea kama shanga. Kwa hivyo,sentensi hii ingeandikwa. Si pete za dhahabu si vidani si shanga na kadhalika (d) Makosa ya uchopekaji wa viambishi vya mnyambuliko wa vitenzi (kauli) katika kauli ya kutenda. Mnyambuliko wa vitenzi ni hali ya kurefusha vitenzi kutoka hali moja hadi hali nyingine kwa kutumia mofimu mwafaka za viambishi tamati. Mtafiti alibaini kwamba wanafunzi wanatatizo la kurefusha vitenzi kwani walitumia viambishi visivyokuwa sahihi katika unyambuaji wa vitenzi katika sentensi. Kulingana na data ya utafiti mtafiti aliainisha makosa haya kulingana na kauli ambazo wanafunzi wangetumia.vitenzi katika kauli ya kutenda huwa haviongezewi viambishi tamati vyovyote, badala yake huwa na kiishio a. Kwa mfano; Mama anapika chakula. ana pik a Mzizi kiishio

82 Kulingana na data ya utafiti, ilidhihirika kuwa wanafunzi huwa na tatizo la kunyambua vitenzi. Sentensi zifuatazo ni mifano iliyonukuliwa kutokana na insha za wanafunzi. (i). Tuliagizia chakula mara moja. (ii). Nilifikia mahali pengine palipokuwa na sherehe. (iii). Kwa shida na uchungu niliokuwa nao nilishtukia kumwona mwalimu kasimama tashti huku aliamrisha kutoa kitabu changu. Katika sentensi (i), (ii) na (iii) vitenzi vilivyokolezwa rangi vinaashiria kuwa na makosa ya mnyambuliko wa kauli ya kutenda. Vitenzi hivi vilinyambuliwa kwa kiambishi i cha kauli ya kutendea Sentensi hizi zinastahili kuwa, i. Tuliagiza chakula mara moja ii. iii. Nilifika mahali pengine palipokuwa na sherehe. Kwa shida na uchungu niliokuwa nao nilishtuka kumwona mwalimu kasimama tashti huku akiamrisha kutoa kitabu changu. Aidha wanafunzi walichopeka kiambishi li kimakosa katika vitenzi vilivyostahili kuwa katika kauli ya kutenda katika sentensi.kwa mfano: i) Ghulamu huyo alikuwa amevalia suti ya samawati yenye danzi zakuvutia ilimwingia na kumkaa bambamu. ii) Wazimamizi walishuka chini walikuwa wamekalia vizuri katika nafasi zao jukwaani.

83 Katika sentensi hizi, kitenzi amevalia na wamekalia vilinyambuliwa kwa kutumia kiambishi li cha kauli ya kutendea ilhali vitenzi hivi vinastahili kuwa katika kauli ya kutenda. Kwa hivyo, kulingana ana mazingira ya sentensi hizi, kitenzi amevalia na wamekalia vinastahili kudondoshwa mofimu li ndipo vichukue kauli sahihi ambayo ni kauli ya kutenda. Hatimaye sentensi hizi zitasoma; i. Ghulamu huyo alikuwa amevaa suti ya samawati yenye danzi za kuvutia ilimwingia na kumkaa bambamu. ii. Wasimamizi walishuka chini walikokuwa wamekaa vizuri katika nafasi zao jukwaani Makosa ya uchopekaji wa neno au maneno katika sentensi. Kuna aina mbalimbali za maneno katika lugha ya Kiswahili. Maneno haya hushirikiana katika uundaji wa sentensi kulingana na jukumu la neno husika katika sentensi inayoshughulikiwa hususan katika ujumbe unaotarajiwa kuwasilishwa. Mtafiti alibaini makosa ya uchopekaji wa maneno tofautitofauti katika sentensi zilizotumiwa na wanafunzi kuandika insha za lugha ya Kiswahili. Mtafiti aliainisha makosa haya kwa kuzingatia aina za maneno na majukumu yake katika sentensi husika. Makosa yaliyobainishwa yaliainishwa kama ifuatavyo:- (a)makosa ya uchopekaji wa nomino. (b)makosa ya uchopekaji wa wakati. (c)makosa ya uchopekaji wa vielezi.

84 (d)makosa ya uchopekaji wa vivumishi. (e)makosa ya uchopekaji wa kiunganishi. (a) Makosa ya uchopekaji wa nomino. Data ya utafiti ilibainisha kwamba wanafunzi walitumia nomino ambazo hazistahili kutumiwa kulingana na mazingira ya sentensi husika. Pamoja na senetnsi hizi ni; Mfano (i) Tuliwapigia rununu na baada ya masaa machache tuliona gari la wazima moto. Nomino rununu ni nomino inayomaanisha kifaa kidogo cha mkononi kinachotumiwa katika mawasiliano. Rununu hurusha na kupokea mawimbi ya sauti. Katika mazingira ya sentensi iliyotolewa mfano hapo juu, nomino rununu ilitumiwa kimakosa.kurekebisha kosa hili, nomino simu inastahili kutumiwa badala ya rununu. Nayo sentensi ingekuwa. Tuliwapigia simu na baada ya msaa machache tuliona gari la wazimamoto. Mfano (ii); Ilikuwa siku ya ijumaa na jioni tulipokuwa na pirikapirika za kutayarisha chakula cha jio. Nomino iliyochopekwa kimakosa katika sentensi hii ni chakula. Nomino chakula ilitangulia chajio.kulingana na lugha ya Kiswahili, nomino hizi haziwezi ktumika mahali pamoja katika sentensi. Kwa hivyo mwanafunzi angetumia nomino chajio na kuacha nomino chakula. Hivyo angeandika; Ilikuwa siku ya ijumaa na jioni tulipokuwa na pirikapirika za kutayarisha chajio.

85 (b)makosa ya uchopekaji wa wakati. Lugha ya Kiswahili ina maneno yanayorejelea wakati fulani katika usemi au ujumbe. Baadhi ya maneno haya ni, asubuhi, sasa, leo na kesho. Matumizi ya maneno haya hutegemea usemi ambamo sentensi imo, kwani kuna usemi wa taarifa na usemi halisi. Usemi halisi ukiwa usemi wa mtu mwenyewe anayetoa ujumbe ilhali usemi wa taarifa ni ripoti kuhusu yaliyosemwa na mtu mwingine. Kuna sheria katika lugha ya Kiswahili zinazoambatana na usemi wa taarifa.pamoja na sheria hizi ni. Usemi Halisi Wakati huu Kwangu Sasa Leo Kesho Usemi wa taarifa Wakati huo Kwake Wakati huo Siku hiyo Siku itakayofuata Jedwali 18: Kielelezo cha nyakati katika usemi halisi na usemi wa taarifa. Kutokana na data ya utafiti, kuna sentensi zilizochopekwa baadhi ya nyakati hizi kimakosa Mfano (i); Alikuwa akishabikia ulinzi boys na mimi starehe club na ndizo zilikuwa zinakutana leo Kulingana na maendelezo ya sentensi hii, usemi uliotumiwa ni usemi wa taarifa kwani ni wazi kwamba mnenaji anatoa ripoti fulani. Baadhi ya kanuni zilizoorodheshwa katika jedwali hapo juu neno leo linastahili kubadilika na kuwa siku hiyo iwapo ni ripoti inatolewa.kwa hivyo sentensi mfano (i) ingekuwa;

86 Alikuwa akishabikia ulinzi boys na mimi starehe club na ndizo zilizokuwa zinakutana siku hiyo. (c) Makosa ya uchopekaji wa vielezi katika sentensi. Waihiga 2003 anasema, vielezi ni maneno yanayotumika kufafanua vitenzi, vivumishi au vielezi vingine. Kulingana na dhana hii, vielezi vina jukumu la kueleza jinsi kitenzi, kivumishi au kielezi kinavyofanyika.katika lugha ya Kiswahili, kuna vielezi ambavyo huundwa kwa kurudiarudia neno moja mara mbili. Baadhi ya vielezi hivi huandikwa kwa kuchanganya maneno haya mawili. Vielezi vingine huandikwa kama maneno mawili yaliyotenganishwa na nafasi ndogo. Kwa mfano: a) Kaka aliandika harakaharaka. b) Kobe hutembea polepole. Data ya utafiti ilidhihirisha makosa ya uchopekaji wa vielezi katika sentensi. Miongoni mwa sentensi zilizobainishwa zikiwa na makosa haya ni, (i) Mimi pamoja na mke wangu tulifuatana unyo kwa unyo hadi garini. Sehemu ya sentensi iliyokolezwa wino, ina maneno mawili unyo na unyo yaliyotenganishwa na kielezi kwa kimakosa. Neno unyo linastahili kurudiwa mara mbili ili kuunda kielezi unyounyo.hivyo kwa halistahili kuwa katikati ya kielezi hiki. Licha ya kutokuwa katikati mwa kielezi unyounyo,

87 halistahili kuwepo kabisa katika sentensi. Kwa hivyo linastahili kudondoshwa na sentensi iwe; Mimi pamoja na mke wangu tulifuatana unyounyo hadi garini. (ii) Mara ghafla tukaona jua la aga miti na giza la ingia. Lugha ya Kiswahili ina vielezi ambavyo hutumiwa katika hali ya mfululizo katika sentensi Kwa mfano; Data aliingia nyumbani haraka sana. N T E E E Vielezi ambavyo hufuatana katika sentensi huwa na jukumu tofautitofauti. Vielezi vinavyofuatana mfululizo kielezi kilichokitangulia. Katika mfano uliopo hapo juu, kielezi nyumbani kimefafanua kitenzi ingia,haraka kikafafanua nyumbani, na sana kikafafanua haraka. Katika mfano (ii), mara na ghafla ni vielezi vilivyofuatana mfululizo. Vielezi hivi vinabeba dhana sawa (bila ya kutarajia). Kwa hivyo, kisarufi, kielezi mara na ghafla havistahili kuandikwa mahali pamoja katika sentensi. Ili kurekebisha kosa hili, kielezi kimoja kinastahili kudondoshwa. Kinaweza kuwa kielezi mara au ghafla ilimradi kimoja kitumike. ( d) Makosa ya uchopekeji wa vivumishi Vivumishi ni maneno yanayotoa habari kuhusu nomino au kiwakilishi chake. Jukumu la kivumishi ni kufafanua au kuvumisha nomino (Waihiga 2003)

88 Data ya utafiti ilikuwa na sentensi ambazo zilikuwa na vivumishi vilivyotumiwa kimakosa. Makosa ya uchopekaji wa vivumishi yaliainishwa katika makundi yafuatayo; i) Makosa ya uchopekaji wa vivumishi vya pekee. ii) Makosa ya uchopekaji wa vivumishi vimilikishi. iii) Makosa ya uchopekaji wa vivumishi virejeshi. iv). Makosa ya uchopekaji wa vivumishi vionyeshi. i) Makosa ya uchopekaji wa vivumishi vya pekee. Naam amakweli chambilecho wahenga na wahenguzi hawakutupaka mafuta kwenye mgongo wa chupa waliponena chanda chema huvishwa pete. Neno kwenye ni kivumishi cha pekee.kulingana na matumizi ya kivumishi kwenye. Kisarufi, nafasi ambayo imechopekwa kivumishi kwenye katika sentensi inastahili kuchopekwa kielezi kwa, ili kwamba sentensi isiwe na utata. Katika hali hii, sentensi hii ingekuwa; Naam amakweli chambilecho wahenga na wahenguzi hawakutupaka mafuta kwa mgongowa chupa waliponena chanda chema huvishwa pete. ii) Makosa ya uchopekaji wa vivumishi vimilikishi. i. Nilijizoazoa kutoka kwa sofa yangu na kufunga mlango. Kulingana na maendelezo ya sentensi hii, yangu ni kivumishi kinachofafanua nomino sofa kama inamilikiwa na nani. Katika upatanisho wa kisarufi. kivumishi kimilikishi mwafaka cha nomino sofa ni langu bali sio yangu kwa hivyo mwanafunzi mhusika alipaswa kuandika sentensi hii kama ifuatavyo;

89 Nilijizoazoa kutoka kwa sofa langu na kufunga mlango. Katika data ya utafiti, mtafiti aligundua kuwa wanafunzi walitumia vivumishi virejeshi ambavyo si sahihi kulingana na nomino zilizorejelewa. Vivumishi virejeshi huzingatia upatanisho wa kisarufi katika sentensi husika. Mtafiti alithibithisha makosa haya kwa kutumia mifano ya sentensi zilizotumiwa na wanafunzi katika uandikaji wa insha. iii) Makosa ya uchopekaji wa vivumishi virejeshi. Nilitoka ndani ya gari hiyo mimi pamoja na shangazi yangu. Katika sentensi hii, kivumishi kirejeshi kilichotumiwa kurejelea nomino gari ni hiyo Nomino gari ni ya ngeli ya LI-YA katika upatanisho wa kisarufi. Kulingana na mazingira ya sentensi hii, kivumishi kirejeshi cha nomino gari ambacho mwanafunzi angetumia katika upatanisho wa kisarufi ni hilo badala ya hiyo. iv). Makosa ya uchopekaji wa vivumishi vionyeshi Vilevile, mtafiti aligundua kwamba, wanafunzi walitumia vivumishi vionyeshi badala ya vivumishi virejeshi katika sentensi. Kwa mfano; Katika mti ule chini kulikuwa na bwawa la maji. Sentensi iliwasilishwa katika usemi wa taarifa ambao umefanya sentensi hii iwe katika wakati uliopita.neno lililokolezwa wino ni kivumishi kionyeshi. Jukumu la vivumishi vionyeshi ni kuonyesha kwa kuashiria mahali au upande kitu kilipo. Vitu huwa karibu au mbali. Hivyo, vivumishi vionyeshi vinavyoonyesha vitu vya karibu hujengwa na mzizi li

90 ilhali vya mbali hujengwa na mzizi le katika mazingira ya sentensi iliyotolewa hapo juu, kionyeshi ule kinaashiria mti ambao uko mbali. Umbali wa mti huu unathibitishwa na sentesni kuwa katika usemi wa taarifa. Kwa sababu ya umbali wa mti kivumishi kionyeshi mwafaka ambacho mwanafunzi angetumia ni huo badala ya ule. Mfano (ii); Siku ile tulifunzwa kuhusiana na msamiati mazingira ya sentensi hii ni ya usemi wa taarifa. Hivyo, siku inayozungumziwa ilipita. Kisarufi hali hii inalazimu kivumishi kionyeshi ile kiwe cha mbali. Kwa hivyo, mwanafunzi angetumia kivumishi kionyeshi hiyo badala ya ile Mfano (iii); Nilihisi maumivu kwenye mguu wangu wa kushoto na nilipo-angalia niliona kichwa kile kikining atu bila ya huruma. Kivumishi kionyeshi kilichotumiwa katika sentensi hii ni kile Mzungumzaji wa usemi huu anatoa ripoti ya jinsi mambo yalivyokuwa. Kisarufi, kivumishi kionyeshi mwafaka katika sentensi hii kingekuwa hicho. (e) Makosa ya uchopekaji wa kiunganishi. Kulingana na Nadharia ya Uchanganuzi Linganuzi (N.U.L), Lado (1957),anasema kwamba,n.u.l huchukulia kuwa wazungumzaji wa lugha hujaribu kuhamisha muundo wa lugha ya kwanza kwa lugha ya pili ili kurahisisha ujifunzaji wa lugha. Kwa hivyo nadharia ya Lado (1957), hushunghulikia jinsi LI inavyomwathiri mwanfunzi wa L2. Katika data ya

91 utafiti,mtafiti alibaini sentensi katika insha za wanafunzi zilizokumbwa na athari za lugha ya kwanza.kwa mfano, Ilikuwa siku ya ijumamosi na jioni tulipokuwa na pirikapirika za kutayarisha chakula cha jio. Sentensi hii imechopekwa kiunganishi na kilichokolezwa wino. Kiunganishi hiki kimesababisha lugha katika sentensi hii iathirike,kwani sentensi hii imehamishwa kutoka lugha ya kwanza, Kigiriama. (a) Ilikuwa siku ya ijumamosi na jioni tulipokuwa na pirikapirika za kutayarisha chakula cha jio.(sentensi yenye makosa) (b)yakala siku ya jumamosi na dziloni furihokala na mkirikiro wa kuthayarisha chakurya cha dziloni. (Sentensi ya (a) katika lugha ya Kigiriama) (c ) Ilikuwa siku ya ijumamosi jioni tulipokuwa na pirikapirika za kutayarisha chakula cha jio.(sentensi ya (a) baada ya marekebisho) Kulingana na data ya utafiti, kuna sentensi zilizobainika kuwa na mchanganyiko wa makosa. Sentensi zifuatazo zilibainishwa kuwa na aina za makosa ya uchopekaji zaidi ya moja. Mfano (i); Nazo tiba za mahospitali ziligoma kwa misanga hiyo.

92 Aina za makosa ya uchopekaji katika sentensi hii ni kama yafuatayo; a) Makosa ya uchopekaji wa kivumishi kirejeshi. Kulingana na jukumu la vivumishi virejeshi, (Kurejelea nomino au kiwakilishi) vinastahili kuchukua nafasi baada ya nomino inayorejelewa au mwishoni mwa kikundi nomino. Kwa sababu hii, katika mfano uliotolewa hapo juu, kivumishi kirejeshi nazo kingechukua nafasi baada ya kikundi-nomino tiba za mahospitali b) Makosa ya uchopekaji wa mofimu za wingi. Makosa haya yalifanyika katika nomino hospitali na kisanga. Hospitali ni nomino kutoka lugha ya kigeni (Kiingereza) ambayo haihitaji kuambishwa katika hali yoyote. Mwanafunzi mhusika alichopeka mofimu ma ya wingi katika nomino hii na akaunda nomino mahospitali ambayo ni kosa la kisarufi. Hivyo nomino hospitali inastahili kubaki hospitali iwapo katika umoja au wingi. Vilevile, nomino misanga ilichopekwa mofimu mi ya wingi kimakosa.nomino hii inatokana na nomino kisanga katika umoja. Kisanga ikiwa ni nomino ya ngeli ya KI- VI, inastahili kudondoshwa kiambishi ki cha umoja kisha ipachikwe kiambishi vi cha wingi. Mwanafunzi alipachika kiambishi mi cha wingi ambacho si mwafaka. c) Kosa la uchopekaji wa kivumishi kirejeshi. Baada ya mwanafunzi kuchopeka mofimu mi ya wingi na kuunda nomino misanga alilazimika kutumia kivumishi kirejeshi hiyo cha upatanisho wa kisarufi ambayo kulingana na nomino misanga ni makosa. Kisarufi, nomino misanga ingekuwa

93 visanga nayo ingechukua kivumishi kirejeshi hivyo ambacho ndicho kirejeshi mwafaka. d) Kosa la mfuatano wa vipashio. Hatimaye sentensi hii Nazo tiba za mahospitali ziligoma kwa misanga hiyo ambayo inampangilio wa; Nazo tiba za mahospitali ziligoma kwa misanga hiyo. V N H N T E N V ingechukua mpangilio wa vipashio kama ifuatavyo. Tiba za mahospitali nazo ziligoma kwa misanga hiyo. N H N V T E N V Makosa ya Hijai/Tahajia. Makosa haya ni makosa yanayotokana na maendelezo mabaya ya maneno katika sentensi za lugha ya Kiswahili. Miongoni mwa makosa haya ni: (i) Kutenganisha neno moja kuonekana kama maneno mawili. Kwa mfano: a) Aliye-fika badala ya aliyefika. b) Utakapo weza badala ya utakapoweza. (ii) Kuunganisha maneno mawili au zaidi kuwa neno moja

94 Kwa mfano; (a)kwasababu badala ya kwa sababu. (b)amakweli badala ya ama kweli. (iii) Kukata silabi vibaya Kwa mfano: a) Chak-ula badala ya chaku-la. b) Sim-ama badala ya simama. (iv)kuongeza herufi isiyofaa katika neno. Kwa mfano: a) Piya badala ya Pia. b) Mutu badala ya mtu.. (iv) Matumizi mabaya ya alama za uakifishaj Ama kutoweka alama za uakifishaji katika nafasi zinazohitajika. Kwa mfano: a) N gombe badala ya Ng ombe. b) Nguo yako ina ngara sana; badala ya, Nguo yako inang ara sana. Makosa ya hijai yaliyoshughulikiwa ni ya kimofosintaksia pekee.makosa haya yaliainishwa katika makundi makuu mawili; (1) Makosa ya kutenganisha neno katika sentensi. (2) Makosa ya kuunganisha maneno mawili au zaidi kuwa neno moja.

95 (1) Makosa ya kutenganisha neno katika sentensi. Mtafiti aliainisha makosa haya kulingana na aina ya neno lililotenganishwa. Hatimaye akaibuka na makundi ya makosa haya kama ifuatavyo: (a) Makosa ya kutenganisha nomino katika sentensi. (b) Makosa ya kutenganisha viambishi katika vitenzi. (c) Makosa ya kutenganisha vielezi katika sentensi. (a). Makosa ya kutenganisha nomino katika sentensi. Nomino ni majina ya viumbe au vitu, ambayo hayawezi kutenganishwa na kuwa maneno mawili au zaidi. Mtafiti alitambua kuwa wanafunzi hufanya makosa ya kutenganisha nomino katika uundaji wa baadhi ya sentensi. Mtafiti alitambulisha makosa haya kwa kuweka kistari katika nafasi iliyotenga nomino husika. Kwa mfano: (i)bibi-harusi na bwana-harusi walifurahi sana. (ii)nilivaa king ale change kilichong aa na kumetameta mithili ya mbala-mwezi. (iii) Yote hayo yaliendelea hadi jua lilipokuwa likiaga miti tulibidi tuite wazima-moto. (iv)siku hiyo ya Juma-mosi tulifua nguo zetu na kupaki. (v)klabu ya wana-chui walitunyeshea na bao la kwanza mtungi. (vi)nilikuwa na wasi-wasi kidogo lakini nilipiga moyo konde na kwenda uwanjani.

96 (vii) Nilijitia hamu-nazo kucheza ngoma nitakazo. (ix)nao wakamchukua mpaka kwenye gari lao na kumpeleka za-hanati. (x)jambo hilo lilinifanya nifurahi ja kibogoyo aliyejaliwa kupata magego katika shamra-shamra za nyama choma. Katika mifano iliyotolewa hapo juu, kutoka sentensi ya kwanza hadi ya nane (1-8) nomino zilizotenganishwa zimeundwa kwa mofu changamano, ambapo kila mofu ina mofimu zake. Mofu changamano huundwa kwa mizizi miwili au zaidi. Aidha, mofu hizi zinaweza kutenganishwa na zikawa mofu huru katika mazingira mengine bali sio katika mazingira ya sentensi ambamo zilitumika katika utafiti huu. Kutenganishwa kwa nomino hizi kumesababisha makosa ya maendelezo ya sentensi. (b). Makosa ya kutenganisha viambishi katika vitenzi. Kitenzi ni neno linalotoa taarifa kuhusu tendo lililofanyika, litakalofanyika au linalofanywa na nomino au kiwakilishi.vitenzi ni viungo muhimu sana katika sentensi, hivyo sentensi yoyote lazima iwe na kitenzi ndipo iweze kueleweka. Hata hivyo, vitenzi vinaweza kuambishwa na vikajisimamia kama sentensi kamili. Uambishaji wa sentensi hufanywa mwanzoni au mwishoni mwa mizizi ya vitenzi husika. Iwapo vitenzi vya kuambishwa haviwezi kujisimamia kama sentensi basi mofimu nyingine huhusishwa katika uundaji wa sentensi hizo kulingana na kanuni au sheria za lugha hiyo.kwa hivyo, viambishi pekee haviwezi kujisimamia na kutoa maana yoyote bila mizizi ya vitenzi. Utafiti huu ulithibitisha kwamba, wanafunzi hufanya makosa ya kutenganisha viambishi katika vitenzi vilivyoambishwa. Mifano ya makosa haya imeonyeshwa katika sentensi zifuatazo zilizonukuliwa katika kazi za wanafunzi.

97 (i)tulienda kwenye msitu mkubwa uliokuwa na miti yenye matunda na kuni zilizo kaukakaukau. (ii) Nilipofika nyumbani siku jua nianzie wapi wala nimalizie wapi. Katika sentensi ya (i) zilizo ni viambishi awali vilivyowekwa mwanzoni mwa mzizi kauka ili kutoa maana iliyodhamiriwa. Hivyo,kitenzi hiki kinastahili kuandikwa zilizokauka badala ya zilizo kauka. Sentensi ya (ii) ina neno siku jua lililoandikwa kama maneno mawili ambayo ni siku na jua. Haya ni maneno mawili katika mazingira ya sentensi hii. Jinsi yalivyoandikwa na mwanafunzi, maana iliyokusudiwa imepotoka, kwani yamejitokeza kama mofimu huru. Ili kutoa ujumbe uliodhamiriwa, maneno haya yanastahili kuandikwa kama neno moja sikujua ikiwa siku ni viambishi awali. Kiambishi si kinasimamia kikanushi ilhali kiambishi ku ni cha wakati uliopita. Mifano iliyotolewa na mtafiti, inadhihirisha wazi kuwa viambishi haviwezi kujisimamia katika sentensi yoyote, kwa sababu viambishi hivi huwa ni mofimu tegemezi, nazo huhitaji mizizi ya vitenzi. ( c ) Makosa ya kutenganisha vielezi katika sentensi. Lugha ya Kiswahili ina vielezi mbalimbali. Vielezi vina majukumu ya kueleza zaidi juu ya vitenzi, vivumishi na vielezi vingine. Kati ya aina za vielezi kuna baadhi ambavyo huambishwa na vingine havihitaji viambishi kwa sababu ni vielezi vilivyoundwa na mizizi pekee (mofimu huru). Vilevile, vielezi vingine hujirudiarudia. Kwa hivyo, vielezi

98 vinapotokezea kitakriri, haimaanishi kuwa mofimu hizi zitenganishwe bali hubaki kuwa kielezi kimoja. Miongoni mwa saentensi zilizokuwa na makosa haya katika kazi za wanafunzi ni; 1. a)dereva alisimamisha gari na tukatoka pole pole b)dereva alisimamisha gari na tukatoka polepole. Katika sentensi ya 1(a) kielezi pole pole kiliandikwa kimakosa, kwa hivyo, (b) ndiyo yenye kielezi kilichoandikwa kwa usahihi yaani, polepole. 2. a) Kwa sababu nilikuwa nikipenda kucheza disko nilisakata ngoma bara bara. b) Kwa sababu nilikuwa nikipenda kucheza disko nilisakata ngoma barabara. 3.a) Mama alipika chakula haraka haraka. b)mama alipika chakula harakaharaka. (2) Makosa ya kuunganisha maneno katika sentensi. Lugha ya Kiswahili ina mofimu mbalimbali ambazo huunganishwa kwa kuunda sentensi hususan maneno ya Kiswahili. Maneno haya huwa ya aina mbalimbali, kwa hivyo, kila neno lazima lijisimamie katika sentensi kulingana na uhitaji. Kwa sababu hii, uunganishaji wa maneno husababisha maendelezo mabaya ya sentensi za lugha ya Kiswahili. Mtafiti aliainisha makosa haya kulingana na aina za maneno yaliyounganishwa, naye akapata makundi yafuatayo: (a) Makosa ya kuunganisha kiunganishi na nomino katika sentensi. (b) Makosa ya kuunganisha kitenzi na nomino katika sentensi.

99 ( c) Makosa ya kuunganisha kiunganishi na kitenzi katika sentensi. (d) Makosa ya kuunganisha kihusishi na nomino. (e) Makosa ya kuunganisha kitenzi na kielezi. (f) Makosa ya kuunganisha kielezi na kiwakilishi. (g) Makosa ya kuunganisha kiunganishi na kiwakilishi. (a). Makosa ya kuunganisha kiunganishi na nomino katika sentensi. Baadhi ya sentensi zilizotambulishwa kuwa na makosa ya uunganishaji wa maneno zilitolewa mifano kama ifuatavyo; (i) Amakweli njia mbili zilimshinda fisi na akapasuka msamba. Ama ni kiunganishi na Kweli ni nomino dhahania. (ii)nilikuwa nafuraha kama mwanamke aliyejaliwa na pacha mbili. Na ni kiunganishi na Furaha ni nomino dhahania. (iii) Mtima wangu ulinidunda du!du!du! jamdundo wa rege nchini Jamaika. Ja ni kiunganishi na Mdundo ni nomino dhahania. Maneno yaliyoandikwa katika mlazo katika mifano iliyotolewa hapo juu, hayastahili kuunganishwa kwa hali yoyote iwayo

100 (b)makosa ya kuunganisha kitenzi na nomino katika sentensi. Miongoni mwa sentensi zilizobainika katika insha za wanafunzi zikiwa na makosa ya uunganishaji wa vitenzi na nomino ni; i) Tulipoendelea kusonga mbele, tulimuona chatu aliyekuwa ananjaa sana. Ananjaa ni maneno mawili yaliyounganishwa kimakosa. Ana ni kitenzi kisaidizi na njaa ni nomino dhahania. ii)nilipowasili, nilifikashule, nikaona kila mmoja anauso wa tabasamu. Sentensi hii ina maneno mawili yaliyoandikwa kwa kuunganisha maneno mawili tofauti. Maneno haya hayastahili kuunganishwa katika hali yoyote ile. Nilifikashule lina kitenzi nilifika na shule ikiwa nomino. anauso lina kitenzi kisaidizi ana na nomino uso. ( c) Makosa ya kuunganisha kiunganishi na kitenzi katika sentensi. Kiunganishi ni neno linalotumika kuunganisha sehemu mbili za sentensi au zaidi. Kwa hivyo, kiunganishi hakistahili kuandikwa pamoja na kitenzi kama neno moja. Kwa mfano: i) Tulitembea katika msitu ilitufike kwa nyanya yangu. Katika sentensi hii maneno mawili yaliandikwa kama neno moja ni kiunganishi ili na kitenzi halisi fika kilichoambishwa kwa mofimu tu mwanzoni na e mwishoni mwa mzizi fik.maneno haya yanastahili kuandikwa kama, ili tufike.

101 ii)nilimbeba mgongoni nanikapanda mtini. Neno nanikapanda liliandikwa kama neno moja lakini ni mchanganyiko wa maneno mawili. Maneno haya yakiwa ni na, kiunganishi na nikapanda ni kitenzi. Katika mazingira ya sentensi hii nikapanda ni kitenzi halisi kilichoundwa mwanzoni mwa mzizi pand kwa viambishi nika na kiishio a. (d) Makosa ya kuunganisha kihusishi na nomino. Kihusishi na nomino ni maneno ambayo hujisimamia yenyewe kiukamilifu katika sentensi. Aidha maneno haya hayawezi kuunganishwa ili kuunda neno moja. Data ya utafiti ilithibiti makosa haya yakifanywa na wanafunzi katika tungo zao za lugha ya Kiswahili. Sentensi zifuatazo ni mifano kutokana na kazi za wanafunzi: Mfano (i); Alianza kuishi maisha ya mateso na yaumaskini. Neno lililoandikwa kwa mlazo katika sentensi iliyotolewa mfano hapo juu, liliundwa kwa kuunganisha maneno mawili. Maneno haya yakiwa ni ya na umaskini. Ya likiwa ni kiunganishi na umaskini ni nomino dhahania, hayastahili kuunganishwa. Kwa hivyo sentensi inastahili kuwa ; Alianza kuishi maisha ya mateso na ya umaskini.

102 Mfano (ii); Tulitembea tulipofika njiani tuliona wanyama wakutisha. Kulingana na maendelezo ya sentensi ya mfano (ii), wakutisha ni kipashio kilichoundwa kwa kutumia kihusishi wa na nomino kutisha. Kutisha ni nomino ya kitenzi-jina kwani kitenzi tisha kilinominishwa kwa kuchopekwa mofimu ku mwanzoni mwa mzizi,tish.kurekebisha sentensi hii,maneno haya yanastahili kutenganishwa. Nayo sentensi ingesoma; Tulitebea tilipofika njiani tuliona wanyama wa kutisha. (e)makosa ya kuunganisha kitenzi na kielezi katika sentensi. Kitenzi na kielezi ni vipashio tofauti katika sentensi ambavyo havistahili kuandikwa pamoja kama neno moja. Data ya utafiti ilithibitisha kuwako kwa makosa ya kuunganisha vitenzi na vielezi katika sentensi. Ifuatayo ni mifano ya sentensi zilizobainishwa kuwa na makosa haya; (i)tukashukuru Mungu tulipofikasalama. Katika sentensi hii,neno tulipofikasalama ni mchanganyiko wa maneno mawili yakiwa kitenzi kielezi. Tulipoka ni kitenzi ilhali salama ni kielezi cha namna kwani kinafafanua zaidi kitenzi tulipofika. Sentensi hii ilistahili kusoma; Tukashukuru mungu tulipofika salama.

103 (f) Makosa ya kuunganisha kielezi na kiwakilishi Katika data ya utafiti, sentensi ifuatayo lilbainisha kuwa na makosa ya kuunganishwa kwa kielezi na kiwakilishi. Tulishauriwa kuwa tusichunge mifugo wenye misitu mikubwa mikubwa tukiwa pekeyetu. Neno pekeyetu ni mchanganyiko wa peke kikiwa kielezi cha namna ilhali yetu ni kiwakilishi kimilikishi cha nafsi ya kwanza wingi. Uunganishaji wa maneno haya umesababisha maendelezo mabaya ya sentensi. (g) Makosa ya kuunganisha kiunganishi na kiwakilishi katika sentensi. Viunganishi na viwakilishi vikiwa miongoni mwa vipashio vya sentensi,kila mojawapo ina majukumu tofauti katika sentensi husika. Kwa sababu hii, vipashio hivi viwili haviwezi kuunganishwa na kuwa neno moja. Vinapounganishwa,husababisha makosa ya kisarufi ya hijai Miongoni mwa sentensi zilizobainishwa katika data ya utafiti kuwa na makosa ya aina hii ni; Tulienda mpaka siteji tulipofika hapo shangazi yangu alikuwa amemtuma mtoto wakeakamwambia mtoto huyo kuwa kuna kuja wageni kwahivyo nenda ukawangoje huko siteji. Katika sentensi hii, kwahivyo liliandikwa kama neno moja kimakosa kwani kisarufi yanapaswa kuwa maneno mawili. Maneno haya yakiwa ni;

104 kwa likiwa kiunganishi na hivyo likiwa kiwakilshi kirejeshi,likirejelea kuja kwa wageni Makosa ya Mfuatano wa Vipashio katika sentensi. Vipashio ni sauti katika lugha lengwa. Sauti hizi zinaweza kuwekwa pamoja kulingana na uhusiano na majukumu. Hatimaye, zikatumiwa mahali pake kulingana na mktadha ili kuunda sentensi au tungo za lugha husika. Kuna aina mbalimbali za vipashio katika uundaji wa sentensi.vipashio vya sentensi ni fonimu, mofimu na neno. Kulingana na upeo wa utafiti,vipashio vilivyoshughulikiwa katika sehemu hii ni maneno ambayo huundwa kutokana na mofimu. Lugha ya Kiswahili ina kategoria nane za maneno. Nazo ni nomino, vitenzi, vivumishi, viwakilishi, vielezi, viunganishi, vihusishi na vihisishi. Nomino ni jina la mtu, kitu au mahali. Katika sentensi, nomino huelezewa zaidi na kivumishi au kitenzi katika sentensi. Kwa mfano; Mama anafua nguo zake. N T N V Kiwakilishi ni neno linalosimamia majukumu ya nomino katika sentensi bila kutaja nomino yenyewe. Aidha, huchukua majukumu ya nomino husika katika sentensi Mimi ninafua nguo zangu. W T N V

105 Kielezi hutanguliwa na kitenzi au kivumishi kwa kuwa hufafanua zaidi juu ya kitenzi au kivumishi Mimi ninafua nguo zangu zote. W T N V E Kulingana na majukumu ya kila kipashio katika sentensi za lugha ya Kiswahili huwa na ruwaza maalum kulingana na mfuatano wa maneno. Kwa mfano; Kadzo anakula embe. Kiima Kiarifu Shamirisho Sentensi hii inaweza kuandikwa katika ruwaza tofautitofauti.la muhimu nikutambua ruwaza iliyosahihi kulingana na mfuatano uliosahihi kisarufi. Mfuatano sahihi wa vipashio katika sentensi ni; Kiima Kiarifu Shamirisho Sentensi iliyopo hapo juu inaweza kutoa ruwaza zifuatazo; 1. Kadzo anakula embe. 2. Kadzo embe anakula. 3. Embe anakula Kadzo. 4. EmbeKadzo anakula.

106 5. Anakula embe Kadzo. 6. Anakula Kadzo embe. Kulingana na sheria za lugha katika mfuatano wa vipashio katika sentensi, sentensi ambayo ina ruwaza sahihi wa vipashio ni sentensi (1). Zaidi,kila kipashio kimechukua nafasi yake na kinatekeleza majukumu yake katika nafasi hiyo.sentensi ya aina hii, yaani sentensi ya kitenzi kimoja hurejelewa kama sentensi sahili. Hata hivyo, sentensi za aina nyingine kama sentensi ambatano na sentensi changamano,vipashio huwa na mfuatano kulingana na majukumu katika nafasi vitakavyochukua katika sentensi Sentensi kamili huwa na sehemu mbili kuu. Sehemu hizi ni Kikundi Nomino (KN) na Kikundi- Tenzi (KT). Kikundi-nomino (KN) ni sehemu ya sentensi inayotokezea upande wa kushoto wa sentensi, nayo hubeba nomino ambayo ni Kiarifu. Kikundi Tenzi (KT) hutoka upande wa kulia wa sentensi, nayo hubeba kitenzi ambacho ni kiarifu, kisha hufuatwa na kitendwa au kitendewa ambacho ni shamirisho katika sentensi. Kwa mfano: Mama anapika chakula KN KT Katika mazingira ya sentensi yoyote, uhusiano wa vipashio huthibitishwa na mpangilio wa vipashio husika katika sentensi hiyo.mtafiti alibaini kwamba wanafunzi hutumia vipashio vya sentensi bila ya kuzingatia utendakazi wake katika sentensi hiyo.

107 Kwa mfano; i) Katika mti ule chini kulikuwa na bwawa la maji. Mbali na makosa ya mpangilio wa vipashio, sentensi (i) hapo juu, ina makosa ya uchopekaji wa kiunganishi katika. Ndani ya mti hakuwezi kuwa na bwawa la maji. Kwa hivyo, neno katika, linastahili kudondoshwa. Kosa lengine ni uchopekaji wa kivumishi kionyeshi ule. Ikiwa sentensi iko katika wakati uliopita na katika usemi wa taarifa, kivumishi kionyeshi ule kinastahili kuwa huo Neno chini linatakikana kuwa nomino ambayo inahusiana na nomino mti. Hali hii inabashiri kuweko na kosa la udondoshaji wa kihusishi ya. Kwa hivyo, sentensi hii inastahili kuwa; Chini ya mti huo kulikuwa na bwawa la maji Mfano (ii); Kila mmoja alinyamaza ji tukabaki sote midomo wazi. Katika sentensi hii neno sote linawakilisha watu wote waliohusika katika matukio yanayoelezwa. Hivyo, sote ni kiwakilishi cha pekee. Kwa sababu hii, kiwakilishi sote kinapaswa kutangulia kitenzi tukabaki katika mazingira ya sentensi yenyewe. Kwa hivyo, sentensi hii inapaswa kuwa: Kila mmoja alinyamaza ji na sote tukabaki midomo wazi. Kuna makosa ambayo hutokea kwa sababu ya kosa lililotokea awali. Makosa haya hayatokani na kundi maalum katika makundi ya makosa yaliyoelezwa awali, bali ni

108 makosa ya mchanganyiko wa aina ya makosa yaliyotambulishwa. Katika utafiti huu makosa haya yamerejelewa kama Makosa Egemezi. Miongoni mwa sentensi zilizobainishwa kuwa na makosa egemezi katika insha za wanafunzi ni; (i) Madakika yalienda yakawa masaa. Dakika ni nomino yenye umbo moja katika umoja na wingi. Katika upatanisho wa kisarufi nomino ya umbo moja katika ngeli ya I-ZI huchukua viambishi awali i katika umoja na zi cha wingi. Nomino dakika katika sentensi hii,imechukua kiambishi ya cha wingi katika upatanisho wa kisarufi. Hivyo mwanafunzi amefanya kosa hili kwa sababu ya kuchopeka kiambishi ma cha wingi katika nomino dakika, badaye kosa la uchopekaji wa kiambishi ya likasababisha kosa la uchopekaji wa kiambishi ma cha wingi katika nomino saa ambayo pia ni nomino ya umbo moja katika umoja na wingi. Kwa hivyo, sentensi hii inatakikana kuwa; Dakika zilienda zikawa saa. (ii) Tuliwapigia simu na baada ya masaa machache tuliona gari la wazimamoto. badala ya Tuliwapigia simu na baada ya saachache tuliona gari la wazimamoto. Mfano: (iii) Tulikula na tukanywa mpaka tumbozetu zikafura kama kiriba. badala ya Tulikula na tukanywa mpaka matumbo yetu yakafura kama kiriba.

109 4.2.3 Kutafuta vyanzo vya makosa ya kisarufi aliyotambulisha mtafiti. Makosa yaliyotambulishwa yaliainishwa kama ifuatavyo:- (i) (ii) (iii) Makosa ya udondoshaji. Makosa ya uchopekaji Makosa ya hijai / tahajia (iv) Makosa ya mfuatano wa vipashio katika sentensi. Kulingana na ujuzi wa mtafiti katika sarufi, makosa yaliyojitokeza katika kazi za wanafunzi, yalisababishwa na vyanzo mbalimbali. Vyanzo hivi vikiwa ni:- (i) Wanafunzi kutokuwa makini wakati wanapofanya mijarabu ya insha za lugha ya Kiswahili. (ii) (iii) (iv) Wanafunzi kutozingatia baadhi ya sheria za lugha ya Kiswahili. Athari za lugha ya kwanza (Kigiriama) katika lugha ya pili (Kiswahili) Ujumuishaji wa maendelezo ya lugha ya kwanza (Kigiriama) na lugha ya pili (Kiswahili). (i) Wanafunzi kutokuwa makini wakati wanapofanya mijarabu ya insha za lugha ya Kiswahili, aidha kukosa kupitia kazi zao kabla ya kuzitoa kwa mtahini. Wanafunzi wanapopewa mjarabu wa kuandika insha za lugha ya Kiswahili, hupewa na maagizo. Miongoni mwa maagizo haya huwa ni muda wa kuandika insha, ambao huwa dakika arubaini (dak.40). Aidha wanafunzi hufahamishwa urefu wa insha kuwa usiopungua ukurasa mmoja na nusu wa karatasi wanazopewa. Hivyo, wanafunzi huchukulia muda kuwa mchache hali ya

110 kwamba hauwatoshi kuwasilisha hoja zao. Kwa hivyo, wanafunzi huandika kwa kasi sana ili waweze kumaliza hoja zao ndani ya muda wa dakika arubaini, kisha kwa urefu uhitajikao. Hivyo basi, wanafunzi hukosa wakati wa kufikiria zaidi na kupanga wanayokusudia kuandika. Hatimaye, huandika wasiyokusudia wakifanya makosa ya kila aina hususan makosa ya kisarufi. Aidha, hukosa wakati wa kupitia nakala zao kabla ya kuzitoa kwa mtahini. Sentensi zifuatazo zilikuwa na makosa ya udondoshaji ambayo mwanafunzi angeweza kuyaepuka kama angekuwa makini wakati akiandika insha yake au kwa kupitia kazi yake kabla ya kutoa kwa usahihishaji. (i) Zawadi hazikujulika* ziwekwe wapi.badala ya :Zawadi hazikujulikana ziwekwe wapi. (ii) (iii) (i) Alikuwa akisema amepata kumbe amepatika*.badala ya: Alikuwa akisema amepata kumbe amepatikana Wanafunzi kutozingatia baadhi ya sheria za lugha ya Kiswahili. Kila lugha ina sheria zake. Ili kudumisha lugha, sheria za lugha lazima zitekelezwe kikamilifu. Lugha ya Kiswahili inazo sheria mbalimbali. Baadhi ya sheria hizi ni;

111 (a).nomino za lugha za kigeni hazihitaji viambishi vyovyote vya wingi. Kwa mfano; Umoja Sahani yangu Shati yangu Wingi Sahani zangu Shati zangu Jedwali 19: Kielelezo cha Nomino za Kigeni zisizohitaji viambishi vya wingi. Miongoni mwa sentensi za wanafunzi ambazo nomino za kigeni ziliambishwa ili kuonyesha hali ya wingi ni; Niliingia chumbani mwangu nikaanza kubukua makaratasi ya mitihani. Badala ya; Niliingia chumbani mwangu nikaanza kubukua karatasi ya mitihani. (b).ukanushaji wa vitenzi katika wakati uliopita, katika nafsi ya pili. Kiambishi ha hutumika lakini irabu /a/ hudondoshwa inapotangulia mofimu /u/ ya nafsi. Hivyo kikanushi ha hutokezea kama h. Kisha mofimu li ya wakati hudondoshwa na badala yake mofimu ku huchopekwa. Kwa mfano; 1 a) Ulikataa kufanya adhabu ndipo ukafukuzwa. b) Hukukataa kufanya adhabu ndipo hukufukuzwa. 2 a) Ulifika kuchelewa.

112 b) Hukufika kuchelewa. Kutozingatia sheria za lugha husababishwa na ; (i) (ii) Kutojali sheria husika. Wanafunzi kutofundishwa sheria za muktadha husika na iwapo walifundishwa hawakuelewa jinsi ya kutumia sheria hizo. (iii) Wanafunzi kutofanya au kutopewa mazoezi ya kutosha baada ya kufunzwa sheria ngeni. Kwa hivyo wanafunzi husahau jinsi ya kutekeleza sheria waliyofunzwa katika uundaji wa sentensi za lugha ya Kiswahili.Kwa mfano; Katika usemi wa taarifa, neno leo hubadilika na kuwa siku hiyo ilhali ta huwa nge. Miongoni mwa sentensi zilizokiuka sheria hii katika kazi ya wanafunzi ni; Shangazi alisema ataenda Mombasa leo, badala ya; Shangazi alisema angeenda Mombasa sikuhiyo. (ii) Athari za lugha ya kwanza (Kigiriama) katika lugha ya pili (Kiswahili). Kulingana na Nadharia ya Uchanganuzi Linganuzi ya Lado (1957),katika kujifunza lugha ya pili, wanafunzi huwa na tabia ya kuhamisha miundo ya L 1 na kuitumia katika L 2. Hivyo, lugha ya pili huathirika kiasi cha kuwa na makosa ya kisarufi. Mtafiti alitumia Nadharia ya Uchanganuzi Linganuzi (N.U.L) iliyoasisiwa na Lado (1957) katika kutambulisha sentensi zilizokuwa na makosa ya kisarufi yaliyosababishwa na lugha ya Kigiriama. Miongoni mwa sentensi zilizotambulishwa kuwa na makosa ya kisarufi yaliyosababishwa na athari za L 1 ni,

113 Mfano 1; a) Ilikuwa siku ya Jumapili na jioni tulipokuwa tukienda nyumbani Sentensi iliyotolewa hapo juu ilinukuliwa kutokana na insha ya mwanafunzi. Sentensi hii ina kosa lauchopekaji wa kiunganishi na kilichokolezwa wino. Kosa hili limesababishwa na athari ya Kigiriama. Katika lugha ya Kigiriama sentensi hii inasoma, b) Yakala siku ya Jumapili na dziloni furihokala fuchenda mudzini. Kisarufi sentensi hii inastahili kusoma, c) Ilikuwa siku ya Jumapili jioni tulipokuwa tukienda nyumbani. Katika kulinganisha miundo ya sentensi 1 (a) na 1 (b), ni wazi kwamba iko sawasawa, kumaanisha mwanafunzi alihamisha muundo wa sentensi 1 (b) na kutunga sentensi 1(a) kisha akaitumia katika uandishi. Japo lugha hizi zote mbili Kigiriama (L 1 ) na Kiswahili (L 2 ) ni lugha za kibantu, sentensi 1 (a) ina makosa ya kisarufi. Mfano 2: 2 a) Nilifikia mahali pengine palipokuwa na sherehe.(sentensi yenye makosa kutokana na L1) b) Nafikira hatu hangine harihokala na shughuli.(sentensi 2(a) katika L1) c) Nilifika mahali pengine palipokuwa na sherehe.(sentensi sahihi) Kitenzi nilifikia 1 (a) kilinyambuliwa katika kauli ya kutendea. Katika mazingira ya sentensi kitenzi nilifikia kilistahili kunyambuliwa katika kauli ya kutenda. Mwanafunzi alitumia muundo wa lugha yake ya kwanza 2(b) katika unyambuaji wa kitenzi hiki. Hali hii

114 ilisababisha makosa ya kisarufi katika sentensi 2(a). Kwa hivyo, mwanafunzi angenyambua sentensi hii katika kauli ya kutenda ambayo ingesoma kama sentensi 2(c) hapo juu. (iv) Ujumuishaji wa sheria za lugha ya kwanza (Kigiriama) na sheria za lugha ya pili (Kiswahili). Richard (1974), anatoa fasili ya ujumuishaji kuwa kutojali mipaka ya sheria yaani utumiaji wa sheria katika muktadha usiokuwamo. Mtafiti alibaini mojawapo ya vyanzo vya makosa ya kisarufi kuwa ujumuishaji.mtafiti alibaini vyanzo hivi kwa kuongozwa na Nadharia ya Uchanganuzi Linganuzi (N.U.L) ya Lado (1957). Lado anasema, wanafunzi wa L 2 huhamisha maana kutoka L 1 hadi L 2 kwa hivyo mwanafunzi huwa na desturi ya kuunda miundo ya lugha lengwa kulingana na tajriba aliyonayo katika lugha anayoifahamu. Hivyo basi, mwanafunzi huigiza miundo aliyozoea katika L 1 kwa kujifunza L 2. Data ya utafiti ilidhihirisha ujumuishaji wa sheria za L 1 na sheria za L 2 zaidi katika mofimu za umoja na wingi wa nomino katika sentensi. Katika lugha ya Kiswahili umoja na wingi wa nomino huthibitishwa na uchopekaji wa viambishi awali au kutochopeka viambishi vyovyote. Nomino kutoka lugha za kigeni ndizo ambazo hazihitaji mofimu zozote kwani hubaki kama mofimu huru katika hali yoyote iwayo.utaratibu wa kuchopeka viambishi awali mwanzoni mwa mzizi wa nomino ili kuunda wingi wa nomino hufanyika katika nomino za lugha za kibantu pekee (Masamba 2001).

115 Kwa mfano; Nomino katika lugha za kibantu Nomino katika lugha za kigeni Umoja Wingi Umoja Wingi Kitabu kitanunuliwa Vitabu vitanunuliwa Meza imechafuka Meza zimechafuka Mti umeanguka Miti imeanguka Roketi ilianguka Roketi zilianguka Msichana amepotea Wasichana wamepotea Samaki ameoza Samaki wameoza Jedwali 20:Kielelezo cha Nomino za kibantu na nomino za kigeni katika hali yaumoja na wingi katika sentensi. Lugha ya kigiriama (L 1 ) na lugha ya Kiswahili (L 2 ) zikiwa miongoni mwa lugha za kibantu, nomino nyingi katika lugha hizi huchopekwa mofimu ili kuziunda katika wingi. Takriban viambishi vyote vya wingi katika lugha hizi (L 1 na L 2 ) vinafanana. Kwa mfano; Kigiriama (L 1 ) Kiswahili (L 2 ) Umoja Wingi Umoja Wingi Mkono udzabandika Mikono idzabandika Mkono umevunjika Mikono imevunjika Kihi changu ni kisha Vihi zhangu ni visha Kiti changu ni kipya Viti vyangu ni vipya Sikiro rinaluma Masikiro ganaluma Sikio linauma Masikio yanauma Jedwali 21:Kielelezo cha Uambishaji wa nomino za L1 na L2 katika hali ya umoja na wingi. Utaratibu ulioonyeshwa hapo juu ni tofauti na utaratabu wa kuunda nomino za wingi kutokana na lugha za kigeni. Nomino za kigeni hazihitaji viambishi ili kuziunda kwa wingi katika lugha ya Kiswahili japo huambishwa katika lugha ya kigiriama.

116 Kwa mfano: Kigiriama (L 1 ) Kiswahili (L 2 ) Umoja Wingi Umoja Wingi Nipa karathasi Nipa makarathasi Nipe karatasi Nipe karatasi Adzagula sahani Adzagula masahani Amenunua sahani Amenunua sahani Nidzaona polisi Nidzaona mapolisi Nimeona polisi Nimeona polisi Jedwali 22: Kielelezo cha Uambishaji wa Nomino za kigeni katika L1 (Kigiriama) katika hali ya wingi. Kulingana na N.U.L ya Lado (1957),anasema kwamba baadhi ya makosa ya kisarufi husababishwa na ujumuishaji wa sheria za uundaji wa nomino za wingi katika L1 na L2.Baadhi ya sentensi zilizobainishwa zikiwa na makosa ya kisarufi yaliyosababishwa na ujumuishaji ni miongoni mwa; Mfano (i); Tuliwapigia rununu na baada ya masaa machache tuliona gari la wazimamato. Mwanafunzi alichopeka mofimu ma ya wingi mwanzoni mwa nomino saa kimakosa. Kosa hili likasababbisha uchopekaji wa mofimu ma katika kivumishi chache na kuwa machache. Sentensi hii inastahili kusoma, Tuliwapigia rununu na baada ya saa chache tuliona gari la wazima moto. Mfano (ii); Niliendelea kustadi makaratasi ambayo yalikuwa ni ya mitihani iliyopita.

117 badala ya Niliendelea kustadi karatasi ambazo zilikuwa ni za mitihani iliyopita Kutathmini kiwango cha Makosa yaliyotambulishwa katika data ya utafiti. Makosa ya kisarufi yaliyobainika katika utafiti ni; 1. Makosa ya udondoshaji. 2. Makosa ya uchopekaji. 3. Makosa ya hijai/tahajia. 4. Makosa ya mfuatano wa vipashio. Makosa haya hubainishwa katika matumizi ya lugha ya Kiswahili katika uandikaji wa insha.ili mwanafunzi aweze kutambua jinsi ya kuepuka makosa haya na kuwa mwandishi mzuri wa insha za lugha ya Kiswahili, ni lazima awe na umilisi wa lugha ya Kiswahili. Makosa ya kisarufi yaliyobainishwa katika utafiti yaliainishwa katika viwango vya kila aina ya makosa kisha vikabainishwa kama ifuatavyo;

118 KANDA MAKOSA YA KISARUFI Udondoshaji Uchopekaji Hijai Mipangilio Jumla Ya Vipashio Ganze Bamba Vitengeni Jumla Jedwali 23:Kielelezo cha aina za makosa ya kisarufi na viwango vyake katika kila kataya Ganze. Aina za makosa ya kisarufi Udondoshaji Uchopekaji Hijai Mfuatano wa vipashio Jumla Jumla Asilimia Jedwali 24: Kielelezo cha viwango vya aina za makosa ya kisarufi.

119 2500 Kiwango cha makosa KEY Ud - Udondoshaji Uch - Uchopekaji H -Hijai Mp - Mpangilio 0 Makosa Jedwali 25: Kielelezo cha viwango vya aina za makosa ya kisarufi katika grafu. Kulingana na matokeo ya utafiti, makosa ya kisarufi katika insha za wanafunzi yanathibitisha uandishi mbaya wa wanafunzi katika insha za lugha ya Kiswahili ambayo yanchangia pakubwa katika matokeo ya mitihani. Wanafunzi wa darasa la nane wa mwaka 2014 kata ya Ganze walikuwa elfu tatu, mia nne sabini na wanane (3478). Kati ya idadi hii, walioshiriki katika utafiti walikuwa mia tatu hamsini na tisa (359). Katika insha mia tatu hamsini na tisa (359), makosa ya kisarufi yaliyobainishwa ni elfu saba, mia saba na arubaini na moja (7741). Ikiwa idadi ndogo 359 kati ya 3478 ilifanya makosa 7741 ya kisarufi, ina maanisha idadi ya wanafunzi ambao hawakushiriki (3119) katika utafiti ingetoa makosa mengi zaidi ya kisarufi. Hili ni thibitisho kwamba kuna makosa mengi ya kisarufi. Makosa haya hupunguza alama za wanafunzi katika mitihani, kwani kwa kila kosa la kisarufi, mwanafunzi hupunguziwa nusu alama. Kwa hivyo, mwanafunzi anapofanya

120 makosa mengi ya kisarufi, hupoteza alama nyingi, hatimaye huanguka mtihani. Kulingana na kiwango cha makosa ya kisarufi yaliyobainishwa katika utafiti (7741), ni wazi kwamba wanafunzi wanafanya makosa mengi ya kisarufi katika uandikaji wa insha, hivyo basi wanapoteza alama nyingi. Hili ni dhihirisho wazi kwamba, makosa ya kisarufi yanachangia pakubwa katika kuanguka kwa mitihani kwa wanafunzi Kurekebisha makosa ya kisarufi yaliyotambulishwa katika data ya utafiti. Ili kuboresha uandikaji wa insha na kuboresha matokeo ya mtihani wa Kiswahili, yatakikana makosa haya yarekebishwe. Kurekebisha makosa ya kisarufi kunahitaji mbinu mwafaka ambazo zitakuwa wazi kwa wanafunzi na walimu. Mtafiti alitoa mbinu za kirekebisha makosa ya kisarufi kama ifuatavyo; (ii) (iii) (iv) (v) (vi) (i) Wanafunzi wafundishwe vyema jinsi ya kuunda maneno na sentnsi sanifu za lugha ya Kiswahili wakiwa katika madarasa ya chini ili wapate msingi mzuri wa lugha ya Kiswahili. Ikiwa msingi bora wa lugha ya Kiswahili ni mwanafunzi kujua silabi za lugha ya Kiswahili. Kutekeleza haya, walimu wanapaswa kuzingatia stadi zote za lugha katika ufundishaji wa lugha ya Kiswahili. Stadi za lugha ya Kiswahili zikiwa ni kusikiliza, kuzungumza, kusoma na kuandika. Walimu watoe mazoezi ya kutosha katika uandikaji wa insha kuanzia madarasa ya chini. Marekebisho ya makosa ya kisarufi yatakayobainishwa katika kazi za wanafunzi yaelezewe wanafunzi darasani. Kupitia kwa washika dau wa elimu wengine, walimu wahakikishe somo la lugha ya Kiswahili lina vitabu vya kusoma vya kutosha. Walimu wadumishe uhusiano mwema na wanafunzi ili kuwavuta karibu zaidi na waweze kupenda somo la insha za lugha ya Kiswahili. Wanafunzi wanaofanya vizuri wapewe motisha ya aina yoyote ili kuzidi kuwapa msukumo wa kufanya vizuri zaidi. Aidha, wanafunzi ambao utendaji wao si mzuri, waweze kufanya bidii pia.

121 (vii) Walimua wa somo la insha za lugha ya Kiswahili wazingatie alama ya wastani wa kihesabu ya insha ili waweze kufahamu vyema utendaji wa wanafunzi. 4.3 Matokeo ya Mahojiano kwa Walimu Miongoni mwa sampuli ya utafiti ni walimu wa somo la insha za Kiswahili katika shule za msingi katika kata ya Ganze. Mtafiti alishirikisha walimu ishirini na wane (24) katika ukusanyaji wa data kwa njia ya maswali ya mahojiano. Walimu walitoa michango yao kwa kutoa maelezo kulingana na maswali ya utafiti.michango ya walimu ilimsaidia mtafiti katika kutoa mapendekezo ya utafiti. Katika swali la kwanza, mtafiti alitaka kujua changamoto wanazopata walimu kutoka kwa wanafunzi katika ufundishaji wa insha. Walimu walioshiriki walitoa changamoto zifuatazo; 1. Si wanafunzi wote wanaofanya mazoezi ya insha yanayotolewa na walimu. 2. Kati ya wanafunzi wanaofanya mazoezi, baadhi yao hukosa kutoa daftari zao kwa usahihishaji. 3. Baadhi ya wanafunzi hukosa kuhudhuria kipindi cha somo la insha. 4. Wanafunzi kutokuwa wabunifu, kwani huunda insha zao kwa kurudia mifano ya insha wanayopewa na walimu wakati wakiwafundisha. Mtafiti aliendelea kutaka kujua sababu za wanafunzi kutofanya mazoezi, kutotoa daftari zao kwa usahihishaji na kutohudhuria vipindi vya somo la insha. Maelezo yaliyotolewa ni kwamba, wanafunzi hutoa sababu za kutokuwa na daftari na kalamu za risasi za kuandika insha. Aidha, wanafunzi wasiotoa daftari kwa usahihishaji hutoa sababu kuwa viranja wahusika huwa tayari wamepeleka daftari za wengine. Kwa

122 hivyo, hukataa kupeleka daftari za wanafunzi wanaomaliza kazi zao kuchelewa. Kuhusu wasiohudhuria vipindi vya insha,walimu wanne walisema kuwa wanafunzi hutoa sababu ya kuwa wagonjwa ilhali walimu wanane walisema huwa hawashughuliki kujua sababu ya wanafunzi kutohudhuria vipindi vya insha. Mtafiti alitaka kujua hatua ambazo walimuhuchukua kwa wanafunzi hawa. Walimu walieleza kwamba, hutoa adhabu kwa wanafunzi, kisha wanafunzi hufanya adhabu na baadaye baadhi yao hususia kufanya mazoezi ya insha. Kwa hivyo, walimu huwafutilia mbali wanafunzi hawa na huendelea na wale wanaojitolea kufanya mazoezi, kwani walimu husema Ukitaka fanya, usipotaka hulazimishwi, wacha, usinipe stress. Katika swali la pili, mtafiti alitaka kujua aina za makosa ya kisarufi wanayofanya wanafunzi katika uandikaji wa insha. Walimu walieleza kwamba, wanafunzi hufanya makosa ya kisarufi ya upatanisho wa kisarufi katika ngeli, njeo na hijai. Makosa ya mfuatano wa vipashio yalikuwa machache. Waliongeza kwamba, kazi ya wanafunzi hukosa mtiririko hususan sentensi wanazotunga. Katika swali la tatu,mtafiti alitaka ufafanuzi wa makosa yanayojitokeza mara kwa mara katika insha za wanafunzi. Maelezo yaliyotolewa na walimu ni kwamba, makosa ya njeo yalijitokeza zaidi kuliko makosa ya ngeli kisha makosa wanafunzi kutozingatia marekebisho yanayotolewa na walimu baada ya ya tahajia kisha ya ngeli. Katika swali la nne, mtafiti alitaka kujua sababu zinazochangia wanafunzi kufanya makosa ya kisarufi.nao walimu walitoa sababu zifuatazo;

123 (i) Wanafunzi kutozingatia marekebisho yanayotolewa na walimu baada ya usahihishaji. (ii) kuwa Wanafunzi kukosa kusoma vitabu vya lugha ya Kiswahili. Vitabu hivi wakaeleza ni vitabu vya hadithi za Kiswahili. Waliongezea kuwa ukosefu wa usomaji wa vitabu vya hadithi husababisha wanafunzi kutokuwa na stadi ya Kiswahili, ambazo ni kusikiliza, kuongea, kuandika na kusoma. (iii) Wanafunzi kukosa kuwa makini wakati wanapofanya mazoezi ya uandishi wa insha kwani huandika insha kwa pupa au harakaharaka kwa sababu ya kukimbilia wakati waliopewa. (Dak.40). Hatimaye, mtafiti alitaka kujua alama za wastani wa kihesabu ambayo wanafunzi hupata zaidi kila wanapoandika insha. La kustaajabisha ni kwamba, hakukuwa na mwalimu yeyote aliyeshughulika kutafuta alama ya wastani wa kihesabu katika somo la insha za Kiswahili. Walimu walieleza kuwa, wao hushughulika kutafuta alama ya wastani wa kihesabu wa somo zima la Kiswahili.

124 SURA YA TANO HITIMISHO NA MAPENDEKEZO 5.1 Utangulizi Utafiti huu ulinuia kuchunguza makosa ya kisarufi katika uandikaji wa insha wa wanafunzi wa shule za msingi katika kata ya Ganze. Katika kuendeleza utafiti, mtafiti aliongozwa na Nadharia ya Uchanganuzi Makosa (N.U.M) ikisaidiwa na Nadhiria ya Uchanganuzi Linganuzi (N.U.L). Katika kutimiza malengo ya utafiti, mtafiti aliongozwa na nadharia tete.katika sura hii, mtafiti anajadili matokeo ya utafiti kwa kuthibitisha ukweli wa nadhria tete za utafiti, hatimaye anatoa mapendekezo kulingana na matokeo ya utafiti Hitimisho Mtafiti anatoa hitimisho la utafiti kwa kujadili nadharia tete za utafiti. (i)nadharia tete ya kwanza Kuna makosa mengi ya kisarufi katika insha za Kiswahili za wanafunzi wa shule za msingi, kata ya Ganze. Kulingana na uchanganuzi wa data ya utafiti, mtafiti alitambulisha makosa mengi ya kisarufi yaliyojitokeza katika insha za wanafunzi.miongoni mwa makosa haya ni makosa ya udondoshaji na uchopekaji wa viambishi virejeshi, viambishi vya umoja na wingi, viambishi vya mnyambuliko viambishi shamirisho na vinginevyo. Aidha, makosa ya udondoshaji na uchopekaji wa maneno katika sentensi kama vile; nomino, vitenzi vivumishi na mengineyo yalidhihirika.

125 Zaidi ya hayo, makosa ya hijai na makosa ya mfuatano wa vipashio yalitambulishwa wazi. Makosa yaliyokuwa katika kazi za wanafunzi ni mengi sana lakini mtafiti alishughulikia makosa ya kimofosintaksia pekee. Makosa ya kisarufi yaliyokuwa ya kifonolojia, kisemantiki na baadhi ya makosa ya hijai kama uakifishaji hayakushughulikiwa, kwa sababu hayakuwa katika upeo wa utafiti. Insha zilizoshughulikiwa na mtafiti zilikuwa mia tatu hamsini na tisa (359) kutoka kwa wanafunzi wa darasa la nane wa shule za msingi katika kata ya Ganze. Wanafunzi wa darasa la nane wa mwaka 2014 kata yaganze walikuwa elfu tatu, mia nne sabini na wanane (3478). Kati ya idadi hii, walioshiriki katika utafiti walikuwa mia tatu hamsini na tisa (359). Katika insha mia tatu hamsini na tisa (359), makosaya kisarufi yaliyobainishwa ni elfu saba, mia saba na arubaini na moja (7741). Ikiwa idadi ndogo 359 kati ya 3478 ilifanya makosa 7741 ya kisarufi, ina maanisha idadi ya wanafunzi ambao hawakushiriki (3119) katika utafiti ingetoa makosa mengi zaidi ya kisarufi. Hili ni thibitisho kwamba kuna makosa mengi ya kisarufi. (ii)nadharia tete ya pili Kuna aina nyingi za makosa ya kisarufi katika insha za wanafunzi. Mtafiti aliainisha makosa ya kisarufi aliyotambulisha katika insha ya wanafunzi, hatimaye akabainisha aina nne kuu. Aina za makosa zilizobainishwa ni; i) Makosa ya udondoshaji. ii) iii) Makosa ya Uchopekaji. Makosa ya hijai / tahajia.

126 iv) Makosa ya mfuatano wa vipashio.katika sentensi. (iii)nadharia tete ya tatu Kuna vyanzo vingi vinavyosababisha kuweka kwa makosa ya kisarufi. Baadala ya mtafiti kuchunguza makosa yaliyofanywa na wanafunzi, alibaini kwamba, kuna vyanzo mbalimbali vilivyosabbaisha makosa haya. Mtafiti alibainisha vyanzo hivi kuwa pamoja na; a) Wanafunzi kukosa umakini wakati wanapoandika insha. b) Wanafunzi kuathiriwa na lugha yao ya kwanza katika kujifindisha lugha ya pili. c) Wanafunzi kutofahamu au kutozingatia sheria za kugha ya Kiswahili. d) Wanafunzi kutopata wakatiwa kupitia insha zao kabla ya kuzitoa kwa usahihishaji Vyanzo vya kufanya makosa ya kisarufi vilivyoorodheshwa hapo juu na vingine ambavyo havimo katika orodha hii, ni dhahiri kuwakuna makubaliano makubwa kati ya matokeo ya utafiti na nadharia tete ya tatu. Kulingana na matokeao ya utafiti, makosa ya kisarufiyaliyobainishwa yanathibitisha kuwa changizo kuu ya matokeo mabaya ya mitihani ya Kiswahili. Hivyo, ilimulazimu mtafiti kutoa mapendekezo ya njia za kurekebisha makosa haya ili kudumisha na kuboresha uandikaji wa insha za Kiswahili iwapo mapendekezo yatatekelezwa Mapendekezo Utafiti huu umethibitisha kwamba makosa ya kisarufi yanachangia kwa kiwango kikubwa matokeo mabaya ya mitihani katika shule za msingi, kata ya Ganze.

127 Katika utafiti huu, makosa ya kisarufi yaliyokithiri kulingana na ukubwa wa changizo ya matokeo mabaya ni makosa ya uchopekaji, makosa ya udondoshaji, hijai au tahajia na makosa ya mpangilio wa vipashio katika sentensi. Ili kurekebisha makosa haya na kuboresha uandishi wa wanafunzi katika somo la Kiswahili, aidha kudumisha lugha ya Kiswahili katika kata ya Ganze, maeneo yote ya Mkoa wa pwani na nchini Kenya kote, mtafiti anatoa mapendekezo yafuatayo: i) Walimu wahakikishe kwamba wanafunzi wanapata msingi mzuri wa uundaji wa maneno ya lugha ya Kiswahili kwa kutumia mofimu mwafaka katika nafasi sahihi katika sentensi. ii) Walimu wahakikishe wanawahusisha wanafunzi katika kusoma vitabu vya hadithi za Kiswahili mara kwa mara. Jambo hili litawezesha wanafunzi kufahamu zaidi jinsi ya kupanga mofimu ili kuunda maneno na sentensi sanifu. Vilevile, kupitia usomaji wa vitabu vya hadithi, wanafunzi watapata ujuzi wa kuwa wabunifu. iii) Kulingana na Nadharia ya Uchanganuzi Makosa (N.U.M) Corder (1967) anasema, wanafunzi wasiadhibiwe kwa kufanya kosa, bali kosa lichukuliwe kama kigezo cha ujifunzaji wa L2. Kwa hivyo, kwa mjibu wa Corder, mtafiti anapendekeza kuwa walimu wasiadhibu wanafunzi kwa kufanya makosa. Aidha, adhabu husababisha mwanafunzi kuwa na mwelekeo hasi juu ya masomo, pia kwa walimu. Hali hii huzidisha kudidimia kwa ushirikiano baina ya walimu na wanafunzi. Inapofika hatua hii, kufaulu kwa mwanafunzi huwa finyu. Kwa hivyo, mtafiti anapendekeza kwamba badala ya kuadhibu wanafunzi, walimu wawape motisha wanafunzi kwa kuwatuza wanaofanya

128 vizuri katika insha. Wanafunzi hawa watuzwe mbele ya wanafunzi wenziwao mbele ya darasa ili wawe kielelezo kwa wanafunzi wengine. Aidha, walimu wawapangie wanafunzi matembezi maalum ya kimasomo. iv) Wanafunzi wafanye mijarabu zaidi ili wapate mazoezi ya kutosha katika uandikaji wa insha. v) Walimu wafanye marekebisho ya makosa yanayofanywa na wanafunzi katika uandikaji wa insha. Marekebisho haya yafanywe darasani pamoja na wanafunzi wote. Kwa kufanya hivi, wanafunzi watajua makosa yao na jinsi ya kuyarekebisha na kuyaepuka. vi) Kulingana na mchango wa walimu kupitia maswali ya mahojiano katika utafiti kuwa wanafunzi hufanya makosa ya kisarufi kwa sababu ya kukimbilia wakati (dak.40), mtafiti anapendekeza kwamba walimu wawapatie wanafunzi muongozo wa kugawanya muda wanaopewa katika uandikaji wa insha. Mwongozo huu, uambatane na mazoezi ya kutosha ili wanafunzi wapate uzoefu wa matumizi ya muda unaostahili. Hali hii itawafanya wanafunzi waweze kuwa makini wakati wanapofanya mijarabu ya insha za lugha ya Kiswahili. vii) Mchango wa walimu kuhusu alama ya wastani wa kihesabu katika somo la insha ni kwamba walimu huzingatia alama ya wastani ya somo zima la Kiswahili bali sio sehemu ya insha, Hivyo basi, mtafiti anapendekeza kuwa, walimu wahakikishe wanatoa alama ya wastani wa kihesabu kwa kila mjarabu wa insha na kwa kila mwanafunzi. Hatua hii itawawezesha walimu kufahamu vyema kiwango cha umilisi wa lugha ya Kiswahili wa kila mwanafunzi. Vilevile, walimu watajua vyema wanafunzi wanaohitaji kupata usaidizi zaidi katika uandikaji wa insha hususan katika kipengele gani cha lugha.

129 viii) Walimu waalike walimu wengine kutoka sehemu nyingine ambazo somo la insha linafanya vizuri ili wazungumze na wanafunzi wao kuhusu somo la lugha ya Kiswahili. Hatua hii itawafanya wanafunzi wapate ari ya kufaulu. Aidha, wanafunzi hawa watachukua lugha ya Kiswahili kuwa somo, bali sio lugha ya kawaida. ix) Watungaji wa mitaala wahakikishe wanazingatia sehemu zote za lugha ya Kiswahili ili walimu waweze kufundisha kila kipengele kinachohitajika katika ujifunzaji wa lugha ya Kiswahili. Iwapo mapendekezo ya mtafiti yatatekelezwa, yatawanufaisha wanafunzi katika kutambua makosa ya kisarufi ambayohufanya katika uandishi wa insha. Aidha, wanafunzi watanufaika kupitia kwa walimu wao ambao kulingana na ushauri wao na mapendekezo ya mtafiti, watatambua kanuni za lugha ya Kiswahili kuhusu aina na vyanzo vya makosa ya kisarufi. Walimu wa lugha ya Kiswahili nao kupitia mapendekezo ya mtafiti, wataimarisha mbinu za ufundishaji kisha wataweza kusaidia wanafunzi kupita mitihani ya lugha ya Kiswahili. Hatimaye, walimu wataweza kutambua njia za kupunguza na kukabiliana na aina mbalimbali za makosa ya kisarufi. Waandishi wa vitabu vya sarufi vya shule za msingi watanufaika kwa kuandika vitabu vya sarufi wakijua vyanzo vya makosa ya wanafunzi ili watoe mafunzo na mazoezi yanayokabiliana na aina za makosa yaliyodhihirishwa katika utafiti huu.

130 MAREJELEO. Corder, S.P (1967) The significance of learners errors International Review of applied linguistics Vol. 5 (1971) Idiosyncratic Dialects and Erro Analysis International Review of applied linguistics Vol. ix: (1974) Error Analysis in J. Allen and S. Corder (eds) Vol. 3 Oxford University Press. (1978) The significance of Learners Errors In Richards J. C. Error Analysis; Perspective on second Language Acquisition. Longman. London. Campbell, Z. M na Qorro M. A (1997) Language Crisis in Tanzania Mkuki na Nyota Publishers, Dar-es-Salam Dulay & Burt (1978) Error and Strategies on Child second Language Learning In Tesol Quarterly. Vol. 8 pp Ellis & Rathbone (1978), Instructed Second Language Acquisition Learning in the classroom T.J. Press Ltd. Great Britain. Els na wenzake (1984), Applied Linguistics and the Learning and Teaching of Foreign

131 Languages. Edward Arnold, London. Gass & Selinker (2008), Second Language Acquisition Routeledge pp 103. The role of native language: A historical overviewnew York and London He Dan (2010), On Error Analysis of English Major Writing from the Perpespective of Interlanguage Katika Journal of Language and Literature Studies. ( ) Halliday, M.A.K et al (1964), The Linguistic Science and Language Teaching Longman. London. James, C (1980), Constructive Analysis.Longman. London Kevogo, D. (2007), Makosa ya Kisarufi na jinsi yanavyoathiri ujifunzaji wa Lugha ya Kiswahili miongoni mwa jamii ya Waluo, wilayani Bondo. Tasnifu ya Uzamili (isiyochapishwa), Chuo cha Uislamu nchini Uganda. KNEC (1998) Examination Report 1998, 2007, 2009, 2010 Kenya Examination Council. TUKI (2002) Kamusi ya Kiswahili sanifu. Toleo la pili.oxford University Press. K.I.E (1993) Kiswahili kwa darasa la saba. Oxford University Press. Nairobi.

132 Lado,R. (1957), Linguistic Across Cultures. Universities of Micghigan Press Michigan. Oxford. Pergamon Larse-Freeman na Long, M.H (1994), An introduction to language Two Acquisition Research.Longman, London Mangwa, D.O (2005), Athari za Ekegusi katika Kiswahili na zinazochangia matokeo mabaya ya mtihani wa kitaifa wa Kiswahili kwa wanafunzi wa kisii wilayani kisii kusini. Tasnifu ya uzamili (isiyochapishwa) Chuo kikuu cha Egerton. Massamba (2001), Sarufi miundo ya Kiswahili Sanifu (SAMIKISA) Taasisi ya Uchunguzi wa Kiswahili (TUKI) Chuo Kikuu cha Dar-es-Salam. Musa (2008), Athari za lugha ya Kigweno katika Kikiswahili na jinsi zinavyoathiri matokeo mabaya ya mtihani wa kitaifa. Tasnifu ya uzamili (isiyochapishwa) Chuo Kikuu cha Islamic Mbale, Uganda. Mudhune (1994), Matatizo ya Kimofosintaksia yalinayowakumba wanafunzi katika jamii ya Waluo katika kujifunza lugha yakiswahili. Tasnifu ya uzamili (isiyochapishwa) Chuo Kikuu cha Islamic, Uganda. Ng ang a (2002), Makosa ya kisarufi katikainsha za wanafunzi na jinsi yanavyoshughulikiwa na walimu katika tarafa ya Ndaragwa.

133 Tasnifu ya uzamili (isiyochapishwa) Chuo kikuu cha Nairobi. Richards, J.C (1984) ErrorAnalysis Perspecive on Second Language Acquisition Longman. London RISSEA (2011) Ripoti ya kongamano lililofanywa Rissea. Selinker, L (1969) International in IRAL Vol.10 Seliger na Shahamy (1989), Second Language Research Methods. UniversityPress,London. Stockwell, Bowen na Martin (1965), The Grammatical Structures of English andspanish. Chicago:Chicago University Press.

134 VIAMBATANISHO Kiambatanisho 1

135 Kiambatanisho: 2 Ripoti ya Kongamano la Matokeo ya Kiswahili katika Mitihani ya KCPE-KCSE

136 Kiambatanisho: 3 Maswali ya mahojiano kwa walimu. 1. Ni changamoto gani mnazozipata kutoka kwa wanafunzi katika ufundishaji wa insha? 2. Ni makosa gani ya kisarufi wanayofanya wanafunzi katika uandikaji wa insha? 3. Ni makosa gani ambayo hujitokeza mara kwa mara katika insha za wanafunzi? 4. Ni sababu gani zinazowafanya wanafunzi kufanya makosa haya? 5. Ni alama gani ya wastani wa kihesabu ambayo wanafunzi hupata zaidi kila wanapoandika insha?

137 Kiambatanisho: 4 Mada ya insha iliyotelewa kwa wanafunzi kama mjarabu wa insha. Umepewa dakika arubaini (dak.40), andika insha isiyopungua ukurasa mmoja na nusu. Mada ya insha ikiwa; Siku ambayo sitaisahau.

138 Kiambatahisho 5: INSHA 1

139 Kiambatanisho 6: INSHA 2

140 Kiambatanisho 7: INSHA 3

141 Kiambatanisho 8: INSHA 4

142 Kiambatanisho 9: INSHA 5

HISTORIA (WASIFU WA) YA MAREHEMU DKT. WILLIAM AUGUSTAO MGIMWA

HISTORIA (WASIFU WA) YA MAREHEMU DKT. WILLIAM AUGUSTAO MGIMWA HISTORIA (WASIFU WA) YA MAREHEMU DKT. WILLIAM AUGUSTAO MGIMWA (MB) ALIYEKUWA WAZIRI WA FEDHA KATIKA SERIKALI YA AWAMU YA NNE YA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA 1. KUZALIWA Marehemu Dkt. William Augustao

More information

CROP PROTECTION PROGRAMME. Identifying the factors causing outbreaks of armyworm as part of improved monitoring and forecasting systems

CROP PROTECTION PROGRAMME. Identifying the factors causing outbreaks of armyworm as part of improved monitoring and forecasting systems CROP PROTECTION PROGRAMME Identifying the factors causing outbreaks of armyworm as part of improved monitoring and forecasting systems R No 7966 (ZA No 0449) FINAL TECHNICAL REPORT 15 October 2000 31 March

More information

Learning by Ear Unce upon a time... in Africa Episode 3: TRADE IN AFRICA. Author: Marta Barroso Editors: Maja Braun, Jan-Philipp Scholz CHARACTERS:

Learning by Ear Unce upon a time... in Africa Episode 3: TRADE IN AFRICA. Author: Marta Barroso Editors: Maja Braun, Jan-Philipp Scholz CHARACTERS: Learning by Ear Unce upon a time... in Africa Episode 3: TRADE IN AFRICA Author: Marta Barroso Editors: Maja Braun, Jan-Philipp Scholz CHARACTERS: Intro/Outro (female/male) Scene 1: June (13, female) Mum

More information

UCHAMBUZI MUUNGANO WA TANZANIA YA MWAKA 1977

UCHAMBUZI MUUNGANO WA TANZANIA YA MWAKA 1977 UCHAMBUZI WA Katiba Katiba YA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA YA MWAKA 1977 Uchambuzi huu umetayarishwa na Kikundi cha Sheria na Haki za Binadamu cha TIFPA kwa niaba ya wana TIFPA kwa msaada wa Ford Foundation

More information

TOKA SABATO KWENDA JUMAPILI CARLYLE B. HAYNES

TOKA SABATO KWENDA JUMAPILI CARLYLE B. HAYNES TOKA SABATO KWENDA JUMAPILI CARLYLE B. HAYNES TOKA SABATO KWENDA JUMAPILI Mjadala wa kihistoria wa Hoja juu ya Sabato, Ukionyesha Jinsi Gani, Lini, Kwa Nini, na Ni Nani aliyefanya Badiliko hilo kutoka

More information

KWA VILE ni kanuni ya Kanisa Anglikana ulimwenguni ambalo ni sehemu ya Kanisa Katholiko kwamba Dayosisi kadhaa ziungane pamoja na kuunda Jimbo;

KWA VILE ni kanuni ya Kanisa Anglikana ulimwenguni ambalo ni sehemu ya Kanisa Katholiko kwamba Dayosisi kadhaa ziungane pamoja na kuunda Jimbo; UTANGULIZI KWA JINA LA BABA NA MWANA NA ROHO MTAKATIFU, AMIN. KWA VILE ni kanuni ya Kanisa Anglikana ulimwenguni ambalo ni sehemu ya Kanisa Katholiko kwamba Dayosisi kadhaa ziungane pamoja na kuunda Jimbo;

More information

Cambridge International Examinations Cambridge Ordinary Level

Cambridge International Examinations Cambridge Ordinary Level Cambridge International Examinations Cambridge Ordinary Level *6782314084* SWAHILI 3162/01 Paper 1 May/June 2016 Additional Materials: Answer Booklet/Paper READ THESE INSTRUCTIONS FIRST If you have been

More information

THE SPINE CLINIC. Spine Care. Huduma Ya Uti Wa Mgongo Kanuni Za Kutunza Shingo Na Mgongo. principles of neck and back care IOM SYSTEM ENDOSCOPE

THE SPINE CLINIC. Spine Care. Huduma Ya Uti Wa Mgongo Kanuni Za Kutunza Shingo Na Mgongo. principles of neck and back care IOM SYSTEM ENDOSCOPE THE SPINE CLINIC IOM SYSTEM ENDOSCOPE Ideal Work Posture Spine Care BONE SCALPEL principles of neck and back care Huduma Ya Uti Wa Mgongo Kanuni Za Kutunza Shingo Na Mgongo For Appointments & Contact KWA

More information

unajua ulichofanya; umevumilia Vema ninataka umwambia Shetani katika jina la Yesu anapokufanyia jambo baya, Toka! Toka!

unajua ulichofanya; umevumilia Vema ninataka umwambia Shetani katika jina la Yesu anapokufanyia jambo baya, Toka! Toka! Title: Preached by Dr. w eugene SCOTT, PhD., Stanford University At the Los Angeles University Cathedral Copyright 2007, Pastor Melissa Scott. - all rights reserved Somo: Imehubiriwa na Dk. w. eugene SCOTT,

More information

Learning by Ear Once upon a time... in Africa Episode 8: COLONIALIZATION. Author: Marta Barroso Editors: Maja Braun, Jan-Philipp Scholz CHARACTERS:

Learning by Ear Once upon a time... in Africa Episode 8: COLONIALIZATION. Author: Marta Barroso Editors: Maja Braun, Jan-Philipp Scholz CHARACTERS: Learning by Ear Once upon a time... in Africa Episode 8: COLONIALIZATION Author: Marta Barroso Editors: Maja Braun, Jan-Philipp Scholz CHARACTERS: Intro/Outro (female/male) Scene 1: Neighbour (43, male)

More information

KUFANIKISHA MAGEUZI YA SHERIA ZA KUMILIKI ARDHI NCHINI KENYA TOLEO MAARUFU LA MSWADA WA KUMILIKI ARDHI YA JAMII

KUFANIKISHA MAGEUZI YA SHERIA ZA KUMILIKI ARDHI NCHINI KENYA TOLEO MAARUFU LA MSWADA WA KUMILIKI ARDHI YA JAMII Hakijamii Hakijamii Economic and Social Rights Centre (Hakijamii) 53 Park Building, kwenye barabara ya Ring Rd, tawi la Ngong Rd Sanduku la Posta 11356-00100, Nairobi Kenya Simu: +254 020 2589054/2593141

More information

Ikimbieni Zinaa. Ellis P. Forsman. Ikimbieni Zinaa (Flee Fornication) 1

Ikimbieni Zinaa. Ellis P. Forsman. Ikimbieni Zinaa (Flee Fornication) 1 Ikimbieni Zinaa na Ellis P. Forsman Ikimbieni Zinaa (Flee Fornication) 1 Ikimbieni Zinaa na Ellis P. Forsman Oktoba 11, 2011 Ikimbieni Zinaa (Flee Fornication) 2 Ikimbieni Zinaa 1 Kor. 6:18 Wakristo wa

More information

Pasaka Na Meza Ya Bwana Sehemu Ya 2

Pasaka Na Meza Ya Bwana Sehemu Ya 2 Pasaka Na Meza Ya Bwana Sehemu Ya 2 Na Ellis P. Forsman Lord's Supper - Part 2) 1 Pasaka Na Meza Ya Bwana Sehemu Ya 2 Na Ellis P. Forsman Marchi 11, 2013 Lord's Supper - Part 2) 2 Pasaka Na Meza Ya Bwana

More information

HOTUBA YA WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS IKULU NA UTAWALA BORA MHESHIMIWA DKT. MWINYIHAJI MAKAME

HOTUBA YA WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS IKULU NA UTAWALA BORA MHESHIMIWA DKT. MWINYIHAJI MAKAME SERIKALI YA MAPINDUZI YA ZANZIBAR OFISI YA RAIS NA MWENYEKITI WA BARAZA LA MAPINDUZI HOTUBA YA WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS IKULU NA UTAWALA BORA MHESHIMIWA DKT. MWINYIHAJI MAKAME KUHUSU MAKADIRIO YA

More information

Learning by Ear Once upon a time... in Africa Episode One: CRADLE OF MANKIND. Author: Marta Barroso Editors: Maja Braun, Jan-Philipp Scholz

Learning by Ear Once upon a time... in Africa Episode One: CRADLE OF MANKIND. Author: Marta Barroso Editors: Maja Braun, Jan-Philipp Scholz Learning by Ear Once upon a time... in Africa Episode One: CRADLE OF MANKIND Author: Marta Barroso Editors: Maja Braun, Jan-Philipp Scholz CHARACTERS : Intro/Outro (female/male) Scene 1: Mum (38, female)

More information

Ni Nani Aliye Upande Wa Bwana?

Ni Nani Aliye Upande Wa Bwana? Ni Nani Aliye Upande Wa Bwana? (Who Is On The Lord s Side?) Na Ellis P. Forsman Ni Nani Aliye Upande Wa Bwana? (Who Is On The Lord's Side?) 1 Ni Nani Aliye Upande Wa Bwana? (Who Is On The Lord s Side?)

More information

DEFERRED LIST ON 23/10/2018

DEFERRED LIST ON 23/10/2018 DEFERRED LIST ON 23/10/2018 SN WP.NO Employer Applicant name Decision made 1 WPC 9595/16 M/S GA Insurance Tanzania ltd Mr. Amit Srivastava Awasilishe Job description, Mkataba wa ajira, kibali current kutoka

More information

SIMON & SCHUSTER S PIMSLEUR SWAHILI 1 READING BOOKLET

SIMON & SCHUSTER S PIMSLEUR SWAHILI 1 READING BOOKLET SIMON & SCHUSTER S PIMSLEUR SWAHILI 1 READING BOOKLET Travelers should always check with their nation's State Department for current advisories on local conditions before traveling abroad. Booklet Design:

More information

PROPOSED STANDARD COUNCIL LEVEL HOSPITALS. Schedule of Material, Labour & Drawings for Septic and Soak way pit PROJECT AREA TANZANIA MAINLAND

PROPOSED STANDARD COUNCIL LEVEL HOSPITALS. Schedule of Material, Labour & Drawings for Septic and Soak way pit PROJECT AREA TANZANIA MAINLAND THE UNITED REPUBLIC OF TANZANIA PRESIDENT S OFFICE REGIONAL ADMINISTRATION AND LOCAL GOVERNMENT PROPOSED STANDARD COUNCIL LEVEL HOSPITALS Schedule of Material, Labour & Drawings for Septic and Soak way

More information

Taarifa ya Utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM (Oktoba, 2010 hadi Septemba, 2012) kuhusu Zanzibar SERIKALI YA MAPINDUZI YA ZANZIBAR

Taarifa ya Utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM (Oktoba, 2010 hadi Septemba, 2012) kuhusu Zanzibar SERIKALI YA MAPINDUZI YA ZANZIBAR SERIKALI YA MAPINDUZI YA ZANZIBAR Mhe. Dkt. Ali Mohammed Shein Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi TAARIFA YA SERIKALI YA MAPINDUZI YA ZANZIBAR KUHUSU UTEKELEZAJI WA ILANI YA UCHAGUZI

More information

EXL6 Swahili PhraseBook Davis

EXL6 Swahili PhraseBook Davis Swahili or Kiswahili, is an official language of Tanzania, Kenya, the Democratic Republic of the Congo, and Uganda. Swahili speakers can also be found in surrounding countries, such as Burundi, Rwanda,

More information

2017 Student Program Curriculum

2017 Student Program Curriculum 2017 Student Program Curriculum Basic Program Information Host Institution: Program Title: Curriculum Title: Language(s): Grade(s) of Learners: Language Background: Program Setting: Program Type: Duration:

More information

Hennepin County Kiongozi cha jinsi ya kuondoa taka

Hennepin County Kiongozi cha jinsi ya kuondoa taka Hennepin County Kiongozi cha jinsi ya kuondoa taka How to get rid of it guide 2 KIONGOZI CHA JINSI YA KUONDOA TAKA Kiongozi cha jinsi ya kuondoa taka kinatoa mwongozo kijumla wa kuondoa taka kwa wakazi.

More information

JAMUHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA RAIS TAMISEMI

JAMUHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA RAIS TAMISEMI JAMUHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA RAIS TAMISEMI Namba za simu;shule ya Sekondari MIONO Mkuu wa Shule: +255 784 369 381S.L.P 26 - CHALINZE Makamu Mkuu wa Shule: +255 787 448 383Tarehe 25.5.2017

More information

NOVENA YA ROHO MTAKATIFU

NOVENA YA ROHO MTAKATIFU NOVENA YA ROHO MTAKATIFU Mpangilio wa sala na nyimbo kwa siku zote tisa Katoliki.ackyshine.com KWA SIKU ZOTE TISA Ufuatao ni mtiririko wa Novena ya Roho Mtakatifu kwa siku zote tisa. Kusali novena hii

More information

Lesson 60: Quantifiers OTE and O OTE

Lesson 60: Quantifiers OTE and O OTE Lesson 60: s OTE and O OTE OTE [all, entire, whole] The usage of OTE varies from one noun class to another. A). OTE GELI [noun class] WA KI VI I JI A K K JIA [noun] msichana wasichana kijiko vijiko mkoba

More information

The history of Zaire as told and painted by Tshibumba Kanda Matulu in conversation with Johannes Fabian

The history of Zaire as told and painted by Tshibumba Kanda Matulu in conversation with Johannes Fabian 1 sur 37 05.02.2006 0:36 ISSN: 1570-0178 Volume 2, Issue 5 (5 October 1999) The history of Zaire as told and painted by Tshibumba Kanda Matulu in conversation with Johannes Fabian Introduction First Session,

More information

KENYA INSTITUTE OF CURRICULUM DEVELOPMENT EDU CHANNEL TV BROADCAST LINE UP AUGUST DEC 2017 WEEKLY TV PROGRAMMES

KENYA INSTITUTE OF CURRICULUM DEVELOPMENT EDU CHANNEL TV BROADCAST LINE UP AUGUST DEC 2017 WEEKLY TV PROGRAMMES KENYA INSTITUTE OF CURRICULUM DEVELOPMENT EDU CHANNEL TV BROADCAST LINE UP AUGUST DEC WEEKLY TV PROGRAMMES TIME MONDAY TUESDAY WEDNESDAY THURSDAY FRIDAY SATURDAY SUNDAY 6.00 AM - 6.20 AM 6.20AM - 6.25AM

More information

Remarks You Must Read & Know Before Buying Guingamp vs RC Strasbourg Tickets: Event date and time are subject to change - these changes are not

Remarks You Must Read & Know Before Buying Guingamp vs RC Strasbourg Tickets: Event date and time are subject to change - these changes are not {@!!!Video} Mbeya City - Mtibwa Sugar Tazama kutangaza 14.01.2019 Liga Huru HDTV Kuishi. Inasaidia, Mbeya City - Mtibwa Sugar ESPN Angalia.. Online Tangaza Kuishi.. Streaming Sopcast Online. Kuishi WATCH

More information

The history of Zaire as told and painted by Tshibumba Kanda Matulu in conversation with Johannes Fabian

The history of Zaire as told and painted by Tshibumba Kanda Matulu in conversation with Johannes Fabian 1 sur 55 05.02.2006 0:38 ISSN: 1570-0178 Volume 2, Issue 7 (6 June 2000) The history of Zaire as told and painted by Tshibumba Kanda Matulu in conversation with Johannes Fabian Introduction First Session,

More information

QUARTERLY REPORT July - September Quarter SERIES NO. SDT:

QUARTERLY REPORT July - September Quarter SERIES NO. SDT: QUARTERLY REPORT July - September Quarter SERIES NO. SDT: 21-146 i Table 1: Value of Domestic Exports, Re-exports, Imports and Balance of Trade by Month...1 Table 2: Balance of Trade by Institutional Sector...1

More information

Appendix: Tables. Table XI. Table I. Table II. Table XII. Table III. Table IV

Appendix: Tables. Table XI. Table I. Table II. Table XII. Table III. Table IV Table I Table II Table III Table IV Table V Table VI Random Numbers Binomial Probabilities Poisson Probabilities Normal Curve Areas Exponentials Critical Values of t Table XI Table XII Percentage Points

More information

W W W. S P O T - H O G G. C O M

W W W. S P O T - H O G G. C O M i v i i - i i vi i i i i i - i q z i v i iiv v i i i j i i ii i xi i qi i i - j x i i i v i 87 i i 9 : i ivi qi i ii i i 7 V 8 5 i @ K i ii i zz i - j i i) iii i ( jii i i i i i i i i i i i K vi : v K

More information

Nicolae JURAVSCHI NOSC President

Nicolae JURAVSCHI NOSC President Oleg ABALIN NKF RM President Dear Karate friends, Nicolae JURAVSCHI NOSC President Victor ZUBCU Minister of Youth and Sports It is a pleasure for me to enjoy along with all the WKF family the historic

More information

The Passion of Africa

The Passion of Africa Africa is the heart of the world an empire of space, sounds, light, life, people, cultures, magnificence not found elsewhere in the world, Africa is magical, it captivates you with is sights, sounds, scents

More information

How to Form a New Sport Club Any club seeking Sport Club status should follow the following guidelines:

How to Form a New Sport Club Any club seeking Sport Club status should follow the following guidelines: University of West Florida Sport Clubs are groups of students that have a common interest in a competitive sport or recreational activity. The group has joined together and organized to further their interest

More information

Match Officials Development. March 1, 2017

Match Officials Development. March 1, 2017 Match Officials Development March 1, 2017 Updated to reflect Leagues May 14, 2018 Contents Assignors Code of Ethics & Guidelines... 3 Assigning... 4 Cancelled Games... 4 Abandoned Games... 4 Appointments...

More information

FREE WITH THE SUNDAY NATION. May 3, 2009 W-DJ. Creating the DJ Brand

FREE WITH THE SUNDAY NATION. May 3, 2009 W-DJ. Creating the DJ Brand FREE WITH THE SUNDAY NATION May 3, 2009 W-DJ Creating the DJ Brand 2 Sunday May3 If you are a DJ and still do audio mixes, you need to up your game. The art of deejaying has gone a notch higher, in gospel

More information

PLAYBOOK FLAG FOOTBALL

PLAYBOOK FLAG FOOTBALL PLAYBOOK FLAG FOOTBALL SPREAD, TRIPS AND STACK American Development Model / 2017 Pilot TABLE OF CONTENTS 1 Introduction to Formations...4 2 Spread Right...5 i. Fils Right...5 ii. McDonald Left...5 iii.

More information

STOCK RETURN VOLATILITY AND COINTEGRATION OF U.S. AND ASIAN MARKETS IN ACCORDANCE WITH THE FINANCIAL CRISIS ( ) THESIS

STOCK RETURN VOLATILITY AND COINTEGRATION OF U.S. AND ASIAN MARKETS IN ACCORDANCE WITH THE FINANCIAL CRISIS ( ) THESIS STOCK RETURN VOLATILITY AND COINTEGRATION OF U.S. AND ASIAN MARKETS IN ACCORDANCE WITH THE FINANCIAL CRISIS (1997-2014) THESIS Presented as Partial Fulfillment of the Requirements For Degree of Sarjana

More information

USA Travel Sports 2019 World Series Information Packet

USA Travel Sports 2019 World Series Information Packet USA Travel Sports 2019 World Series Information Packet Important Deadlines Tournament Date: Schedules Published: Will be posted to the web site under SCHEDULES/SCORES Rosters Due in the Online System Login

More information

WAEC Sample Questions and Schemes - Uploaded online by GONJA (ELECTIVE)

WAEC Sample Questions and Schemes - Uploaded online by  GONJA (ELECTIVE) ) SCHEME OF EXAMINATION GONJA (ELECTIVE) There will be two papers, Papers 1 and 2, both of which must be taken. PAPER 1: Will test candidates language skill development. It will consist of four sections,

More information

REPUBLIC OF KENYA COUNTY GOVERNMENT OF KILIFI COUNTY PUBLIC SERVICE BOARD

REPUBLIC OF KENYA COUNTY GOVERNMENT OF KILIFI COUNTY PUBLIC SERVICE BOARD REPUBLIC OF KENYA COUNTY GOVERNMENT OF KILIFI COUNTY PUBLIC SERVICE BOARD APPLICANTS SHORTLISTED AND INVITED FOR INTERVIEWS FOR COUNTY ATTORNEY AND CHIEF OFFICER POSITIONS All persons shortlisted hereunder

More information

uṯēndi wa ja'fari bismillähi ar-rahmani ar-rahīmi

uṯēndi wa ja'fari bismillähi ar-rahmani ar-rahīmi ا ت ن د و ج ع ف ر uṯēndi wa ja'fari The Ballad of Ja'far ب س م الل ه الر حم ن الر ح ي م bismillähi ar-rahmani ar-rahīmi In the name of God, the Compassionate, the Merciful (١) ب س م ل ه ا و ل * پ و ك ا

More information

Game Fee & Assigning Protocol

Game Fee & Assigning Protocol 2016 The Ontario Soccer Association Match Officials Development Department Game Fee & Assigning Protocol This guide outlines the requirements that are in addition to the CSA Regulations for the Registration

More information

The competition: International open individual kata, kumite karate competition for children, youth, cadet, junior and adult categories.

The competition: International open individual kata, kumite karate competition for children, youth, cadet, junior and adult categories. Goju Cup 2015 The competition: International open individual kata, kumite karate competition for children, youth, cadet, junior and adult categories. Date of the competition: 03. October 2015 Saturday,

More information

SPORTS AUTHORITY OF INDIA NETAJI SUBHAS NATIONAL INSTITUTE OF SPORTS PATIALA SYLLABUS FOR DIPLOMA IN COACHING

SPORTS AUTHORITY OF INDIA NETAJI SUBHAS NATIONAL INSTITUTE OF SPORTS PATIALA SYLLABUS FOR DIPLOMA IN COACHING SPORTS AUTHORITY OF INDIA NETAJI SUBHAS NATIONAL INSTITUTE OF SPORTS PATIALA SYLLABUS FOR DIPLOMA IN COACHING JUDO SPORTS AUTHORITY OF INDIA NETAJI SUBHAS NATIONAL INSTITUTE OF SPORTS: PATIALA DIPLOMA

More information

International Triathlon Union (ITU) An Olympic distance competition (1.5km swim, 40km cycle, 10km run)

International Triathlon Union (ITU) An Olympic distance competition (1.5km swim, 40km cycle, 10km run) International Triathlon Union (ITU) EVENTS Men: Women: An Olympic distance competition (1.5km swim, 40km cycle, 10km run) An Olympic distance competition (1.5km swim, 40km cycle, 10km run) ATHLETE / NOC

More information

Female sitting dance with vocal accompaniment, Aceh CD572

Female sitting dance with vocal accompaniment, Aceh CD572 Female sitting dance with vocal accompaniment, Aceh CD572 Music transcribed by Helen Catanchin October 2011 CD572 Chapter 30, 22:02-25:27 (3:25 total) Notes: Musical accompaniment and dance motation for

More information

Pennington County 4-H Member s Record

Pennington County 4-H Member s Record Pennington County 4-H Member s Record Name : First Middle Last Home Address: Street City State Zip Code Home Phone Number:( ) - - Cell Phone Number: :( ) - - Boy: Girl: Birthday: Name of Parent (s) or

More information

7/01/10 UNITED STATES JUDO ASSOCIATION REFEREE CERTIFICATION PROGRAM

7/01/10 UNITED STATES JUDO ASSOCIATION REFEREE CERTIFICATION PROGRAM 7/01/10 UNITED STATES JUDO ASSOCIATION REFEREE CERTIFICATION PROGRAM I. Aim & Purpose of the United States Judo Association (USJA) Referee Certification Program: The aim of this referee certification program

More information

Name of Competition: Contest in Mathematical Linguistics within the Winter Mathematical Competitions. Area: Linguistics. Scale: National.

Name of Competition: Contest in Mathematical Linguistics within the Winter Mathematical Competitions. Area: Linguistics. Scale: National. Name of Competition: Contest in Mathematical Linguistics within the Winter Mathematical Competitions. Scale: National. Venue: Ruse or Pleven in even-numbered years, Varna or Burgas in odd-numbered years.

More information

walaka Ua Lohe Au Manu Kani Time for Sovereignty Kahikinui O Pu u Mähoe U i Läna i City Ike Au iä Kaho olawe always Hawaiian

walaka Ua Lohe Au Manu Kani Time for Sovereignty Kahikinui O Pu u Mähoe U i Läna i City Ike Au iä Kaho olawe always Hawaiian Ua Lohe Au Manu Kani Time for Sovereignty Kahikinui O Pu u Mähoe U i Läna i City Ike Au iä Kaho olawe always Hawaiian walaka Walaka Kanamu Walaka Kanamu Walaka Kanamu Walaka Kanamu Today we trample over

More information

Regis University Athletics 2018 Report on Athletic Program Participation and Financial Support Data

Regis University Athletics 2018 Report on Athletic Program Participation and Financial Support Data 2018 Rept on Athletic Program Participation and Financial Suppt Data Name of Repting Institution: Regis University Repting Year: May 1 st, 2017-April 30 th, 2018 Current Classification: NCAA Division II

More information

TELECOMMUNICATIONS DEMAND IN THEORY AND PRACTICE

TELECOMMUNICATIONS DEMAND IN THEORY AND PRACTICE TELECOMMUNICATIONS DEMAND IN THEORY AND PRACTICE by LESTER D. TAYLOR Department of Economics, University of Arizona, Tucson, Ariz,, U.S.A. KM *' '? il Щ V'Jf] KLUWER ACADEMIC PUBLISHERS DORDRECHT / BOSTON

More information

Human Strength Data Tables 10/24/06

Human Strength Data Tables 10/24/06 Push: Pushing forward in pounds on a round knob (59mm) at various heights using 1 preferred hand. Free posture is unrestricted. Standard posture has one foot 30 cm in front of the other and elbow at 90

More information

Tournamation. Fishing Tournament Automation Software. User Guide. Tournamation User Guide

Tournamation. Fishing Tournament Automation Software. User Guide. Tournamation User Guide Tournamation Fishing Tournament Automation Software User Guide Page 1 I. Introduction Tournamation is a Fishing Tournament Automation Software. The user may define the event, challenges, registration and

More information

Inkling Fan Language Character Encoding Version 0.3

Inkling Fan Language Character Encoding Version 0.3 Inkling Fan Language Character Encoding Version 0.3 What follows is a proposed encoding for the characters in the Inkling fan language for standardization among font creators. This encoding would make

More information

TOWN OF JACKPOT, NEVADA ADVISORY BOARD PUBLIC MEETING NOTICE

TOWN OF JACKPOT, NEVADA ADVISORY BOARD PUBLIC MEETING NOTICE 1594 POND DRIVE - JACKPOT, NV 89825 PHONE (775)755-2448, FAX (775)755-2439 PUBLIC MEETING NOTICE Board M Jesse Hof Theresa H Ed Komp Bruce Rir Jeff Youn Jackpot S Shawn Bu Brian Hu Rosalind The Town of

More information

Youth Progression Rules & Regulations

Youth Progression Rules & Regulations Youth Progression Rules & Regulations January 1 2018 The USTA Northern Youth Progression Pathway is a comprehensive and consistent, section-wide system for players from ages 7 through 10, which is easily

More information

Please refer to the ISAF website for the details of the submissions on this agenda/referred to in these minutes.

Please refer to the ISAF website   for the details of the submissions on this agenda/referred to in these minutes. Windsurfing & Kiteboarding Committee Agenda The Windsurfing & Kiteboarding Committee will meet at 09:30 13:30 hours on Sunday 4 November 2012 at the Royal St George Yacht Club, Dun Laoghaire, Dublin, Ireland

More information

TANZANIA BUREAU OF STANDARDS

TANZANIA BUREAU OF STANDARDS TANZANIA BUREAU OF STANDARDS PROCUREMENT PLAN FOR GOODS, NON-CONSULTANCY, CONSULTANCY SERVICES AND WORKS FOR FINANCIAL YEAR 2018-2019 S/n Description of the Procurement Tender No Lot No Procurement Method

More information

Acknowledgments...iii. Section 1: Introduction to /ILE... 1

Acknowledgments...iii. Section 1: Introduction to /ILE... 1 Contents Acknowledgments...iii Section 1: Introduction to /ILE... 1 Chapter 1: A High-Level Introduction to ILE... 3 The Organization of the Book... 4 What Is Was OPM?... 6 Problems with OPM... 6 What

More information

MARIBOR OPEN - 12 th Robi Rajh

MARIBOR OPEN - 12 th Robi Rajh MARIBOR OPEN - 12 th Robi Rajh - 2016 International Tournament in JU-JITSU, April 16 th and 17 th INVITATION Dear sport friends! Please find enclosed invitation to Maribor Open International Tournament

More information

MON GRADE PROMOTION SYLLABUS PERSONAL RECORD OF ACHIEVEMENT

MON GRADE PROMOTION SYLLABUS PERSONAL RECORD OF ACHIEVEMENT Novice - 1ST MON - FUNDAMENTAL SKILLS Ushiro-ukemi O-soto-otoshi Kesa-gatame Novice - 1ST MON - PERFORMANCE SKILLS Osoto-otoshi into Kesa-gatame Escape from Kesa-gatame by trapping Uke s Novice - 1ST MON

More information

VENTURA COUNTY AIR POLLUTION CONTROL BOARD

VENTURA COUNTY AIR POLLUTION CONTROL BOARD VENTURA COUNTY AIR POLLUTION CONTROL BOARD John C. Zaragoza Kathy I. Long Steve Bennett Mike Morgan Thomas Holden Brian Brennan Peter Foy Linda Parks Jonathan Sharkey Paul Miller Supervisor, District V

More information

Rules & Regulations on Membership Approved (January 28, 2017) a. Regular Members shall meet all requirements in the ASA By-Laws and the following;

Rules & Regulations on Membership Approved (January 28, 2017) a. Regular Members shall meet all requirements in the ASA By-Laws and the following; 1. Membership Requirements Rules & Regulations on Membership Approved (January 28, 2017) a. Regular Members shall meet all requirements in the ASA By-Laws and the following; i. Must file with the ASA annually

More information

UN Conference on Trade & Development (UNCTAD)

UN Conference on Trade & Development (UNCTAD) UN Conference on Trade & Development (UNCTAD) UNCTAD was founded in 1964 and is headquartered in Geneva. Sessions of UNCTAD are held about every four years. The Trade & Development Board governs between

More information

JUDOSCOTLAND GRADE PROMOTION SYLLABUS RECORD OF ACHIEVEMENT

JUDOSCOTLAND GRADE PROMOTION SYLLABUS RECORD OF ACHIEVEMENT Novice 6TH KYU - FUNDAMENTAL SKILLS Yoko-Ukemi Mae-Mawari-Ukemi (x3) Ushiro-ukemi O-soto-otoshi De-ashi-barai Uki-goshi Kesa-gatame Mune-gatame Kuzure-kesa-gatame Novice 6TH KYU - PERFORMANCE SKILLS Osoto-otoshi

More information

universities, which is at least an average grade of C+ in the Kenya Certificate of Secondary Education (KCSE).

universities, which is at least an average grade of C+ in the Kenya Certificate of Secondary Education (KCSE). Bachelor of technology in Institutional Catering and Accommodation Management The aim of this programme is to offer education and training in catering and institutional management and to equip the candidates

More information

Harlan County High School. Council Meeting Minutes. Regular Meeting. Principal Burkhart called the meeting to order at 3:40 pm.

Harlan County High School. Council Meeting Minutes. Regular Meeting. Principal Burkhart called the meeting to order at 3:40 pm. Harlan County High School SBDM Council Meeting Minutes Date: November 12 2015 Time: 3:15 pm Location: HCHS Media Center Regular Meeting I. Call Meeting to Order: Principal Burkhart called the meeting to

More information

KYU GRADE PROMOTION SYLLABUS PERSONAL RECORD OF ACHIEVEMENT

KYU GRADE PROMOTION SYLLABUS PERSONAL RECORD OF ACHIEVEMENT Novice 6TH KYU - FUNDAMENTAL SKILLS Ushiro-ukemi Yoko-Ukemi Mae-Mawari-Ukemi (x3) O-soto-otoshi De-ashi-barai Uki-goshi Kesa-gatame Mune-gatame Kuzure-kesa-gatame Novice 6TH KYU - PERFORMANCE SKILLS Osoto-otoshi

More information

2019 Football Canada Cup / U16 Challenge Out-of-Province Referee-In-Chief Expression of Interest

2019 Football Canada Cup / U16 Challenge Out-of-Province Referee-In-Chief Expression of Interest The CFOA has been entrusted with the responsibility of recommending suitable candidates for Football Canada Cup and U16 Challenge (East and West) RIC positions. The duties and required qualifications are

More information

BULLETIN

BULLETIN www.badminton2018.eu BULLETIN 21st to 28th July 2018 Dear EDSO Members, Deaflympic Committee of Slovakia has the honor to invite you to participate in the 1st Youth and 8th European Deaf Badminton Championships,

More information

4. Kindly submits your Enrolment Forms (Form A & Form B) ( preferable) and Non-Liability Forms (Snail-mail) to:-

4. Kindly submits your Enrolment Forms (Form A & Form B) ( preferable) and Non-Liability Forms (Snail-mail) to:- To: Affiliates of Malaysia Karate Federation Dear Sir, 28 th National Senior Karate Championship (2008) Ref : MGKF/SA/6/2008 Date : 30th. April 2008 On behalf of Malaysia Karate Federation (MAKAF), we

More information

INTERNATIONAL HOCKEY FEDERATION (FIH) Hockey

INTERNATIONAL HOCKEY FEDERATION (FIH) Hockey INTERNATIONAL HOCKEY FEDERATION (FIH) Hockey A. EVENTS (2) Men s Event (1) Women s Event (1) 12-team tournament 12-team tournament B. ATHLETES QUOTA 1. Total Quota for Hockey: Qualification Places Host

More information

CIRCLEVILLE BAND BOOSTER MEETING MINUTES

CIRCLEVILLE BAND BOOSTER MEETING MINUTES CIRCLEVILLE BAND BOOSTER MEETING March 5, 2018 @ 7:00 PM Meeting called to order by: Facilitator: Minutes prepared by: Officers Present: Others Present: JR Davis @ 7:15 p.m. JR Davis @ H.S. Library Tracy

More information

XXIII. Slovenian International Amateur Senior Men's Championship 2017

XXIII. Slovenian International Amateur Senior Men's Championship 2017 n Golf Association XXIII. n International Amateur Senior Men's Championship 2017 23 rd 25 th May 2017 I. Venue n International Senior Men s Amateur Championship 2017 II. Date 22 nd (practice round), 23

More information

Bokuto Ni Yoru Kendo Kihon Waza Keiko Ho

Bokuto Ni Yoru Kendo Kihon Waza Keiko Ho Bokuto Ni Yoru Kendo Kihon Waza Keiko Ho Basic Kendo Practice Methods Using a Bokuto Shikake Waza: Attack Initiation Techniques 1. Ippon Uchi no Waza (Single strike techniques) 2. Ni / San Dan no Waza

More information

REAL ESTATE DEVELOPMENT LAW

REAL ESTATE DEVELOPMENT LAW REAL ESTATE DEVELOPMENT LAW By Rick Daley Senior Lecturer in Law The Moritz College of Law at The Ohio State University Also available on Law School Exchange at: http://exchange.westlaw.com/ AMERICAN CASEBOOK

More information

Hawaii Judo Academy Gokyu Test

Hawaii Judo Academy Gokyu Test Hawaii Judo Academy Gokyu Test Name: Date: GENERAL INFORMATION Know the following information: 1. What is the name of you club? Hawaii Judo Academy 2. Name of Head Instructor? Takata 3. What is the name

More information

Faculty of Medicine Calendar for the Academic Year

Faculty of Medicine Calendar for the Academic Year Faculty of Medicine Calendar for the Academic Year 2018-2019 PHASE I CELL SCIENCES - I SUBJECT COMMITTEE Start Date October 08, 2018 End Date November 29, 2018 Exam Date November 30, 2018 CELL SCIENCES

More information

AU STATUTORY MEETINGS AND PARALLEL EVENTS From 25 June to 3 July 2018

AU STATUTORY MEETINGS AND PARALLEL EVENTS From 25 June to 3 July 2018 PROGRAMME OF EVENTS DURING THE PERIOD OF THE JUNE/JULY 2018 ASSEMBLY OF THE UNION NOUAKCHOTT, MAURITANIA As at 1 June 2018 AU STATUTORY MEETINGS AND PARALLEL EVENTS From 25 June to 3 July 2018 AU STATUTORY

More information

Ushiro-ukemi Yoko-Ukemi Mae-Mawari-Ukemi (x3) O-soto-otoshi De-ashi-barai Uki-goshi Kesa-gatame Mune-gatame Kuzure-kesa-gatame

Ushiro-ukemi Yoko-Ukemi Mae-Mawari-Ukemi (x3) O-soto-otoshi De-ashi-barai Uki-goshi Kesa-gatame Mune-gatame Kuzure-kesa-gatame Novice 6TH KYU - FUNDAMENTAL SKILLS Ushiro-ukemi Yoko-Ukemi Mae-Mawari-Ukemi (x3) O-soto-otoshi De-ashi-barai Uki-goshi Kesa-gatame Mune-gatame Kuzure-kesa-gatame Osoto-otoshi into Kesa-gatame De-ashi-barai

More information

Rebedon Farm. Rebecca McGregor STALLION CONTRACT GENERAL TERMS

Rebedon Farm. Rebecca McGregor STALLION CONTRACT GENERAL TERMS Rebedon Farm Rebecca McGregor 43 Colby Place, Phillipsburg NJ 08865 610-905-2851 beckypbb@hotmail.com STALLION CONTRACT GENERAL TERMS This contract, for the breeding season of 2012, is made and entered

More information

Modified Forms of Bowls for Fun

Modified Forms of Bowls for Fun i) Corner-to-Corner This is a fun way to keep people involved while waiting for an event to happen for example: the organised play to start or a meal. As most clubs always need extra funds, you could charge

More information

2018 WTA Future Stars Finals

2018 WTA Future Stars Finals 14U - Purple YAN-YI YANG [1] CHARLOTTE YEO MINSEO KIM KOMANG GINA KUSUMA DEWI TANG LOK SHU OPHELIA ANJALIKA KURERA [8] Sets Games Standings YAN-YI YANG [1] 6-0 6-1 6-3 6-0 THU THU 7-5 1-6 10-7 6-1 42-22

More information

ITF/CAT Southern African Junior Individual & Team s Championships & January 2019

ITF/CAT Southern African Junior Individual & Team s Championships & January 2019 ITF/CAT Southern African Junior Individual & Team s Championships 2019 07 10 & 11 15 January 2019 Organised by the Confederation of African Tennis (CAT) in conjunction with the International Tennis Federation

More information

DOUGLAS COFFEE COUNTY PARKS AND RECREATION 2019 (11 & 12) MIDGET LEAGUE BASKETBALL RULES AND REGULATIONS

DOUGLAS COFFEE COUNTY PARKS AND RECREATION 2019 (11 & 12) MIDGET LEAGUE BASKETBALL RULES AND REGULATIONS DOUGLAS COFFEE COUNTY PARKS AND RECREATION 2019 (11 & 12) MIDGET LEAGUE BASKETBALL RULES AND REGULATIONS I. REGISTRATION 1. All participants must have a birth certificate on file at DCCPRD, their registration

More information

Crusaders of Oklahoma Rugby Union Football Club Bylaws

Crusaders of Oklahoma Rugby Union Football Club Bylaws Crusaders of Oklahoma Rugby Union Football Club Bylaws Article I Organization Crusaders of Oklahoma Rugby Union Football Club was founded on June 1st, 2007. Article II Mission Statement The mission of

More information

P O Box NAKURU

P O Box NAKURU P O Box 478 0722-874095 NAKURU Email: ayrshiresociety@yahoo.com LIVESTOCK BREEDERS SHOW & SALE 2018 I. INTRODUCTION Dates: - 9 TH -11 TH August, 2018 Venue: - Jamhuri Park - Nairobi Organizers: - Representatives

More information

When Bad Things Happen to Good Property

When Bad Things Happen to Good Property When Bad Things Happen to Good Property Table of Contents Biographies...xi Foreword....xvii Chapter 1: Introduction Part I: Real Estate I. Did Something Bad Happen to Your Property?........ 1 II. Scope

More information

East Los Angeles College Inter- Club Council

East Los Angeles College Inter- Club Council East Los Angeles College Inter- Club Council ICC MINUTES MEETING Location: Edison Foyer Date: February 16 th, 2012 1301 Avenida Cesar Chavez Time: 12:15pm Monterey Park, Ca 91754 I. CALL TO ORDER Meeting

More information

Constitution and By- Laws. Article V. Officers and Committee Chairpersons. Article IX. Operating Policies and Procedures

Constitution and By- Laws. Article V. Officers and Committee Chairpersons. Article IX. Operating Policies and Procedures Highway 2 and 27 Exhibition Hockey League Constitution and By- Laws Article I. Name and Address Article II. Purpose Article III. Membership Article IV. Executive Board Article V. Officers and Committee

More information

European Fencing Confederation Confédération Européenne d Escrime

European Fencing Confederation Confédération Européenne d Escrime European Fencing Confederation Confédération Européenne d Escrime 28.05.2012 Information Letter no. 23-2012 Dear Member Federation, attached are our information for the Championships in Legnano. Please

More information

DUBLIN CITY ARCHIVES DCSA/13/1. Dublin City Sports Archive at Dublin City Archives

DUBLIN CITY ARCHIVES DCSA/13/1. Dublin City Sports Archive at Dublin City Archives DUBLIN CITY ARCHIVES DCSA/13/1 Irish Hockey Union Minutes Books (1898-1999) Dublin City Sports Archive at Dublin City Archives Catalogued by Diarmuid Francis Bolger, M.Phil Public History and Cultural

More information

All ingredients are on the TSCA inventory or comply with TSCA requirements

All ingredients are on the TSCA inventory or comply with TSCA requirements Silicone Art Materials ODORLESS SILICONE SOLVENT Material Safety Data Sheet page 1 I. PRODUCT AND COMPANY IDENTIFICATION Name On Label Silicone Art Materials ODORLESS SILICONE SOLVENT Manufacturer Tom

More information

The NJROTC Area Six Leadership Academy. Orienteering 201. Beyond the Cadet Field Manual

The NJROTC Area Six Leadership Academy. Orienteering 201. Beyond the Cadet Field Manual The NJROTC Area Six Leadership Academy Orienteering 201 Beyond the Cadet Field Manual XI. Host a Meet XII. Keep Learning I. Get Ready X. Analyze Your Performance II. Know the Rules IX. Use Course Strategy

More information

XXIV. Slovenian International Amateur Senior Men's Championship 2018

XXIV. Slovenian International Amateur Senior Men's Championship 2018 n Golf Association XXIV. n International Amateur Senior Men's Championship 2018 22 nd 24 th May 2018 I. Venue n International Senior Men s Amateur Championship 2018 II. Date 21 st (practice round, players

More information

Parking Control Bylaw Hearing and Deliberations and Alcohol Control Bylaw Deliberations

Parking Control Bylaw Hearing and Deliberations and Alcohol Control Bylaw Deliberations i i ii ii f - ii i i V E ii i ji L ii L Fx L J i I i i J i J ii IEF EXEUIVE i ii i - ii i f i i 4 3 44 6.i@..z ji -i 66 3 @x..z Fx 66 436.fx@x...z L J 66 4.@x...z ii 6 4.ii@x...z 6.@x...z x i 3 46 x.i@x...z

More information